Naandika nikijua hasa nini kinaendelea. Makonda fanya haya usidhurike

Naandika nikijua hasa nini kinaendelea. Makonda fanya haya usidhurike

Hakika kikijitokeza chama kizuri cha Siasa chenye maono yanayogusa wengi kitajipatia wafuasi wa kutosha.

Bado kiu ya watanzania ni kubwa sana wengi wanakuja na kujinadi kwamba watakata kiu ya wananchi kumbe wanakata kiu yao binafsi na kufanya safari yetu Kuwa ndefu zaidi.
 
Mke wa Bashite ni mmeru na sasa wapo maeneo ya kwa msola njiro Arusha.

Eti rwanda 😂
By the way Bashite ameanza kupiga kelele kwasababu ameshapata taarifa kuwa file lake lipo kwenye final stage kabla halijafika kwa DPP.

NB: britanicca ungefanya citation kuwa huu uzi wako ni copy and paste kutoka Twitter kwa fbuyobe.
 
Ushauri kwako Makonda kunusuru maisha yako na familia yako!

Hama Nchi Kwa Muda watu uliowatesa ni wengi ila kwakuwa tumeambiwa samehe 7 mara 70 tumeshasamehe ila Kwa Usalama wako zaidi hamia Kwa Mkeo ukweni Rwanda Au Nenda Ulaya Kasome hata Miaka minne utarudi Tanzania hasira za wengi zikiwa zimetulia,


Kuna Mawili

Kuna Kupoteza maisha kutoka Kwa hao watesi

Au Kuna kufungwa Kabisa maana wapo wenye vielelezo vyote juu yako!

Najua a safari yako ya Kwenda ufaransa ilifeli Kwa kutokana na kigezo ulichoombea asylum haitafutwi hivyo!

Kuna mtu mmekaa wote kwenye gari Masaa 4 mbezi beach alitumwa Kwa kazi maalumu kukushauri baadhi ya mambo kuhusu wewe na Jamaa wa VX na wanachama wa mambo fulani ukaonekana kuogopa ila alivyoondoka ukashupaza shingo tena!

Mifumo Duniani kote ipo hata Kama Serikali ipo ….

Nakusihi tena usisahau kufuatilia hayo mambo ama by December 2023 tutakuja kusema habari nyingine Mdogo wangu ! Anza maisha upya nchi yeyote

Ukifika huko wala usihangaike nao uwawezi tena kwakuwa huna cheo!

Pia salimisha ile bastora umiliki wake haujahakikiwa


Britanicca
Du…kweli Makonda jua limemchwea!
Hata Riz alimtuhumu madawa ya kulevya!
Kibao kimegeuka.
Ataponaje?
 
Hata mm nilikuwa najiuliza kwann Ids ni zilezile kwa mambo yale yale?...Toka 2016 nijiunge rasmi humu ndani. Watu wanalipwa kumpambania mtu mtandaoni
Wanalipwa ndo maana kelele mingi, tunajuwa ukweli kuwa hao wapenda mabadiliko nao wana maboss ambao wako upande wa pili, hatuhangaiki tena.

Kwa ufupi upinzani ni ka genge ambako kqzi yake ni kuisaidia serikali kufanya mambo yake.

Lazima vikelele kelele viwepo.ndo nchi ibaenda.

Bure kabisa
 
We suffer more often in imagination than in reality - Seneca

Ifike mahali kama nchi tujaribu kukomaa na kuachana na hizi siasa mufilisi za kuviziana na kukomoana kama tuko Sicily au Colombia. Paul Makonda amefanya makosa mengi sana na ambayo yana ushahidi, hivyo apelekwe mahakamani ili liwe fundisho kwa wengine. Kutishia kumuua au kumtesa kisaiokolojia bila kufuata sheria ni kutengeneza tatizo jingine kubwa zaidi siku za mbeleni. Serikali isitumie rasilimali zake katika kufanikisha michezo kama hii ambayo haina manufaa kwa nchi.
Serikali ikichukua hatua mapema kumshitaki Makonda kwa matumizi mabaya ya madaraka, ndiyo pona yake.

Mtoa mada kasema kinaga ubaga, kuna wazito wanaoweza/kutaka kulipiza kisasi kwa waliyotendewa.
Wa kumuokoa Makonda ni serikali kumshitaki kisheria.
 
Zamani nilikuwa napenda sana comments zako. Naona bado bado ukogo vile vile ni mwana democrasia haswa.

Nilivyoendelea kukuwa nikajua wapuuzi tunao wapigia kelele na kuwa pigani humu mitandaoni na mitaani kumbe wanakula sahani moja na upande wa pili. Staki tena haya mambo ni ya kujiumiza bure bora nibaki katikati.

Sisi tunapiga kelele wao wanajali matumbo yao na familiya yao.

Ukiendelea kukua kuna siku utajua hiki nilichokiandika.
Tell her
 
Zamani nilikuwa napenda sana comments zako. Naona bado bado ukogo vile vile ni mwana democrasia haswa.

