Nadharia yangu namba 5 kwanini binadamu tumeumbwa duniani

Nadharia yangu namba 5 kwanini binadamu tumeumbwa duniani

Kwakua umeswma huiamin biblia basi hatuwez kukujibu tena ila kwa ufupi mungu ana jina na anataka tumwabudu na tunavyomwabudu tunampa sifa kwa wale wanaomzuhakimfano mzur ni kisa cha ayubu , uvumilivu na ustahimilivu ulimletea sifa mungu kwamba kuna binadamu wanao weza kumtegea hata wapatwe na nini
 
Nimekuwa nikisema mara nyingi kuwa sikubaliani na fundisho la Dini hizi( Abrahamic religion/ ukristu, uislamu, na Judaism) kuhusu sababu kwanini binadamu tumeumbwa duniani

Mafundisho ya Dini hizi yanasema bila aibu kwamba ; 👇👇👇👇

" Mwenyezi Mungu alituumba wanadamu ili tumuabudu"

Nikasema kuwa hoja hii ni ya kitoto sana Kwa sababu kwanza inakwenda kinyume kabisa na sifa za Mungu kama zilivyo andikwa kwenye Biblia, Qur'aan na Talmud.

Kwa mujibu wa mafundisho ya vitabu hivyo ni kwamba Mungu ni Mwanzo na Mwisho. Hana Mwanzo wala mwisho . Wala hafananishwi na kitu chochote Kile.

Amekamilika na anajitosheleza Kwa kila kitu.

So unaposema " Mungu ametuumba ili tumuabudu", tafsiri Yake ni kwamba unasema " Mungu na yeye ni muhitaji. Anahitaji kuabudiwa" Ndio maana wasio muabudu kwa mujibu wa mafundisho hayo watachomwa kwenye moto wa Jehanamu..


Nikawauliza mashekhe na wachungaji.

Okay mnasema Mungu ametuumba ili tumuabudu Je tusipo muabudu atapungukiwa na Nini? Wakajiuma uma wakasema " Hatopungukiwa na kitu"


Nikawauliza Tena " Je tukimuabudu Mungu kitu gani kitaongezeka kwake?

Jibu likawa . Hakuna kitu.

Then nikawauliza kama ndo hivyo Sasa Kwa Nini mnasema Mungu ametuumba ili tumuabudu?

Majibu yao ni vitisho vitisho tu vya kitoto.

Ila sijawalaumu Kwa sababu najua tofauti Kati ya Dini na sayansi katika suala zima la kutafuta majawabu ya maswali ambayo universe inatuuliza ni moja.

Religion is searching for the answers from the conclusion where are science is searching for the answers towards the conclusion.

Kwa mfano swali " Hivi Kwa Nini binadamu tupo duniani?"

Dini tayari imesha conclude kwamba tupo hapa Kwa ajili ya kumuabudu Mungu but science bado inatafuta majibu.

As u can see tayari Dini imekuweka kwenye corner ya " Tumeumbwa ili tumuabudu" So udadisi wako lazima Uwe revolved around " Tumeumbwa ili tumuabudu"

Uanze kutafuta dalili kwenye nature ambazo Zina suggest kwamba Mungu ametuumba ili tumuabudu. ( The nature does not suggest this )

Ukiniuliza nina fikiri ni Kwa Nini sisi tupo hapa duniani, jibu ambalo ni sahihi kuliko yote ni hili hapa chini👇👇👇👇👇

Anaejua sababu halisi Kwa Nini sisi wanadamu tupo hapa duniani ni yule aliye tuumba na kutuleta hapa duniani.


Hilo hapo juu ndio jibu sahihi kuliko yote juu ya swali kwanini binadamu tupo duniani.

However pamoja na usahihi wa jibu hilo hapo juu still bado sisi kama wanadamu tunalo jukumu la kutumia akili ambazo ametupa Mungu ili tujue ni sababu Gani hiyo ambayo imemfanya Mwenyezi Mungu atuumbe na kutuleta duniani...

As a matter of fact , dalili kwenye nature Zina suggest kwamba, aliye tuumba na kutuweka duniani amejificha na bado haja communicate chochote na sisi viumbe wake kujidhihirisha kwetu ila anataka sisi wenyewe tutumie akili ambazo ametupa kumjua yeye ni nani,kwanini ametuumba, jina lake halisi anaitwa nani( So far mpaka Sasa hakuna mwanadamu ambae analijua jina halisi la.Mwenyezi Mungu) etc.

