Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

MUNGU YUPI SASA ALIWEKA HIZI SHERIA??????? MAANA KILA MUNGU WA KILA DINI ANA SHERIA ZAKE MKUU...
Hizi sheria, ni Designer Mkuu wa Universe ndo ameziweka, Kwa wanadamu ndo maana kwa Kila dini unaona sheria za maadili zinafanana maana Kila mtu amewekewa utashi wa kujua jema na mabaya.
Kuna kitu ukifanya unahisi msuto Fulani hivi ila ukizidi kufanya na kurudia ile aibu inakutoka sasa ile aibu ndo Muumba ameweka.
 
Ndo sio Sasa sheria za mtu. Haya Mimi Nina miaka 22 na demu wangu ana miaka 20. Tunafanya Mapenzi bila kucheat na tunatumia uzazi wa mpango. Haya kosa langu hapo Mimi Ni Nini.
Kosa lako litakuwa kumuacha.
Ukisoma vile vitabu vya Mwanzo vya Musa, mwanaume akifanya mapenzi na mwanamke bikra na akagundulika, anapaswa amuoe mwanamke huyo .
Pili kosa lako lingine ni kutumia uzazi wa Mpango, Designer Mkuu aliumba shahawa kwa ajili ya kupass genes from generation to generation Ili kizazi kisipotee, kufanya mapenzi kupitia condom unazuia mipango ya nature ya kuzaliana ,hilo ni kosa.
 
Mkuu naona uko vizuri, hasa upande wa dini yako (uislam).

Na kweli unavyosema, mimi huwa nasoma maandiko mengi na mengine hata siyo biblia wala Qur'an lakini ni yahusuyo tu imani.

Sasa nikuulize tena kitu kimoja, nitatumia mbinu gani kupima kuwa hiki kitabu ni cha kweli na hiki siyo (mfano kati ya Qur'an na biblia) na ukizingatia vyote vinamzingatia Mungu muumbaji ?

Na je, unaweza kunambia kati ya Biblia na Qur'an ni kipi kilianza kuwepo ?
Kipimo cha kutumia Ili kujua kitabu gani kimesema kweli ni akili yako tu., Yani ukivisoma vitabu hivyo viwili utagundua kipi kimesema kweli na kipi kimeongea uongo na kwenye hivyo vitabu viwili ukiona kitu hakiingii akiilini mfano concept ya utatu ukiona haiingii akilini basi ujue ni Uongo huo.

Injili(Biblia) ilianza kabla ya Qur'an na Qur'an yenyewe inatambua na kuheshimu hilo,..lakini hiyo hiyo Qur'an inasema kwamba Kuna baadhi ya watu waliamua kuuza Maneno ya Mungu kwa thamani ndogo ya maslahi yao kwenye Dunia, wakabadilisha baadhi ya mambo kwenye Hivyo vitabu vya mwanzo(Biblia) kabla ya Qur'an .... Mfano jiulize tu, Je concept ya Utatu mtakatifu imetoka kwa Mungu au watu wamejitungia?
 
ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.
Kwa maelezo yako ni kuwa hujaridhishwa na sifa anazopewa na wanadamu, ila wewe ni mwanadamu pia, una nafasi kwa kadri ulivyomjua Mungu kuumpa sifa unazoona zinamfaa.
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Siyo Hawa alikuwa dhaifu, ila binadamu wote ni dhaifu, hata Mungu aliyewaumba nadhani wanamjua kwa asilimia ndogo sana, kwahiyo usitegemee majibu makamilifu. Kwakuwa umeamini uwepo wake rekebisha matendo yako uendane naye kukwepa jehanamu. Ni yeye pekee anayejua kwanini aliumba viumbe dhaifu. Kingine jihadhari sana na shetani, alishuka na nguvu za kutosha, asikutumie kwa malengo yake.
 
Na ujumbe wa huyo Mungu mmoja huujui, hujui yupoje. Hujui anataka Nini, hujui atafanyaje, so usimpe sifa na sheria ambazo watu wa kale walimbunia.
So, umekubali na kuamini kwamba Kuna Mungu Mmoja Muumbaji?
 
