Nabii GeorDavie: Yesu akirudi leo atataka kutumia gari yangu na atataka nimfuate Airport

Nabii GeorDavie: Yesu akirudi leo atataka kutumia gari yangu na atataka nimfuate Airport

Nabii Geordavie amesema kwamba endapo Yesu angerudi leo, angehitaji kutumia gari lake na kumtaka amfuate uwanja wa ndege kwa ajili ya msafara wa hadhi yake. Nabii huyo alieleza kuwa Yesu angekuwa na mtazamo tofauti, akiamua kukaa naye na kuchagua gari miongoni mwa alizonazo ili kuendana na hadhi yake.

"Nadhani atakuwa na mtazamo tofauti, jambo la kwanza ataamua kukaa na mimi na atataka kutumia gari langu, atachagua katika hizi (gari) na ataomba nimfuate airport (uwanja wa ndege) kwasababu ndio hadhi yake na kutakuwa na msafara kabisa."
Huu ni moja ya mifano hai inayodhihirisha upungufu mkubwa wa akili kwa kila mtu/jamii inayowaamini hawa WENDAWAZIMU,na kukubali kuongozwa nao kiroho.
Sasa waone namna wanavyoongozwa KUMWABUDU na KUMTUMIKIA Shetani waziwazi.
 
Huyo atakuwa ni yesu wa mchongo. Huyu jamaa anamfanya Yesu kama msela tu, anaonesha jinsi asivyo na imani. Kumbe huduma yake ni abrakadabra tu anadang'anya wehu waliokusanyika kambini kwake wakimsikiliza na kumuamini kuwa ni nabii na mtume kumbe ni zuga tu
Atakuwa anamaanisha Yesu yule mchezaji wa kabumbu.
 

Nabii Geordavie​

Akili kubwa hii
Vilaza wafia dini hapo ni povu kwa kwenda mbele .....
 
Nabii Geordavie amesema kwamba endapo Yesu angerudi leo, angehitaji kutumia gari lake na kumtaka amfuate uwanja wa ndege kwa ajili ya msafara wa hadhi yake. Nabii huyo alieleza kuwa Yesu angekuwa na mtazamo tofauti, akiamua kukaa naye na kuchagua gari miongoni mwa alizonazo ili kuendana na hadhi yake.

"Nadhani atakuwa na mtazamo tofauti, jambo la kwanza ataamua kukaa na mimi na atataka kutumia gari langu, atachagua katika hizi (gari) na ataomba nimfuate airport (uwanja wa ndege) kwasababu ndio hadhi yake na kutakuwa na msafara kabisa."
Yaani nimesikiliza hayo maongezi huyo na bii ni tapeli asiye kuwa na shukurani . Anakula na kuvaa na kuendesha magari yanayo tokana na sadaka za mafukara huku akiwakejeri kuwa sadaka zao hazitoshi kununuwa kiatu chake. Hata maongezi yake hana mvuto kwa sababu ni fake kuanzia sauti mpaka kicheko. Halafu ni shamba anafikiri kutabiriwa na mzungu ndio ujaja. Pia uso wake na mikono yake utafikiri ni watu wailwili tafauti . Anatumia mkorogo?
 
Hawa manabii na mitume feki ni wapotoshaji sana wa imani kwa wasiojua vema neno la Mungu
 
Nabii Geordavie amesema kwamba endapo Yesu angerudi leo, angehitaji kutumia gari lake na kumtaka amfuate uwanja wa ndege kwa ajili ya msafara wa hadhi yake. Nabii huyo alieleza kuwa Yesu angekuwa na mtazamo tofauti, akiamua kukaa naye na kuchagua gari miongoni mwa alizonazo ili kuendana na hadhi yake.

"Nadhani atakuwa na mtazamo tofauti, jambo la kwanza ataamua kukaa na mimi na atataka kutumia gari langu, atachagua katika hizi (gari) na ataomba nimfuate airport (uwanja wa ndege) kwasababu ndio hadhi yake na kutakuwa na msafara kabisa."
Amini usiamini, anapata waumini!
 
Kwa kumsaidia tu Yesu alivaa kanzu sizani kama akija atavaa suti kama yeye,pili alifuga ndevu sizani kama akija atakuwa amenyoa stairi kama yeye, alisari kwa kusujudu yaani paji lake kugusa chini,sizani kama akija atakuwa anapiga makelele na kujisifia kama yeye, Sasa sijui Yesu ataenda kusali wapi?
Yesu yuaja katika utukufu mkuu kuhukumu ulimwengu. Kama unatarajia kumwona Yesu mwenye madevu; Yesu mvaa kanzu; Yesu mpiga paji la uso chini hadi kovu jeusi tii utasubiri sana. Mwapotea kwa kukosa ufahamu na maarifa.
 
kYesu yuaja katika utukufu mkuu kuhukumu ulimwengu. Kama unatarajia kumwona Yesu mwenye madevu; Yesu mvaa kanzu; Yesu mpiga paji la uso chini hadi kovu jeusi tii utasubiri sana. Mwapotea kwa kukosa ufahamu na maarifa.
kwa hiyo atakaporudi ataachana na Ibada aliyokuwa akiifanya hapo kabla halafu ataiga ibada za wazungu?au ataenda kusali na Viongozi wa dini wanaosapoti ndoa ya jinsia moja?mda mchache mambo mengi
 
Nabii Geordavie amesema kwamba endapo Yesu angerudi leo, angehitaji kutumia gari lake na kumtaka amfuate uwanja wa ndege kwa ajili ya msafara wa hadhi yake. Nabii huyo alieleza kuwa Yesu angekuwa na mtazamo tofauti, akiamua kukaa naye na kuchagua gari miongoni mwa alizonazo ili kuendana na hadhi yake.

"Nadhani atakuwa na mtazamo tofauti, jambo la kwanza ataamua kukaa na mimi na atataka kutumia gari langu, atachagua katika hizi (gari) na ataomba nimfuate airport (uwanja wa ndege) kwasababu ndio hadhi yake na kutakuwa na msafara kabisa."
Wandugu, ukisoma Mathayo 24, mstari wa 1-44, utagundua Yesu alieleza kwa kirefu sana majira yanayokaribia kuja kwake. kutokea kwa manabii wengi wa uongo, vita mahali mahali n.k, na kwamba kuja kwake kutakuwa kwa ghafla, kama umeme utokeavyo mashariki ukaonekana magharibi, ndivyo itakavyokuwa. Manabii wa uongo wapo wengi sana.

kuan watu hawaelewi jambo hili, hapa duniani tunatembea na wanadamu wengi tu ambao ni nusu mtu nusu shetani, walizaliwa hivyo, hao hata watubu vipi hawasamehewi kwa sababu walishahukumiwa, sehemu yao ni ktk ziwa la moto na baba yao shetani, na shetani anawatumia kama maajenti wake kufanya yale anayotaka dhidi ya kanisa. ndio maana wanaweza kufanya makufuru, kupotosha injili, kujitajirisha na kutapeli, wapo tu, walishatabiriwa.

Ndugu zangu, tujiandae, ujio wa Yesu hatakuja kama mwanzo,

MATENDO 1:11, Yesu alipokuwa anapaa mbele ya machi ya mitume wake, alikuwa anapaa kwenda mbinguni. Malaika walisimama karibu yao wakwaambia,. Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

Kama alivyopaa, ndovyo atakavyoshuka. hawezi kushuka akafikia airport akahitaji huyu mhubiri aje amchukue kwa gari yake iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
 
Back
Top Bottom