Na hiki ndicho ninacho kifanya. So far tayari nimesha suggest nadharia kama 4 kwanini ninadhani sisi tumeletwa hapa duniani na Leo nina kuja na nadharia namba Tano ...

Stay tuned. Inakuja very soon
"still bado sisi kama wanadamu tunalo jukumu la kutumia akili ambazo ametupa Mungu ili tujue ni sababu Gani hiyo ambayo imemfanya Mwenyezi Mungu atuumbe na kutuleta duniani..."
NB:UKIACHA WENGE,SIYO MUDA UTAWAELEWA VIONGOZI WA DINI WALICHOKUJIBU. AKILI NYINGI,HUONDOA.....?
 
Kwakua umeswma huiamin biblia basi hatuwez kukujibu tena ila kwa ufupi mungu ana jina na anataka tumwabudu na tunavyomwabudu tunampa sifa kwa wale wanaomzuhakimfano mzur ni kisa cha ayubu , uvumilivu na ustahimilivu ulimletea sifa mungu kwamba kuna binadamu wanao weza kumtegea hata wapatwe na nini
Hakuna anae lijua jina la Mungu. Sidhani hata kama Malaika wanalijua jina lake
 
"still bado sisi kama wanadamu tunalo jukumu la kutumia akili ambazo ametupa Mungu ili tujue ni sababu Gani hiyo ambayo imemfanya Mwenyezi Mungu atuumbe na kutuleta duniani..."
NB:UKIACHA WENGE,SIYO MUDA UTAWAELEWA VIONGOZI WA DINI WALICHOKUJIBU. AKILI NYINGI,HUONDOA.....?
Hata hujasomeka
 
TUKIANGALIA ASILI YA MWANADAMU KUANZIA MWANZO KABISA.....
Mungu hakutuumba ili tuishi hapa Duniani bali alikusudia tuishi huko mbingu nyingine.
Kama umesoma dini "in details" utakuwa unafaham kuwa zipo mbingu (universe 7) na hii ya kwetu ikijumuisha Sayari zote ndio ya kwanza kabisa kutokea chini.
Sasa baada ya kuwa tumemkosea kupitia kwa baba yetu Adam, Mungu akaona atushushe huku mbingu ya chini kabisa kama sehemu ya Mtihani........TAMBUA KUWA, HAPA TUPO KWENYE CHUMBA CHA MTIHANI

Kwa wale watakaofaulu, wakitwaliwa watarudishwa ile mbingu aliyokuwa akiishi Adam na mkewe Hawa(kabla ya kushushwa Duniani) na wale watakaofeli basi watapata adhabu kali sana.
Na hii inaingia akilini kabisa kwani haiwezekani, haya majizi, wachawi, wanaotesa wengine bila sababu, wauaji nk nk yapite tu hivi hivi; Lazima kuna mahala haki itatolewa.....

Kwa bahati nzuri Mungu kwa upendo wake akatupa na "marking scheme" kabisa ambayo ni QURAN pia Torati, Zaburi na Injili/Biblia kwa vizazi vya nyuma; kazi kwetu, kufaulu mtihani
Nirudi kwenye mada; Ukiambiwa kusudi la kuletwa duniani ni kumuabudu Mungu...maana yake ni kuwa, Watu wakinyenyekea kwa Mungu, watafanya matendo aliyo yaamrisha (kuepuka Wizi, Uchawi, kupunja kwenye mizani, kupindisha sheria, Uasharati nk) na hivyo kufaulu mtihani.

HUWEZI KUSEMA UNA MUABUDU MUNGU HALAFU UNAFANYA MATENDO MACHAFU ALIYOYAKATAZA , HUKO NI KUUCHAFUA UTUKUFU WA MUNGU!

Kwa utalaam uliopo hapa duniani hadi sasa hatujaweza kuona huko nyuma ya Jua kuna nini, inamaana hata mbingu ya pili hatuna elimu nayo....
So unataka kusema Mungu hajui matokeo yetu kwenye mtihani wake? Kwa maana ya kwamba hajui kama tutafaulu ama tutafeli?
 
Kwa nini unahitimisha moja kwa moja kwamba tuliumbwa, wakati bado hauna uthibitisho huo?