Siyo Hawa alikuwa dhaifu, ila binadamu wote ni dhaifu, hata Mungu aliyewaumba nadhani wanamjua kwa asilimia ndogo sana, kwahiyo usitegemee majibu makamilifu. Kwakuwa umeamini uwepo wake rekebisha matendo yako uendane naye kukwepa jehanamu. Ni yeye pekee anayejua kwanini aliumba viumbe dhaifu. Kingine jihadhari sana na shetani, alishuka na nguvu za kutosha, asikutumie kwa malengo yake.
Hakuna ushahidi wala uthibitishobwowote kwamba kuna Mungu aliyewaumba watu.

Tena, huyo Mungu anayesemwa kawaumbwa Adam na Hawa, anaweza kuthibitishwa kimantiki kwamba hayupo.

Zaidi, wasomi wa Biblia walioisoma kwenye ma seminary na kuifundisha mpaka vyuo kama Harvard wanasema mnavyoisoma na ilivyo kiuhalisia ni vitu tofauti kabisa, huyo Adam hakuwahi kuwepo, huyo Hawa hakuwepo, hizo ni stories za mafumbo ya utamaduni wa Wayahudi tu watu wasioielewa Biblia wanazichukulia kama habari za kweli.
 
Hizi sheria, ni Designer Mkuu wa Universe ndo ameziweka, Kwa wanadamu ndo maana kwa Kila dini unaona sheria za maadili zinafanana maana Kila mtu amewekewa utashi wa kujua jema na mabaya.
Kuna kitu ukifanya unahisi msuto Fulani hivi ila ukizidi kufanya na kurudia ile aibu inakutoka sasa ile aibu ndo Muumba ameweka.
Acha uwongo Sheria hazifanani. Wengine wanakula nguruwe wengine hawali, wengine wake wanne wengine mmoja, wengine wavae magunia wengine wasivae. Hizi Ni sheria za watu. We unaweza ukakuta mchwa kwenye kichuguu ukawaambia wakuabudu na wafuate sheria zako au utawaunguza. Jua jinsi ulimwengu ulivyokuwa mkubwa sisi Ni Kama bacteria katika ulimwengu... Huyo muumbaji kwani ajali kuhusu bacteria wanajamianaje au wanavaaje.. Ina msaidia Nini yeye
 
Kosa lako litakuwa kumuacha.
Ukisoma vile vitabu vya Mwanzo vya Musa, mwanaume akifanya mapenzi na mwanamke bikra na akagundulika, anapaswa amuoe mwanamke huyo .
Pili kosa lako lingine ni kutumia uzazi wa Mpango, Designer Mkuu aliumba shahawa kwa ajili ya kupass genes from generation to generation Ili kizazi kisipotee, kufanya mapenzi kupitia condom unazuia mipango ya nature ya kuzaliana ,hilo ni kosa.
Turudi hapa.. Kama sex bila lengo la kuzaa Ni kuzini au kuuwa. Nieleze kwanini nature hiyo hiyo imempa mwanamke siku salama na zisizosalama, na nature hio hio imempa mwanamke tabia ya kuua yai kila mwezi. Hii inaonyesha kuwa vitabu hivi vimeandikwa na jamii isiyo na ujuzi wa Mambo ya kidunia. Na hizi sheria zimetungwa na watu wajinga wa kale.
 
Turudi hapa.. Kama sex bila lengo la kuzaa Ni kuzini au kuuwa. Nieleze kwanini nature hiyo hiyo imempa mwanamke siku salama na zisizosalama, na nature hio hio imempa mwanamke tabia ya kuua yai kila mwezi. Hii inaonyesha kuwa vitabu hivi vimeandikwa na jamii isiyo na ujuzi wa Mambo ya kidunia. Na hizi sheria zimetungwa na watu wajinga wa kale.
Sheria unazoziiita za watu wa kale ndiyo zilikua Bora compared na sheria zilizopo zama hizi... Sheria za siku hizi ndiyo zinaleta upuuzi wa haki za ushoga & Transgender na ujinga kama huo.
 
Mstari
Kwa hiyo turudi kule kule kwenye sayansi kuwa "In every action there is equal and opposite reaction" 🥱

Lakini mkuu kama Mungu ndiye alimfanya Lucifer kuwa shetani kwa nguvu zake mwenyewe basi kazi yake itakuwa haina maana.

Kwa sababu kwa muktadha wako wewe even now Mungu ndiye anae ku-control

Utende dhambi ama usitende,uende mbinguni ama jehanam, yaani kana kwamba sisi hatuna free will tena isipokuwa Mungu ndiye anakifsnyia wewe maamuzi kwa free will zake mwenyewe.

