Mzee Mwinyi: Nyerere alitaka pawepo mgombea binafsi lakini CC ya CCM ilimkatalia, pia CCM ilipinga vyama kuungana ikihofia itakufa

Kuna haja Wenyenchi Tubadilike kwa Kumchagua MTU na sio chama!

Hata sasa watu wanachagua watu na Sio vyama, ila wanagombea kwa tiketi ya vyama. Watanzania asilimia 80 huchagua kwa ushabiki, rushwa, hofu, mazoea, kutegemea mgombea na sio sera. Ni watu wachache sana huchagua mtu kutokana na sera. Ilani za vyama sio ilani, bali ni orodha ya mahitaji yote ya wananchi, lakini utekelezaji ni utakachoona unaweza na utakavyo.
 
Mzee Mwinyi 'kakosea' sana kutoa siri za 'kilingeni' hadharan

Huu mtindo wa kuandika vitabu inabidi uchochowe kwa viongozi wote ikiwemo makamu wa marais, na mawaziri wakuu, iko siku mtu atakuja kutaja jinsi ccm inakaa madarakani kwa kubadilisha matokeo halisi.
 
Tuombe uzima, cha Jakaya kitakuwa na ladha yake kama hatoweka sana 'diplomasia' yake
Huu mtindo wa kuandika vitabu inabidi uchochowe kwa viongozi wote ikiwemo makamu wa marais, na mawaziri wakuu, iko siku mtu atakuja kutaja jinsi ccm inakaa madarakani kwa kubadilisha matokeo halisi.
 
Hivi vitendo vya Magufuli kama kuteka, kuua watu, kujeruhi, kupora pesa za watu, kupendelea Chato, kununua ndege nk kinyume cha sheria ya manunuzi zilikuwa ni sera za ccm?
 
Duh! Inaonekana uelewa wako ni mdogo sana!!
 
Viongozi wetu walifanya baadhi ya mambo mazuri lakini natilia shaka sana kama daima wamekuwa na dhamira njema. Naona ni kama wakati wote tumekuwa na viongozi ambao wapo kwaajili ya CCM.
 
We naye huna exposure..... Huu mfumo upo hta Uganda na Kenya hapo. Kinachotokea independent huwa ana lean mrengo fulani

Mfano Mohammed Ali wa jicho pevu, alikua independent aliyekua mrengo wa ODM/Odinga hivyo basi ana expect kura zake zitoke kwa wanachama wa ODM kwenye jimbo husika.

Hakuna independent anaye hang hewani..... Ni either uwe rulling party au opposition sema tu unakua huna chama kimakaratasi.
 
Kwani nchi zilizoruhusu mfumo huo endapo mgombea binafsi anashinda anatekeleza sera gani?hayo masera ndo yanayotukwamisha kwenda mbele.shida wabongo kila kitu tunaogopa.we don't like to risk our position,let's allow it.ccm ikifa kwani shida ni nn wabunge wenyewe ni wachumia tumbo tena ni wanafiki wakubwa,kauli zao kea Sasa ni tofauti kabisa na zile waliokuwa wanatoa wakati wa marehemu JPM
 
Hapa wewe ndio unachemka.

Katiba yetu inasema Waziri mkuu ndio mtendaji mkuu wa shughuli zote za Selikari na kama haitoshi ikasema waziri Waziri mkuu atatokana na chama chenye wabunge wengi bungeni

Kuhusu sera tunatakiwa kuwa na sera ya taifa ambayo kiongozi yeyote anatakiwa atekeleze hayo yalioainishwa kwenye sera kwanza.

Ifike mahali wagombea binafsi turuhusiwe maana sera za vyama ni za ovyo sana.

Sera za vyama ni kikwazo kwa maendeleo ya nchi hii maana wengi wanaangalia maslahi ya chama kuliko Taifa.

Angalia wazo kama hilo CCM ilikataa sio kwa sababu za kitaifa, usalama au kiuchumi ila kwasababu tu CCM itang'oka madarakani. Je CCM wamekataa mawazo mangapi mazuri kisa tu hayana maslahi kwa chama chao?
 
Mwinyi anajua ukweli kuwa CCM ipo hapo sababu ya dola
 
Kwani ivyo vyama viki shinda vina tekeleza sera ya nani?

Jibu ni Na yeye angekua na sera yake ambayo itakua ime fanya watu wa mchague
 
CCM ndiyo imeleta huu umaskini wa kutisha
 
Swali lilikuwa huyo mgombea binafsi akishinda atatekeleza sera gani?
Kwani lazima aweke maandishi ambayo hayatekelezeki ?

Katiba imeandikwa nataratibu mbalimbali zipo kwa maandishi lakini kila siku tunalalamika kwamba katiba haitekelezwi ?

Kwa nini iwe lazima kuwa na sera wakati hizo zilizoandikwa nyingi hazitekelezwi ?
Pili ugumu wa kufanya kazi akishinda.Mfano kashinda uraisi halafu wabunge wote wanatoka kwenye chama.Aweza pigiwa kura ya kutokuwa na imani naye wakati wowote na akatolewa madarakani.
Mkuu sidhani kama hii sheria ya kuwa na imani ingekuwepo laiti kama angepitishwa mgombea binafsi.

Na bila shaka hili la kuwa na imani ama kutokuwa na imani na raisi halikuwa rasmi kwamba ndo litakuwepo endapo angechaguliwa mgombea binafsi.

Maana yake ni kwamba unasema nyerere alichemka kupendekeza mgombea binafsi kwa kutumia kipengele ambacho hakikuwa rasmi kwamba kitumike kwa mgombea binafsi.

Hivyo kusema nyerere kachemka sio sawa.


.Pia aweza kwamishwa na walio wengi bungeni na kwenye watendaji
Shida yako unadhani kuwa huo utaratibu ungepita basi taratibu zingine zingebaki vilevile.

Unatakiwa uelewe kuwa taratibu zingebadilishwa.

Pengine lilipendekezwa hilo kwanza alafu lingekubaliwa ndo marekebisho mengine yangefuata.

Kwa maana hiyo unatakiwa uiwache kauli ya kusema nyerere alichemka wakati alipendekeza jambo ambalo lingekubaliwa ndipo mabadiliko ambayo unasema wewe maechemka ndo yangefanyika
 
Sasa kama kama mgombea binafsi sio rahisi kushinda, kwanini mnaogopa kuruhusu? Kwanini uogope kitu ambacho hakina madhara kwako?
 
Hapo Mzee Nyerere alichemka

Swali lilikuwa huyo mgombea binafsi akishinda atatekeleza sera gani? sababu hana sera yeyote anakuwa tu kama mlevi tu anayetoa tu ahadi hewa za majukwaani
Mpaka ifikie wananchi wanaamua kumoa urais ina maana kuna sera atakuwa ameziwasilisha kwa wananchi na wakazikubali. Pia kama nchi kuna uwezekano wa kuweka sera ambazo ni lazima kwa kila rais atakayebahatika kuwa madarakani kuzitekeleza. (mfano wa nchi ya Marekani)
 
kitabu hiki jana kimeharibu mechi ya simba na yanga na kuwatia watu hasara isiyoelezeka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…