Hivi wewe mwenyewe uliumbwa au ulizaliwa na wazazi wako?

Hakuna binadamu aliyeumbwa.

Binadamu hawaumbwi wala hawaletwi duniani.

Binadamu wanazaliwa duniani kupitia wazazi wao.
 
Kwa nini unahitimisha moja kwa moja kwamba tuliumbwa, wakati bado hauna uthibitisho huo?

Hivi wewe mwenyewe uliumbwa au ulizaliwa na wazazi wako?

Hakuna binadamu aliyeumbwa.

Binadamu hawaumbwi wala hawaletwi duniani.

Binadamu wanazaliwa duniani.
🙏🙏🙏🙏
 
Swali la kwanini Mungu alituumba ni swala la kuamini wala huwezi kutumia theory utafeli Bro, akili za Mungu hazichunguziki:
Kama akili za Mungu hazichunguziki, Wewe ulitumia akili gani kumchunguza huyo Mungu ukajua na kufahamu kwamba hachunguziki?

Ulijuaje kwamba Mungu hachunguziki?

Au uliambiwa na kuaminishwa tu hivyo?

Na wewe unataka kuaminisha watu wengine ulicho aminishwa.
Wewe shika tu:
Mungu alituumba ili tuwe na uhusiano wa karibu naye, kumtukuza, na kutimiza kusudi lake la kipekee kwa maisha yetu, kwa kuishi katika upendo na kutunza uumbaji wake.
Kwa nini unataka watu washike tu, badala ya kujua?
 
"still bado sisi kama wanadamu tunalo jukumu la kutumia akili ambazo ametupa Mungu
Una uthibitisho upi kwamba akili zetu tumepewa na Mungu?

Au unajaribu kufosi imani na mafundisho yako ya kidini tu?
ili tujue ni sababu Gani hiyo ambayo imemfanya Mwenyezi Mungu atuumbe na kutuleta duniani..."
Hakuna Mungu aliyeumba kitu chochote kile.

Mungu hayupo.

Huyo Mungu mmemtunga vichwani mwenu tu.

Binadamu hawaumbwi na wala hatukuumbwa.

Binadamu Tunazaliana sisi kwa sisi.

Binadamu wanazaliwa.
NB:UKIACHA WENGE,SIYO MUDA UTAWAELEWA VIONGOZI WA DINI WALICHOKUJIBU. AKILI NYINGI,HUONDOA.....?
 
Ili uwe mtihani, Mungu aliamua kutupa utashi wa kuamua wenyewe tufanye nini na tuache nini bila yeye kutulazimisha ILA kwa ajili ya upendo wake akaona atupe kabisa na guidelines ya nini anataka tufanye na nini hataki kupitia vitabu vitakatifu. Inamaana tutahukumiwa kwa kutumia guideline alizotoa.
Kusema anajua au hajui matokeo yetu...hilo silijibu kwa sasa....
Una amini kwamba Mungu anajua mambo yote kuhusu kila kitu yaliyopita yaliyopo na yajayo?
 
Kwa nini unahitimisha moja kwa moja kwamba tuliumbwa, wakati bado hauna uthibitisho huo?

Hivi wewe mwenyewe uliumbwa au ulizaliwa na wazazi wako?

Hakuna binadamu aliyeumbwa.

Binadamu hawaumbwi wala hawaletwi duniani.

Binadamu wanazaliwa duniani kupitia wazazi wao.
Binadamu tulitoka Wapi kama hatujaumbwa?
 
TUKIANGALIA ASILI YA MWANADAMU KUANZIA MWANZO KABISA.....
Mungu hakutuumba ili tuishi hapa Duniani bali alikusudia tuishi huko mbingu nyingine.
Kama umesoma dini "in details" utakuwa unafaham kuwa zipo mbingu (universe 7) na hii ya kwetu ikijumuisha Sayari zote ndio ya kwanza kabisa kutokea chini.
Sasa baada ya kuwa tumemkosea kupitia kwa baba yetu Adam, Mungu akaona atushushe huku mbingu ya chini kabisa kama sehemu ya Mtihani........TAMBUA KUWA, HAPA TUPO KWENYE CHUMBA CHA MTIHANI

Kwa wale watakaofaulu, wakitwaliwa watarudishwa ile mbingu aliyokuwa akiishi Adam na mkewe Hawa(kabla ya kushushwa Duniani) na wale watakaofeli basi watapata adhabu kali sana.
Na hii inaingia akilini kabisa kwani haiwezekani, haya majizi, wachawi, wanaotesa wengine bila sababu, wauaji nk nk yapite tu hivi hivi; Lazima kuna mahala haki itatolewa.....

