Mhafidhina07
JF-Expert Member
- Aug 1, 2014
- 3,340
- 4,659
Nchi nyingi duniani zimepitia katika kandamizi za kimabavu za nchi nyenginezo (expansionism)) hii inatokana na kwamba mkataba wa mwanzo wa maisha ulikuwa unategemea sana vita (SURVIVE for war) nguvu zako katika vita zitakuhakikishia kutawaliwa au kutawala (State of Nature).
Nchi kama marekani, na Uchina ambazo ni nchi zenye uchumi mkubwa kwa sasa zimepitia shuruba hiyo lakini,zimefanikiwa kujitafuta na kuweza kusimama kama dola,lakini bado nchi zetu zinaendelea kushika mkia katika Kila nyanja kiasi ambacho nchi hizi hazijitambui kuwa zenyewe zinamamlaka na nguvu kama nchi kutokana na kwamba wanauza dola kwa maslahi na ujinga wa viongozi wetu.
Siwezi kuamini kabisa kuwa nchi ina miaka 50 bado inategemea kwa wamerekani kiasi cha kufika kuzarauliwa kwa kuambiwa ikubali ushoga na mengineyo, principle na kidunia zimeharibu mamlaka za dola hasa neno" Demokrasia" ambalo nchi nyingi kubwa imeianzisha kuendelea kuibaka Afrika kwa mlango wa Nyuma.
Ushauri
Nchi za Afrika zijitafakari na kukubali kuungana kupitia mawazo/nadharia za wapiganaji uhuru Kwame Nkurumah,Mandela na akina nyerere waliona kabisa Afrika itashindwa pakubwa itengenezwe Dola kama ya Marekani,japo viongozi wengi watanunulika lazima tuwe na mfumo mpya wa siasa tukiondoa wa sasa hivi.
Nchi kama marekani, na Uchina ambazo ni nchi zenye uchumi mkubwa kwa sasa zimepitia shuruba hiyo lakini,zimefanikiwa kujitafuta na kuweza kusimama kama dola,lakini bado nchi zetu zinaendelea kushika mkia katika Kila nyanja kiasi ambacho nchi hizi hazijitambui kuwa zenyewe zinamamlaka na nguvu kama nchi kutokana na kwamba wanauza dola kwa maslahi na ujinga wa viongozi wetu.
Siwezi kuamini kabisa kuwa nchi ina miaka 50 bado inategemea kwa wamerekani kiasi cha kufika kuzarauliwa kwa kuambiwa ikubali ushoga na mengineyo, principle na kidunia zimeharibu mamlaka za dola hasa neno" Demokrasia" ambalo nchi nyingi kubwa imeianzisha kuendelea kuibaka Afrika kwa mlango wa Nyuma.
Ushauri
Nchi za Afrika zijitafakari na kukubali kuungana kupitia mawazo/nadharia za wapiganaji uhuru Kwame Nkurumah,Mandela na akina nyerere waliona kabisa Afrika itashindwa pakubwa itengenezwe Dola kama ya Marekani,japo viongozi wengi watanunulika lazima tuwe na mfumo mpya wa siasa tukiondoa wa sasa hivi.