Kama nitakuwa nimekuelewa vizuri lakini.
Mstari
Kwa hiyo turudi kule kule kwenye sayansi kuwa "In every action there is equal and opposite reaction" 🥱

Lakini mkuu kama Mungu ndiye alimfanya Lucifer kuwa shetani kwa nguvu zake mwenyewe basi kazi yake itakuwa haina maana.

Kwa sababu kwa muktadha wako wewe even now Mungu ndiye anae ku-control

Utende dhambi ama usitende,uende mbinguni ama jehanam, yaani kana kwamba sisi hatuna free will tena isipokuwa Mungu ndiye anakifsnyia wewe maamuzi kwa free will zake mwenyewe.

Kama nitakuwa nimekuelewa vizuri lakini.
Hujanielewa vizuri kama ulivyohisi kwenye mstari wako wa mwisho. Soma swali la mtoa mada Kisha soma jibu langu. Kiufupi shetani hayuko na malaika mbinguni, huko alishafukuzwa na hana nguvu mbele ya Mungu kama mtoa mada anavyodhani. Nguvu ya shetani iko duniani anakojaribu kushawishi watu, nguvu yake ndio mtihani wa binadamu katika kumtukuza na kumjuwa Mungu. God doesn't control everything but He is capable of and can do that at His own will and convenience. Sasa nilitoa disclaimer kwamba we can't discuss God empirically but logically.
 
Zaidi, wasomi wa Biblia walioisoma kwenye ma seminary na kuifundisha mpaka vyuo kama Harvard wanasema mnavyoisoma na ilivyo kiuhalisia ni vitu tofauti kabisa, huyo Adam hakuwahi kuwepo, huyo Hawa hakuwepo
Hao wasomi wa Biblia toka seminary na kufundisha Havard walijuaje hayo? kutoka source ipi? kama unaweza share please?!
 
Hivi vyote Ni visingizio vya dini ili tusiulize maswali. Ni Bora kuwa na maswali ambayo Sina majibu kuliko majibu ambao siruhusiwi kuuliza maswali.
Twende taratibu ndugu SimbaMpole123 kama kweli umedhamilia kujifunza na kuelimika.
Kabla sijaendelea kukufafanulia naomba nkuulize swali dogo,

Unafahamu kuwa only jambo ambalo umeli experience via mind ndilo pekee unaweza kulielezea? You cannot explain something beyond your mind experience. Hilo jambo aidha uliliona kupitia macho,ama ulisikia kupitia masikio,ama ulionja kupitia ulimi ama uliguswa kupitia ngozi ama Kupitia pua.

Our mind experience, depends on our only five Senses ambazo nimezitaja hapo juu(Masikio,pua,ulimi,ngozi na Macho)

Tunapo sema our mind is limited,maana yake ni kwamba tunategemea experience kutoka kwenye Five senses ili ku develop our experience of life and perception of life..

Hivyo basi,kuna vitu hatuwezi kuviona kwa kutumia macho yetu ya kawaida kwa kutambua kuwa we are limited. tunajikuta tunatumia microscope kuangalia.

Kuna harufu hatuwezi kuzinusa kwa kutumia pua zetu, then tunamtumia mbwa kuwinda.. mifano ni mingi.
Ndipo tukasema kuwa our mind is limited.

Ili uwe na ufahamu wa hayo mambo, unahitaji kwenda beyond your five senses of human experience. Hapo ndipo kazi inaanzia.
 
Fuy3-pkWcAEp6Z8.jpeg


Iwafikie wale wote wanaopinga uwepo wa THE BEST DESIGNER/THE BEST CREATOR!.,
Human being is a work of art& engineering.... Yani Mtu alivyo tu inaonyesha kuna ufundi ambao umefanya mpaka ukaona mifumo yote kwenye mwili wa binadamu kuanzia:-
1. Respiratory system
2. Digestive system,
3. Circulatory System
4. Nervous System
5. Endocrine system
6. Muscular system
7. Skeletal system
8. Immune system
9. Urinary system
10. Reproductive system.


Yani, Ingetosha kabisa kuangalia mwili wako na jinsi unavyofanya kazi kujua kwamba kuna DESIGNER aliyeweka mifumo yote hiyo., Au kama unahisi mwili wa binadamu na jinsi unavyofanya kazi umejitokeza tu from nowhere, let's conclude that hata robots tunazoziona zimejitokeza tu from nowhere..... Does it make sense?
 
Back
Top Bottom