Nadhani mimi ndie mwanamke mwenye sifa mbaya kuliko wote JF

Linichome kwani lina shoti za umeme!
Kila siku nasoma biblia kuandaa mahubiri na sichomi ila ni bora utumie maneno yako yanaweza kiwa ya maana kuliko hayo unayodhani yananichoma

yakob 1:13-15

Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

ww umeshavutwa na kudanganywa na mwovu ibilisi shetani either kwa kujua au kwa kutokujua, tamaa yako uliyonayo ya kuwa atheist ikiishakuchukua mimba itazaa dhambi ya kumkufuru roho mtakatifu, na mwisho utapata mauti ya kiroho na hutafanikiwa kuurithi ule uzima wa milele, sikuhikumu ila nakuombea ulione hili jambo kwa jicho la kiroho na ubadilishe huo mtazamo wako..mm niishie hapa kwa leo...BWANA YESU ASIFIWE
 
Amen ila bado siamini mkuu🙏🏼
 
Reactions: 511
Mimi binafsi nimekuelewa mno na kaa hapo unapopaamini ila.........

UKweli usiosemwa sana na watu ni kuwa, karibia kila mtu ana wasiwasi na uwepo wa Mungu ila wengi wanashindwa kusema wanabaki wanagugumia nafsini mwao. Mbaya zaidi ni malezi na makuzi tuliyokulia kwa kuamini kuwa haitakiwi kuhoji juu ya yeye ila tusikilize na tuseme Amina!

Ila kiukweli kabisa kabisa, watu wana maswali mengi mnoo na shaka nyingi sana juu ya uwepo wake. Wanaogopa kukufuru
 
Umemaliza yote mkuu.
Ila ni suala la muda watu watajiweka wazi
 
Ana ndugu kwa baba yake mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…