Mzungu hana rafiki, kapindua meza Kenya ipo siku atapindua meza Tanzania!

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Hakuna mtu alikuwa karibu na mzungu kama Raila, hakuna aliyekuwa ana ushawishi mbele ya mzungu hapa Afrika kama Raila mpaka hata walisema Obama ni cousin yake, lakini siku imefika na mzungu kapindua meza na Raila hatakiwi tena. Najua mtasema Ruto kashinda kidemokrasia lakini ukweli ni kwamba zmungu kabadilika na kaenda na Ruto.

Hata hapa TZ inakuja, mtampapatikia mzungu mnavyoweza, mtacheza Movie zote lakini siku moja atapindua meza na tutakayemuapisha mtashangaa na kutafuta pa kujifichia.

Endelezeni tu matusi na kejeli kwa sababu sasa hivi mzungu mko naye au mnaamini hivyo atleast siku moja mtashangaa kama Raila anavyoshangaa, anapiga simu hakuna anayepokea, hata Obama hapokei tena, siku inakuja, nchi yetu inarudi.

 
Watanzania kwa kujifanya wajuaji wa ndani
 
Reactions: RMC
Mimi maisha yote najua sisi wananchi wenye nchi ndio tunamchagua rais wa nchi. Kumbe kuna mzungu ndie anae tuchagulia rais😳
 
Hiyo sim yenyewe unayotumia kupost
Humu katengeneza mzungu.....

Ova
 
Huyu mzee kachoka sana sidhani kama ana uwezo wa kuongoza hata serikali ya mtaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
".....siku inakuja, nchi yetu inarudi, …"
Hizi kauli za kujipa matumaini bila mikakati hizi ni kujipa hatihati bure tu. Eti siku inakuja, inakuja lini? Kuna mikakati yo yote ya kuileta siku hiyo au ni kutandika tu kiibodi mitandaoni humu na kujiapiza?

Nchi yetu inarudi, inarudi kutoka wapi? Kwa mianasiasa hii ya Afrika hii inayoendeshwa na hao wazungu kama miroboti huku ikifisadika kupindukia ndiyo unawekeza matumaini yako kwayo? 😳😳😳
 
Mzungu ndio anapiga Kura? Wenzenu Kenya, Zambia na Malawi walisha jitambua nyie mmewekeza kwenye majungu, yaani investment kubwa ni ujinga na majungu
 
Huyo mzungu anaye sumbua Kenya ndio nani ? Na huyo mzungu atakaye wapa madaraka ninyi malaya wa kisiasa ni nani huyo ?
 
Mzungi tanzania hawezi kupindua. TZ kuna madini mengi na rasilimali nzuri kuliko Kenya.

Bado yupo sana na chama la wana.

Wakiamua ccm chali
 
Sasa mzungu akimchoka huyu akaungana na yule sisi tunafaidika nini? Merely utakuwa politicians maana ndio wanufaika wa madaraka hivyo unaomba mzungu awe upande wako ili ushike madaraka! Poor you!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…