TANZIA Mzee Paul Sozigwa, aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Mwalimu Julius Nyerere afariki Dunia

A
Aiseee.. MUNGU akuhurumie mzee binti ameuliza swali matokeo yako unatoa povu badala ya kumpa jibu sahihi
Msichana gani huyu mvivu wa kusoma. Hana haja ya kuuliza maswali ya kivivu, kwanini asingejipa muda wa kusoma hii post kwanza kabla ya kukurupuka kuuliza. Mwenye post kawaweka vitu vyote vya muhimu vinavyopunguza maswali ya aina hii.
 
Jazakallahu kheri,
 
Nchi hii ina dhuluma sana. Victoire niliwahi kusikia marehemu alikuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa RTD.

Kama mpaka anakufa alikuwa hajalipwa mafao yake basi tutegemee laana kwa hii nchi yetu.

Mzee amepumzika kwa Amani.
 
Nchi hii ina dhuluma sana. Victoire niliwahi kusikia marehemu alikuwa pia Mkurugenzi Mkuu wa RTD.

Yes Alikuwa Mkurugenzi and press secretary of the president. Alishika nafasi nzuri tu. Lakini hakufanya transition nzuri pale mfumo wa vyama vingi ulipoingia. Alibaki kwenye chama na hakuwa na cheo cha kuchaguliwa kama vile ubunge. Hivyo chamani walipomtosa hakuwa mshiko tena.
 
Reactions: BAK


Katika picha hii mtu aliye hai ni Rais Benjamin Mkapa tu! Wengine hao wengine wametutoka nakumbuka Habibu Harahara alikufa vibaya kwa kukatwa na panga la helikopta waliokuwa wamepanda yeye na Mwalimu Nyerere. Alikatwa na panga hilo kwa bahati mbaya nafikiri ilikuwa kama siyo Mtwara ni Lindi. Msiba wake ulisikitisha sana.
 
Sasa hiyo ni sifa nzuri?

Hapo cha kujifunza kuhusu uadilifu wa ujamaani ni kwamba utaishia kutembea na viatu vinachomoka soli kama Mzee Sozigwa.

Kambona alipinga hizi itikadi akakimbizwa na Nyerere.

Hawa Wazee walikuwa na Matumizi Mbaya ya Fedha na wakifulia wanasingizia Uadilifu,

Uadilifu sio lazima uhusishwe na Ukosefu wa Maarifa ya kupanga Mipango yako imara ya kiuchumi kabla ya kustaafu!

Walikuwa wanalipwa Mishahara na Marupurupu kadhaa Kama Watumishi wengine wengi tu!

Kama Sie Watumishi wa kawaida tu hatukuwa Wezi na hata tungetaka kuwa Wezi hatukuwa na cha kuiba lakin mbona tuliweza kujipanga vyema kabla ya kustaafu?

Hawa Wazee waliendekeza Nyumba zisizo rasmi na ndipo walipomalizia Fedha zote!

Alichanganyikiwa baada ya Mali zote kuporwa na Mpango wake wa kando ikiwemo Nyumba lakin Wasiojua wanahusisha na Siasa!

Huyu Alistaafu Muda mrefu kabla hata ya kuingia Jk Ikulu, kazi alizokuwa anafanya baada ya kustaafu kwake ni za Kisiasa sio kiutumishi ambazo hazina Pension!
 
Alikuwa na rais Mwinyi, si Nyerere. Walikwenda kuangalia hali kusini baada ya mafuriko.
 

Ilikuwa Wakati wa Alhaj Sheikh Ally Hassan Mwinyi, kilikuwa kihele hele cha kuwahi kupata Matukio ya Rais wakati anashuka kwny Ndege kabla ya kuangalia Usalama wake!
 
Kama mpaka anakufa alikuwa hajalipwa mafao yake basi tutegemee laana kwa hii nchi yetu.

Mzee amepumzika kwa Amani.
Nikionaga haya mambo yanawatokea watu waliolitumikia taifa na then serikali kupitia SSRA inazuia fao la kujitoa kule kwenye mashirika ya hifadhi ya jamii, nguvu hua zinanishiia kabisa. RIP Mzee Sozigwa
 
Poleni wafiwa. Nakumbuka huyu Mzee alikuwa msemaji sana ktk kipindi cha propaganda cha MAZUNGUMZO BAADA YA HABARI. Alikuwa anangea mafunbo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…