lukubuzo Samsis,
Luku...
Saigon tulianza kama Everton na jezi zetu rangi ya blue kama Everton ya Uingereza.
Tumezinunua Dar es Salaam Music and Sports Independence Avenue na no. tumetilisha kwa Fakrudin.
Umenikumbusha mbali sana udogo wangu.
Nyumbani mama anagomba natumia muda mwingi kucheza mpira kuliko kusoma.
Tuko Mnazi Mmoja mechi kali nikiangalia kushoto kwangu namuona "Guy" Gharib kulia namuona Jumanne Masimenti pembeni namuona Kodo nyuma nasikia sauti ya Chico Centre Back wetu yeye mpirani alikuwa akihamasisha kwa Kiingereza, ''On him..'' ''Score...'' nakumbuka kama jana hii ni 1966 sote ni watoto.
Nikivaa jezi no. 7.
Tulikuwa na coach...
Mpira unakwenda kwa kasi sana na coach anapiga kelele nje za kututia moto tuzidishe mashambulizi ...
Leo sisi ni wazee na hao niliowataja wametangulia mbele ya haki...
Leo bint yangu kanihimiza nifanye mazoezi asubuhi...
Sasa tuje katika haya maneno yako hapo chini:
"M.Said aka mzee wa
sago saigon ni mrongo kwa kujitungia
ufongo ili apate sapoti ya kidini huko madrasa na misikitini. Huyu mtu ni hatari ana ajenda ya ugaidi nyuma yake
wakian farid wa uamsho,serikali lazima itolee macho kwa huyu
gaid aliyejificha kwa mgongo wa dini.''
Nilikuwa nimekupuuza kwa maneno yako ya kipuuzi kuna wafuatiliaji wa darsa ninazotoa hapa hawa hawaandiki hapa wao ni wasomaji tu lakini wanawasiliana na mimi wengi wao wanajiita wanafunzi wangu,
Hawa baadhi toka jana usiku wamekuwa wakiniletea ujumbe kuwa nizungumze kuhusu hili sula la ugaidi ili tuepushe nyuzi tunazojadili hapa kuvurugwa na kuharibiwa na watu mfano wa wewe.
Kwanza nataka nikufahamishe kuwa serikali haikuhitaji wewe kuwapa taarifa zangu kwani mimi nafahamika kwingi khasa kwenye vyuo vikuu ambavyo vinasomesha African History na hii inatokana na uandishi wangu wa historia ya Tanganyika inayokwenda nyuma miaka 100.
Kitabu nilichoandika ni katika rejea muhimu na baadhi ya vyuo hivi nimealikwa kuazungumza.
Orodha ya magaidi wote dunia nzima iko Marekani na wao wameisambaza ulimwengu mzima pamoja na Tanzania.
Haya Wamarekani wamefanya baada ya 9/11.
Hawa magaidi watakamatwa popote duniani watakapoonekana.
Sasa nikufahamishe kuwa kuanzia mwaka wa 1998 nimekuwa kwa kipindi cha miaka 8 nikisafiri Afrika ya Mashariki kwa vipindi vifupi vifupi nikiingia Kenya na Uganda kwa likizo za shule ambako wanangu walikuwa wanasoma.
Nimesafiri kwenda Afrika ya Kusini, Swaziland, Nigeria, Ethiopia, Egypt, Germany, Holland, Switzerland, Dubai, Oman na Saudi Arabia na Marekani na nchi nyingine naingia zaidi ya mara moja.
Ili uingie nchi ya kigeni unahitaji visa na kuna nchi kabla ya kugongewa visa nchi hizi wanapeleka taarifa zako Marekani na kwengineko kutaka kujua kama umo katika orodha ya magaidi.
Naamini hili sasa umelifahamu.
Ama nimesikitika sana umewataja masheikh waliotuhumiwa kwa ugaidi ambao wako rumande sasa mwaka wa sita na ushahidi bado haujaweza kuletwa mahakamani wahukumiwe.
Umeniumiza sana roho yangu.
Hapa ningependa kukufahamisha kuwa hakuna hata Mtanzania mmoja ambae amepata kuhukumiwa kwa kosa la ugaidi.
Nakusihi sana ndugu yangu uache hizi fitna na upuuzi huu.
Najua unachomwa na historia hii niliyoandika kuhusu mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika lakini huu ndiyo ukweli ikiwa wazee wako hawakushiriki wala si jambo kubwa hivyo la kukuhangaisha wewe kwani isingewezekana kila mtu awemo.
Huna sababu ya kutukana watu kwa hili.
Sasa isiwe kwa kuwa nakushindeni kwa hoja mnakimbilia ''udini,'' ''ugaidi'' na maneno mengine ya kipuuzi.
Nakuwekea hapo chini mhadhara niliotoa Chuo Kikuu Cha Ibadan, Nigeria kuhusu ugaidi soma ili unifahamu zaidi isiwe unanijua kwa Saigon Club peke yake:
ISLAM, TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT 8 th – 10 th FEBRUARY 2006 Venue University of Ibadan Conference Centre ...
mohamedsaidsalum.blogspot.com