Kwa bahati nzuri Mungu kwa upendo wake akatupa na "marking scheme" kabisa ambayo ni QURAN pia Torati, Zaburi na Injili/Biblia kwa vizazi vya nyuma; kazi kwetu, kufaulu mtihani
Nirudi kwenye mada; Ukiambiwa kusudi la kuletwa duniani ni kumuabudu Mungu...maana yake ni kuwa, Watu wakinyenyekea kwa Mungu, watafanya matendo aliyo yaamrisha (kuepuka Wizi, Uchawi, kupunja kwenye mizani, kupindisha sheria, Uasharati nk) na hivyo kufaulu mtihani.

HUWEZI KUSEMA UNA MUABUDU MUNGU HALAFU UNAFANYA MATENDO MACHAFU ALIYOYAKATAZA , HUKO NI KUUCHAFUA UTUKUFU WA MUNGU!

Kwa utalaam uliopo hapa duniani hadi sasa hatujaweza kuona huko nyuma ya Jua kuna nini, inamaana hata mbingu ya pili hatuna elimu nayo....
Duuh dhambi ya Eva na Adam bado inatuhusu hadi leo ila dhambi nyingine ni personal hii nayo inafikirisha sana
 
Binadamu wa kwanza mkuu alizaliwa na nani??,
Hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kila binadamu alizaliwa kutoka kwa mama yake, Na process hii ni endless to infinity...

Uwepo wa utofauti wa vinasaba DNA 🧬 unathibitisha kwamba hakuna binadamu wa kwanza kwa watu wote.

Uwepo wa utofauti wa rangi zetu Unathibitisha wazi kwamba hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kuna waafrika weusi, wazungu weupe, wahindi weupe, weusi. Kuna wajapan, wachina na wafilipino. Kuna wakorea, kuna waarabu n.k

Utofauti huu wa rangi ni uthibitisho tosha kwamba hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kama kungekuwa na binadamu wa kwanza duniani wa watu wote, Basi binadamu wote duniani tungefanana kwenye kila kitu. Kwanzia rangi zetu, DNA zetu na tabia zetu.

Pia kuna uwepo wa hali kama Albinism pia na magonjwa ya kurithi. Ni uthibitisho tosha kwamba hakuna binadamu wa kwanza.

Kwa sababu kama binadamu wa kwanza angekuwa na hali kama ya ualbino, Basi binadamu wote tungekuwa maalbino leo hii.

Lakini sivyo tuko tofauti na tuna tofautiana kwenye vitu vingi sana.

Hivyo hakuna binadamu wa kwanza duniani.
 
Hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kila binadamu alizaliwa kutoka kwa mama yake, Na process hii ni endless to infinity...

Uwepo wa utofauti wa vinasaba DNA 🧬 unathibitisha kwamba hakuna binadamu wa kwanza kwa watu wote.

Uwepo wa utofauti wa rangi zetu Unathibitisha wazi kwamba hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kuna waafrika weusi, wazungu weupe, wahindi weupe, weusi. Kuna wajapan, wachina na wafilipino. Kuna wakorea, kuna waarabu n.k

Utofauti huu wa rangi ni uthibitisho tosha kwamba hakuna binadamu wa kwanza duniani wa watu wote.

Kama kungekuwa na binadamu wa kwanza duniani wa watu wote, Basi binadamu wote duniani tungefanana kwenye kila kitu. Kwanzia rangi zetu, DNA zetu na tabia zetu.

Pia kuna uwepo wa hali kama Albinism pia na magonjwa ya kurithi. Ni uthibitisho tosha kwamba hakuna binadamu wa kwanza.

Kwa sababu kama binadamu wa kwanza angekuwa na hali kama ya ualbino, Basi binadamu wote tungekuwa maalbino leo hii.

Lakini sivyo tuko tofauti na tuna tofautiana kwenye vitu vingi sana.

Hivyo hakuna binadamu wa kwanza duniani.
Sasa binadamu ametokeaje duniani, nadhani ndio nadhalia ya mtoa mada ilipokuja ya kuumbwa.
 
Back
Top Bottom