Mzee Mwinyi katika hili la kuongeza muda wa Asante kwa Rais Magufuli hapana, tunakukatalia kwa nguvu zetu zote

Mzee Mwinyi katika hili la kuongeza muda wa Asante kwa Rais Magufuli hapana, tunakukatalia kwa nguvu zetu zote

Mkuu mzee mwinyi ni 90+ years

Kweli atasoma hii kitu yote
 
Katiba sio sheria kutoka kwa Mungu na ndiyo maana kuna mabadiliko ya katiba.

Katiba inaweza kubadilishwa kukidhi haja ya wakati.
Mwinyi hatakiwi kulaumiwa kwani hayo yalikuwa ni maoni yake kama jinsi watu wengine walivyotoa maoni ya aina hiyohiyo na pia mpo nyie mnaotoa maoni kwamba katiba ibaki hivyo hivyo.

Yeye kaona wakati huu ni muafaka kubadilisha katiba ili Magufuli aendelee kwa miaka mitano zaidi. Kwa maoni yake, ni kama kumpa asante. Na Magufuli akamjibu palepale kwamba; " mbona wewe hukuongeza muda wako".

Basi nadhani, kutoa maoni ushauri sio dhambi, dhambi ni kumshambulia mtoa ushauri au maoni kitu ambacho ilitakiwa ajibiwe kwa hoja za kisiasa tu.
 
Ndio maana hata simwamini mtoto wake!
Yeye kwake kila kitu Ruksa!
 
Katiba sio sheria kutoka kwa Mungu na ndiyo maana kuna mabadiliko ya katiba.

Katiba inaweza kubadilishwa kukidhi haja ya wakati.
Mwinyi hatakiwi kulaumiwa kwani hayo yalikuwa ni maoni yake kama jinsi watu wengine walivyotoa maoni ya aina hiyohiyo na pia mpo nyie mnaotoa maoni kwamba katiba ibaki hivyo hivyo.

Yeye kaona wakati huu ni muafaka kubadilisha katiba ili Magufuli aendelee kwa miaka mitano zaidi. Kwa maoni yake, ni kama kumpa asante. Na Magufuli akamjibu palepale kwamba; " mbona wewe hukuongeza muda wako".

Basi nadhani, kutoa maoni ushauri sio dhambi, dhambi ni kumshambulia mtoa ushauri au maoni kitu ambacho ilitakiwa ajibiwe kwa hoja za kisiasa tu.
Shein aongozewe mitano tena ili mwanae asubirie kwanza
 
Niliwahi kushauri kuwa huyu mzee abaki Nyumbani acheze na wajukuu mambo ya Kumuweka kwenye majukwaa ya kisiasa ni kumdharirisha tu haya hemu tazama alichongea jana ni aibu tupu, mimi nasema wacha familia yake na yeye mwenyewe waendelee kukaza vichwa tu kuna siku mtu atafia kwenye High table
 
Sasa mjukuu unataka muda usiongezwe bila sababu za msingi..nakutonya tu kama Mungu atajaalia afya njema tutapiga piga kura ya kumuongeza muda.
Unajua kilichokua kikiendelea Rusia?. Wengi hawakuamini kilichotokea lakini leo putin ni mpaka 2036.
 
Sasa mjukuu unataka muda usiongezwe bila sababu za msingi..nakutonya tu kama Mungu atajaalia afya njema tutapiga piga kura ya kumuongeza muda.
Unajua kilichokua kikiendelea Rusia?. Wengi hawakuamini kilichotokea lakini leo putin ni mpaka 2036.

Unaweza kumuondolea mihula ili atawale tani yake lakini naye ni binadamu na ipo siku atakufa, hatoishi milele. Sasa unataka kweli marais watakaokuja nao watawale wafie madarakani?
Maana hiyo katiba utakayoiunda itarithiwa na mwingine na mwingine na mwingine.

Ukianza kubadili mihula, hiyo ndo itakuwa tabia ya watawala watakaofuata, nao watabadili tu, mwishowe nchi hii itatumbukia katika tawala za kidhalimu na wananchi watakuwa hawana namna zaidi ya kuchukua mtutu na kuingia msituni. Hii ndo aina ya nchi unayoitaka?
 
