Mfano sio sahihi huu ndugu. Mtoto mdogo hafundishiki hivo kumtolea bomu ni sahihi. Ila teenager anaefundishika ukimpa options kukubali au kukataa ni uamuzi wake na hakuna unachoweza kufanya labda nd wale wazazi anampeleka mtoto jeshini. Lakini pia ukija kweny uhalisia kuna mchangiaji alitoa jibu zuri sana kuwa wewe unaweza ukawa na vision kuwa unaenda kazini unamgonga mtoto mdogo so ukajipa option kuwa basi siendi kazini ili niepushe hiyo ajali na ukawa sahihi kwa wakati huo. Ila vipi ukajua possiblity zote kama Mungu anavojua kuwa labda huyo mtoto ambae ungemgonga atakuja kuua wazazi wako baadae na watanzania wenzio wengi tu. Je usingeendelea na maamuzi ya kwenda kazini. Watu wa hollywood nawakubali hata utengenezaji wao wa movie wanasoma knowledge nyingi sana ila hupendelea knowledge ilioko kweny bible maan ni fikirishi sana. Kwa mfano kwenye movie ya avengers infinity war ni kwamba doctor strange alikuwa na uwezo wa kuamisha fight ya thanos kwenda universe nyingine badala ya duniani. Ila katika vision yake aliona katika vita zisizo na idadi dhidi ya adui humanity imeshinda mara moja na kwa conditions fulani so alichokifanya akaruhusu humanity iwe defeated pale wakanda sababu kuna conditions hazijawa met bado kusave time ili atengeneze nafasi ya ushindi time inayokuja(endgame) kwa kuwa itakuwa salama zaidi.Haya sio majibu ya Logic, hakuna logic bila reasoning na endapo uta reason tu mambo ya Imani utagundua kuwa huwezi kutoa majibu ya maana
Ni kwenye issue moja tu ndio binadamu wote waga wanafanana Akili haijarishi wana level gani ya Elimu, wametokea wapi,wamekulia wapi ni kwenye issue za DINI
Uongee na ambae hajasoma kabisa formal education,awe ameishia st 7,awe ni form four,awe ni Advance awe ni chuo kikuu wote awe professor wote wanakuwa katika level moja ya uelewa
Uwezo wa Ku reason unakuwa sawa kwa sababu muda huo kinachowaendesha ni hisia za uoga na Tamaa ya ku satisfy Desire walizonazo katika Maisha
Kwa lugha nyepesi vile Mungu anatuona Sisi ni kama vile tuwaonavyo watoto wadogo ambao bado hawana utambuzi, mtoto ambae popote alipo kuna 80% akafanya kitu ambacho hatakiwi kufanya
Kwa maana hiyo Mungu alijua fika kuwa Adamu atakula tunda alilowakataza, ila akaacha tu wale kwakuwa aliwaambia wasile, Alafu ili iweje?
Yani mfano una mtoto mdogo sehemu anayocheza kuna Bomu la kuzikwa Ardhini, wewe kama mzazi unapaswa kumwambia usicheze hapo kuna mabomu yalizikwa yanaweza kukulipukia au unapswa kuondoa Bomu kabisa hapo ili uhakikishe mtoto anakuwa sehemu salama?
Ukiamucha aendelee kucheza sehemu ya hatari na Bomu likamlipukia, ukaja kuulizwa ilikuaje ukamuacha hapo utajibu kuwa nilimpa options either aendelee kucheza hapo au aondoke ila yeye akaamua kuendelea kucheza hapo, hilo ni jibu la Logic au utaonekana Akili haziko sawa?