Mzee Mwinyi katika hili la kuongeza muda wa Asante kwa Rais Magufuli hapana, tunakukatalia kwa nguvu zetu zote

Kafanya makubwa kwake na familia yake kwa kuipa maisha na sio kwetu tunaosemeshwa namba.
Hayo makubwa achilia propaganda yamesaidia nini kuboresha maisha ya walipa Kodi zaidi ya njaa na umasikini nchini baada ya kuuwa uchumi.
 
Akili kbwa hii, itakuwa kama Baba yake kwanza Zenj kisha anaingia Bara

Mzee amesha piga hesabu, magu akijiongeza hata mitano mingine, inatasha mwanae kumaliza awamu zake Zanzibar aje achukue na bara. Ni malengo tu
 
Katiba ni mali ya wananchi, pamoja na ukomo wanaweza kubadili kipengele kwa manufaa ya umma. Alichoanzisha JPM kitunzwe kwa nguvu zote.
 
Alisema mi5 ya Ahsante labda ya kumpa kijana nafasi
 


Mzee anataka mitano mingine ya "asante", Tangu lini urais ukatolewa kwa shukrani.
 
Katiba sio msaafu ,acha mambo ya ajabu we dogo,tutaibadilisha kulingana na mahitaji
 
Hii nchi kwa sasa, vijana shida....wazee shida. Kiukweli unafiki umeshika hatamu.
 
Naunga mkono JPM kuongezewa angalau miaka mitano.Akitawala miaka kumi na tano atatufikisha.
 
Mimi pia awali nilifikiria sana umuhimu wa kubadilisha katiba angalau kwa mazingira maalum ya Rais Magufuri kwa kazi ya kipekee na nzito aliyoifanya kwa muda mfupi na matokeo makubwa kuonekana. Maeneo yaliyonishawishi zaidi kuwa Rais anastahili kuongezwa angalau miaka 5 au 10 baada ya muda wake ni kupiga vita rushwa, ubadhirifu, na ufisadi ambao nchi nyingi za Afrika zimeshindwa. Pili uwezo wake wa uongozi na maono, tatu utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa kasi kubwa na kwa maslahi ya taifa na mipango kadhaa ya kiuchumi ambayo ni ya kihistoria mf Stiglers umeme, Kuhamia Dodoma , Ujenzi wa fly overs, REA. Na hatimaye kuingiza uchumi wa kati.Pamoja na changamoto alizopata za utekelezaji amesukumwa mno na utashi binafsi wa kisiasa. Siyo kitu rahisi kupata Rais mwingine wa aina hii tutakapokosea huko mbele baada ya muda wake kuisha itakuja kuwa majuto ni mjukuu. Pengine hata Mwalimu Nyerere angekuwa hai angeshauri aongezwe muda Rais wa sasa -who knows -kwa vile yule mzee alikuwa Pragmatist na mwenye maono ya mbali.Hivyo kama nchi kadhaa zilivyofanya mf China, Urusi kwa maslahi ya nchi zao zimebadilisha katiba zao na kuongeza muda wa maraisi sisi ni nani. Ni kweli Katiba siyo msahafu au biblia kwa hili la eneo la muda wa kuongoza linaweza kufanyika kwa KURA YA MAONI ya wananchi ambao ndiyo wenye nchi kuamua na kwa sababu maalum ya kimaslahi ya taifa. Iwapo hoja hii itashindikana basi maandalizi makubwa ya kuweka succession plan yafanywe kwa kumtambua mtu makini atayeingia viatu vya magufuri au katiba isukwe upya kulinda mafanikio yaliyopatikana na mifumo thabiti iwekwe kipindi hiki kutupeleka mbele.Nchi kama Marekani imeweza kuendelea na mfumo wa vipindi vya miaka miwili kutokana na mifumo yake imara na sera za kitaifa ambazo hazibadilishwi kwa upepo wa Rais. Hii inaweza kuwa option 2. Tunashauri Usalama wa Taifa waanze kazi ya kufanya utafiti na upekuzi maalum na wa kina hali itakavyokuwa baada ya Magufuri na nani mzalendo atatuvusha huko mbelena bila kusahau optios mbalimbali.Tukishindwa kuwa na Open program basi nakubaliana na wanaosema aongezwe muda huyu aliyepo baada ya miaka yake 10 Uongozi wa nchi haujaribiwi.
 
Umeandika gazeti dah, alie mponda kiatu yule mzee alikuwa na akili sana.

Kila mtu ashinde mechi zake kama ss wana simba, wengi wanawazia tu nafasi zao atakae kuja atawacha wawe walipo saivi,.

Njaa mbaya sana, Jiwe kafanya mazuri, ila yupo mmwingine atafanya mazuri zaidi,
 
Hofu yenu ni nini?, Mzee Mwinyi kuongea ni jambo moja lakini Bw John kimoyomoyo naye anasema "za kuambiwa ongeza na za kwako" muwe na imani.
 
Bahati nzuri hata Mh Rais kashasisitiza mara nyingi kuwa ataheshimu katiba
Labda hofu ya Watu ni vile ahadi ya kutokula inatolewa kabla ya kufika kwenye sherehe, tukikaribia na kusikia ile harufu ya pilau bado Mwenzetu atasema hali au atasema "nitaonja"?.
 
Mwinyi amejiaibisha sana kwa kauli yake hii, amejionesha utupu wake.

Mkapa alishakataza kuongeza muda, Magufuli akishakataa, Mwinyi anaonekana anajipendekeza kwa mtu badala ya kuangalia katiba.

Kwani Tanzania imekosa viongozi mpaka imtegemee mtu mmoja?

Yani Mwinyi kasahau maneno ya Nyerere kwamba kwa kufuata katiba hakuna mtu atakayekaa urais zaidi ya miaka 10?

Mwinyi kaona kitu gani kitakachotufanya tuvunje katiba kwa kumtegemea mtu mmoja?

Na tukivunja hivyo, kipi kitatuzuia tusivunje tena na kuifanya nchi iwe ya kifalme?

Mkapa alionya kwenye kitabu chake kuhusu hizi yabari, Mwinyi kasoma hata dondoo tu?

Mkapa on presidential term-limits
 
Bahati nzuri hata Mh Rais kashasisitiza mara nyingi kuwa ataheshimu katiba
Labda hofu ya Watu ni vile ahadi ya kutokula inatolewa kabla ya kufika kwenye sherehe, tukikaribia na kusikia ile harufu ya pilau bado Mwenzetu atasema hali au atasema "nitaonja"?.
 
Kama kafanya mazuri, huenda akaja atakayefanya mazuri zaidi.

Kama akina Kikwete wasingeheshimu katiba yeye angepatikana?

Na yeye aheshimu katiba ili tupate waliobora zaidi yake mapema!

Mwalimu alikuwa pragmatist, lakini hakuwa pragmatist kuruhusu mambo ya kipumbavu

Katiba huwa haitungwi kwa ajili ya mtu mmoja huwa inatungwa kwa ajili ya all weather ili siku akija rais mbovu isaidie kulinusuru Taifa dhidi ya ubovu wake na akija mzuri basi imsaidie kufanya uzuri wake to a maximum

Ukibadili katiba halafu akafa akaja mwingine mbovu, muuaji, mwizi, mshenzi, muuza nchi unataka naye atawale kwa katiba inayomruhusu kutawala mamihula yote hayo bila kikomo?

Ni ufinyu wa mawazo kudhani kama katiba ikibadirishwa basi huyo atakayekuja baada ya Magufuli hatoitumia katiba hiyohiyo au naye hatataka aibadili ili naye atawale mimiaka mingi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…