Mzee mmoja alikuwa haudhurii misiba leo kafariki, kinachoendelea hapa naona ni msiba wa familia tu

Mzee mmoja alikuwa haudhurii misiba leo kafariki, kinachoendelea hapa naona ni msiba wa familia tu

Kwahiyo Wana nzengo mnamkomoa marehemu!
Nendeni mkamsitiri mwenzenu acheni mambo yenu hayo.
 
Juzi kati mtaani kulikuwa na msiba, mwili ukatolewa ndani tayari kwa safari ya kwenda kuzika kitongoji cha mbali. Kuna watu walitaka tule kwanza ila wengi wakasema haina haja ya kula, tukaenda kuzika bila kula. Tuliporudi kutoka mazikoni ndio tukapewa chakula. Chakula kikawa ni ugali kwa mboga za majani tu, wengine tukajitenga kula ugali kwani ugali tumekula nyumbani ya nini kula tena? Tuliambiwa kula msibani ni lazima usipokula na kwako hawaji kula utaachiwa vyakula ule mwenyewe kwa kuwa huwa huli kwenye misiba ya wenzako hivyo ni lazima ushiriki kula hata kama ni uji
😂😂😂

Kwan Kuna Sheria inasemaje kuhusu aina ya mapishi mazikoni?
 
Mzee mmoja amefariki na M/Mungu alimjaalia kweli enzi za uhai wake mali kweli kweli za kutosha, katika kujumuika na nzengo Mzee hakuwa na historia ya kuhudhuria misiba ya wengine na hata kushiriki tu hakuwa anafanya hivyo enzi za uhai wake kabisa na hakuwa anajali.

Sasa ya Mungu mengi bwana leo yeye ndio amefariki toka Jumatatu. Nyumbani kwake pamewekwa maturubai na ratiba ya mazishi ila hakuna watu.

Bahati mbaya hata watoto wake mke pia walimuiga tabia. Wapo wenyewe na ndugu majirani hakuna hata mmoja na watu hawana habari napo ni kama vile hakuna kitu vinaendelea pale kila mtu anaendelea na mambo yake.

Hii stori inakuja kufanana kidogo sana na hii yangu ambayo niliishugudia.

Hii imenikumbusha mwaka 2019 nilihudhuria msiba wa babu huko Musoma kijijini cha Nyabange Wilaya ya Butiama. Nzengo walikuja kama kawaida wakashughulika kila kitu wakaandaa, lilipofika suala la kula kile chakula wakaitana baadae nikaona kila mtu anaenda kwake, kila kitu walicho andaa walikiacha kama kilivyo tukabakia ndugu tu.

Wakasema, mjomba ambae ndio msiba ulikuwa umepangwa hakuwa anakula kwenye misiba na yeye alikuwa anachangia tu. Na mke wake alikuwa anakuja kupika na kuondoka kula hawali wala hawakai kwenye msiba wa nzengo. Waligoma kabisa, sasa chakula walichokuwa wameandaa nikama sisi ndugu tusingekimaliza hata kama tungekula siku 2 bado kingebaki kingi tu. Ikabidi ndugu waitane na wakaongee na wazee mjomba akapigwa faini ya mbuzi ndio wakaja kushiriki.

Toka hapo mjomba hajawahi kuacha kuhudhuria misiba anakwambia nilichokiona sikuile ni fedheha hata kama unauwezo ile ni mbaya sana.
Hata msipoenda atazikwa tu
 
Ila ni sawa tu maana wasioenda wamewapunguzia gharama wafiwa. Kama familia inajiweza kiasi hapo ni kununua tu jeneza, wakodi watu wachache wa kusaidia kuzika makaburini, siku imeisha.
Huwa tunacomplicate sana misiba
Ndio maana kuna umuhimu wa kuwepo na yale makampuni ya mazishi hata huku Tanzania.

Jamaa wanahandle kila kitu hadi mourners (watakaolia msibani)
 
Mzee mmoja amefariki na M/Mungu alimjaalia kweli enzi za uhai wake mali kweli kweli za kutosha, katika kujumuika na nzengo Mzee hakuwa na historia ya kuhudhuria misiba ya wengine na hata kushiriki tu hakuwa anafanya hivyo enzi za uhai wake kabisa na hakuwa anajali.
Nimefurahi kusikia aliwekeza kwa ajili ya familia yake,naona hao watatosha kumzika baba yao.
Haina maana unajiunga na vyama mia moja vya kufa na kuzikana lakini uwekezaji sifuri,siku mbili baada ya msiba mkeo anaanza kuhangaika ya nini?
 
Haya mambo naonaga ni ya kipumbavu tu na huchangiwa na ufukara. ..kwamba majiran wakija ndio atafufuka? Hii tabia ya kuona kua kila msiba uhudhurie hata kama haikuhusu ..
Mambo ya ya kizamani haya. Kipindi hicho watu walikuwa hawana shughuli za kufanya. Msiba watu walikuwa wanakesha wiki nzima kwa mfiwa. Mwanzisha thread andani hiyo familia ya huyo mzee imekomolewa? Sana sana hao majirani ndiyo wanahangaika kuchungulia mambo yasiyowahusu.
 
Mzee mmoja amefariki na M/Mungu alimjaalia kweli enzi za uhai wake mali kweli kweli za kutosha, katika kujumuika na nzengo Mzee hakuwa na historia ya kuhudhuria misiba ya wengine na hata kushiriki tu hakuwa anafanya hivyo enzi za uhai wake kabisa na hakuwa anajali.