Ukiongoza Taifa la ndiyo ,goi goi nk ayo usiyashangae
 
Mzee wetu ana mengi na pale mlimani alisema jambo... baada ya jambo hilo alisoma alama za nyakati na ameshajua namna ya kuenenda na utawala huu ili siku zake ziishe vema.
Zingatia pia mgombea wa SMZ uchaguzi huu ni nani...
 
Ndio maana alizabwa kibao hadharani kwa ujinga Kama huu,huyu Mzee Ni kjinga Sana,hastahili heshima yoyote nchi hii.
Nyerere Baba la,Hakuna Kama Nyerere.Asingevumilia ujinga huu.
Nchi hii Haina wazee Tena wenye hekima.ni wachumia tumbo tumbo.
 
Mzee amesha piga hesabu, magu akijiongeza hata mitano mingine, inatasha mwanae kumaliza awamu zake Zanzibar aje achukue na bara. Ni malengo tu
Mzee anataka Magufuli apewe miaka mingine 5 kama asante. Kule Zanzibar mwanae Hussein Mwinyi atakuwa amemaliza kipindi cha pili. Watakuja na karata ni zamu ya Mzanzibar kupewa nafasi ya kugombea kupitia CCM!
Lakini Magufuli akimaliza 2025 kama katiba inavyosema. Mwanae hawezi kuwacha kugombea Zanzibar kipindi cha pili na kukimbilia kugombea uraisi wa Tanzania. Hataonekana ana tamaa na hatapata upinzani mkubwa sana!!
 
Unaweza kumuondolea mihula ili atawale tani yake lakini naye ni binadamu na ipo siku atakufa, hatoishi milele. Sasa unataka kweli marais watakaokuja nao watawale wafie madarakani?
Maana hiyo katiba utakayoiunda itarithiwa na mwingine na mwingine na mwingine.

Ukianza kubadili mihula, hiyo ndo itakuwa tabia ya watawala watakaofuata, nao watabadili tu, mwishowe nchi hii itatumbukia katika tawala za kidhalimu na wananchi watakuwa hawana namna zaidi ya kuchukua mtutu na kuingia msituni. Hii ndo aina ya nchi unayoitaka?

kATIBA ya nchi ni mkataba kati ya Watawala na Wataliwa. Kwa UMRI wake MWINYI ni INCOMPETENT hata ku- influence mabadiliko ya y akatiba. Nafurahi Mh Raisi alimtolea nje kiaina. Wazee kama hawa, wa aina hii, wa sampulii hii, ni LIABILITY kwa taifa. Wanastahili kupuuzwa kwa namna zote.
 
Shein aongozewe mitano tena ili mwanae asubirie kwanza


Hapa hatuzungumzii juu ya raisi ni nani!!---- Suala lililopo mezani ni; je wakati unaruhusu kubadili katiba ili kukudhi haja ya wakati??-- ni hapo Mzee Mwinyi ndipo alipokuwa anazungumzia kumuhusu Magufuli kuwa amefanya mambo makubwa kiasi kwamba inastahili katiba ibadilishwe ili aendelee kufanya makubwa zaidi. Hayo yalikuwa ni maoni na ushauri wake kama Raisi mstaafu na kama raia, sasa dhambi yake ipo wapi hapo??--- mbona hata wewe unapinga katiba kubadilishwa je na yeye akulaumu kwa kuifanya katiba kuwa ni sheria ya Mungu???, ni sheria ya Mungu tu ndiyo isiyoweza kubadilishwa na mwanadamu.
Sheria ya mwanadamu inabadilishwa na mwanadamu kukidhi haja ya wakati.

Itakuwa.ni ujinga kushikilia sheria zilizopitwa na wakati ilhali zinaweza kurekebishwa kukidhi haja ya wakati huo.

Mimi siungi mkono Magufuli kuongeza muda lakini sikubali Mwinyi alaumiwe kisa kutoa maoni yake.
 
Back
Top Bottom