Nilivyoendelea kukuwa nikajua wapuuzi tunao wapigia kelele na kuwa pigani humu mitandaoni na mitaani kumbe wanakula sahani moja na upande wa pili. Staki tena haya mambo ni ya kujiumiza bure bora nibaki katikati.

Sisi tunapiga kelele wao wanajali matumbo yao na familiya yao.

Ukiendelea kukua kuna siku utajua hiki nilichokiandika.
Du mpaka sasa ulikuwa hujaelewa?
 
We suffer more often in imagination than in reality - Seneca

Ifike mahali kama nchi tujaribu kukomaa na kuachana na hizi siasa mufilisi za kuviziana na kukomoana kama tuko Sicily au Colombia. Paul Makonda amefanya makosa mengi sana na ambayo yana ushahidi, hivyo apelekwe mahakamani ili liwe fundisho kwa wengine. Kutishia kumuua au kumtesa kisaiokolojia bila kufuata sheria ni kutengeneza tatizo jingine kubwa zaidi siku za mbeleni. Serikali isitumie rasilimali zake katika kufanikisha michezo kama hii ambayo haina manufaa kwa nchi.
Ndg nikajuwa wanaowindwa kama swala v simba ni wa nje ya chama pendwa,kumbe hadi ndani kwa ndani!!.Kweli cheo ni mapambo ya muda ishi na watu vema.Maskini hafilisiki.
 
Angeenda hata Angola huko ama hata Congo tu kwa njia za panya si mshiko anao anakaaa huko hata miaka kumi anageuka huku watu wameshatulia sasa anapo kaaa watu wanamuona wanazidisha hasira.

Sent from my SM-M305F using JamiiForums mobile app
 
Mku huu ushauri ni mzuri sana.
Ila kubwa zaidi awaombe Watanzania Msamaha huu utamsaidia sana kwani tulio na huruma ni wengi.
Aombe msamaha kama aliowahi kuomba Rais Moi hili asipolifanya ninaamini atakuja kujutia wakati huo yuko Jela au la japokuwa simwombei hili limkute kabisa kwani ameshajifunza kuendana na mazingira au anayoyapitia aliyekuwa Mku wa Wilaya ya Hai
Makonda haruhusiwi kuingia US, kwa sababu ya "kuwanyima watu haki ya kuishi".

Muuaji mnamshauri akimbie bila ya kufikishwa mahakamani? Siungi mkono yeye kuviziwa mafichoni, lakini ni halali kabisa kwa yeye kukamatwa na kufikishwa mahakamani ili ajibu tuhuma dhidi yake.

Waliopo kwenye vyombo vya dola, wanaeleza kwamba mtu huyu aliongoza kikundi cha kuwateka, kuwaua na kuwapoteza watu waliokuwa wakimkosoa marehemu na serikali yake, na kwamba kikundi hicho kiliaminika na kupewa nguvu na marehemu kuliko taasisi rasmi ya TISS. Kikundi hiki kiliwajibika moja kwa moja kwa marehemu. Kikundi hiki, kwa kauli za Siro, zaidi kilifahamika kama "Watu Wasiojulikana", japo walikuwa wanajulikana.

Huyu ni vema akamatwe mapema, ajibu tuhuma dhidi yake, awataje watu wake aliokuwa akiwatumia kuendesha uharamia. Mmoja tunaambiwa yupo mahabusu kule Kusini mwa nchi kwa kosa la kumpora fedha mfanyabiashara na kisha kumwua.

Sabaya wakati akiwapora watu fedha kwa nguvu, alikuwa akiwaambia kuwa, hii inaitwa Makonda style! Sabaya naye ni shahidi muhimu dhidi ya Makonda.

Sanane kapotezwa
Azory kapotezwa
Kanguye kapotezwa
Lisu alimanusura
Mo alitekwa na kuachiwa
Roman alitekwa na kuachiwa
GSM waliporwa mamilioni ya pesa kwa vitisho mbalimbali
Mengi aliporwa mamia ya mamilioni kwa kudanganywa
Familia ya Chacha kule Mwanza waliporwa kiwanja Capripoint
Kuna watu wengine waliporwa fedha kwa ahadi kuwa ataongea na marehemu walegezewe kodi na wawe karibu na Serikali.

Makonda atendewe haki, asiviziwe mitaani, apelekwe mahakamani kama alivyofanyiwa Sabaya, akajibu tuhuma mbalimbali, ikiwemo za mauaji. Makonda ni mwovu mkubwa, kwa kiasi kikubwa, zaidi ya Sabaya. Mwanafunzi wake wa uovu, Sabaya, yupo jela, mwalimu wake yupo huru. Hii siyo haki.
 
Wanalipwa ndo maana kelele mingi, tunajuwa ukweli kuwa hao wapenda mabadiliko nao wana maboss ambao wako upande wa pili, hatuhangaiki tena.

Kwa ufupi upinzani ni ka genge ambako kqzi yake ni kuisaidia serikali kufanya mambo yake.

Lazima vikelele kelele viwepo.ndo nchi ibaenda.

Bure kabisa

hahahaha Mwenyekiti Mzee wa Saigon..
 
Back
Top Bottom