Sasa ya Mungu mengi bwana leo yeye ndio amefariki toka Jumatatu. Nyumbani kwake pamewekwa maturubai na ratiba ya mazishi ila hakuna watu.

Bahati mbaya hata watoto wake mke pia walimuiga tabia. Wapo wenyewe na ndugu majirani hakuna hata mmoja na watu hawana habari napo ni kama vile hakuna kitu vinaendelea pale kila mtu anaendelea na mambo yake.

Hii stori inakuja kufanana kidogo sana na hii yangu ambayo niliishugudia.

Hii imenikumbusha mwaka 2019 nilihudhuria msiba wa babu huko Musoma kijijini cha Nyabange Wilaya ya Butiama. Nzengo walikuja kama kawaida wakashughulika kila kitu wakaandaa, lilipofika suala la kula kile chakula wakaitana baadae nikaona kila mtu anaenda kwake, kila kitu walicho andaa walikiacha kama kilivyo tukabakia ndugu tu.

Wakasema, mjomba ambae ndio msiba ulikuwa umepangwa hakuwa anakula kwenye misiba na yeye alikuwa anachangia tu. Na mke wake alikuwa anakuja kupika na kuondoka kula hawali wala hawakai kwenye msiba wa nzengo. Waligoma kabisa, sasa chakula walichokuwa wameandaa nikama sisi ndugu tusingekimaliza hata kama tungekula siku 2 bado kingebaki kingi tu. Ikabidi ndugu waitane na wakaongee na wazee mjomba akapigwa faini ya mbuzi ndio wakaja kushiriki.

Toka hapo mjomba hajawahi kuacha kuhudhuria misiba anakwambia nilichokiona sikuile ni fedheha hata kama unauwezo ile ni mbaya sana.
Ni ujinga tu na umaskini wetu. Watu vyakula wanakula kwa msharti hawali hovyo wanaishi kwa dozi. Nani anataka kufupisha maisha kisa watu wanalazimisha desturi? Halafu unakuta mzee alikuwa anajitoa kweli kwenye michango na kusaidia jamii ila anahukumiwa k2a kutokula. Kwanini hawakuwa wanakataa hata michango yake ili ajifunze akiwa hai?
 
Nimefurahi kusikia aliwekeza kwa ajili ya familia yake,naona hao watatosha kumzika baba yao.
Haina maana unajiunga na vyama mia moja vya kufa na kuzikana lakini uwekezaji sifuri,siku mbili baada ya msiba mkeo anaanza kuhangaika ya nini?
Hao watoto wanashindwa kujiongeza tu.
 
Mzee mmoja amefariki na M/Mungu alimjaalia kweli enzi za uhai wake mali kweli kweli za kutosha, katika kujumuika na nzengo Mzee hakuwa na historia ya kuhudhuria misiba ya wengine na hata kushiriki tu hakuwa anafanya hivyo enzi za uhai wake kabisa na hakuwa anajali.

Sasa ya Mungu mengi bwana leo yeye ndio amefariki toka Jumatatu. Nyumbani kwake pamewekwa maturubai na ratiba ya mazishi ila hakuna watu.

Bahati mbaya hata watoto wake mke pia walimuiga tabia. Wapo wenyewe na ndugu majirani hakuna hata mmoja na watu hawana habari napo ni kama vile hakuna kitu vinaendelea pale kila mtu anaendelea na mambo yake.

Hii stori inakuja kufanana kidogo sana na hii yangu ambayo niliishugudia.

Hii imenikumbusha mwaka 2019 nilihudhuria msiba wa babu huko Musoma kijijini cha Nyabange Wilaya ya Butiama. Nzengo walikuja kama kawaida wakashughulika kila kitu wakaandaa, lilipofika suala la kula kile chakula wakaitana baadae nikaona kila mtu anaenda kwake, kila kitu walicho andaa walikiacha kama kilivyo tukabakia ndugu tu.

Wakasema, mjomba ambae ndio msiba ulikuwa umepangwa hakuwa anakula kwenye misiba na yeye alikuwa anachangia tu. Na mke wake alikuwa anakuja kupika na kuondoka kula hawali wala hawakai kwenye msiba wa nzengo. Waligoma kabisa, sasa chakula walichokuwa wameandaa nikama sisi ndugu tusingekimaliza hata kama tungekula siku 2 bado kingebaki kingi tu. Ikabidi ndugu waitane na wakaongee na wazee mjomba akapigwa faini ya mbuzi ndio wakaja kushiriki.

Toka hapo mjomba hajawahi kuacha kuhudhuria misiba anakwambia nilichokiona sikuile ni fedheha hata kama unauwezo ile ni mbaya sana.

Yeye keshakufa hata msipomzika hakuna shida, issue ni ndugu zake nao wana Dhambi hiyo? Maana ndo mnawaadhibu!
 
Bunda kijana kafariki wazazi wanaishi huko, eti wakamzika tu ila hawawezi kusaidia familia kuandaa chakula eti marehemu hakuwa anafika msibani , eti mtu anaishi Dar msiba ukitokea awe anaenda kuzika, yaani mie nilichoka wale watu!
 
Siungi mkono watu kutojumuika na jamii,lakini jamii tujifunze kuna watu wapo busy ili wewe uishi vizuri.
upate umeme,maji ulinzi n.k
wasipokuona kwenye hiyo sijui nzengo yao wanaweka bifu
 
Back
Top Bottom