myoyambendi
JF-Expert Member
- Sep 13, 2013
- 166,767
- 705,461
Aisee..Siyo kwa ubaya ndugu zangu, misumari ni mingi sana, ukiweka japo kabiashara kako sehemu ili kakusaidie wewe na familia yako ikianza tu kuchanua kuna viherere wanajifanya kuizima.
Sasa nikasema dawa na mimi ni kutembea, simlogi mtu ila naweka mambo sawa, nailinda biashara yangu. Kwani kuna ubaya ndugu zangu?
SawasawaAcha tu nichelewe nibaki kwa Mungu... Mungu hana mashart...nitalala nitaamka kwa amani...nitaomba muda wote ajibu asijibu sawa tu.
Imani ya KRISTO ni yale yote aliyoamini KRISTO na aliyoamini kutoka kwa MUNGU ndio aliyoyafundisha.Hivi imani ya kristo ni ipi?
Jiandae kufa masikini dear!Acha tu nichelewe nibaki kwa Mungu... Mungu hana mashart...nitalala nitaamka kwa amani...nitaomba muda wote ajibu asijibu sawa tu.
Kwani hao wanaohidumu kuanzia pastor na wengine, nimeandika hao ndo tunaowategea na kuwaabudu?wanaohudumu huko makanisani nao ni binadamu tu kama huyosheikh au mganga yoyote wa kienyeji.
Jiandae kufa masikini dear!
Yani uishi kwa shida na uende motoni... Kwa uzinzi na unafki na uongo mfano tu sijamanisha wewe
Connection tafadhari.Mkuu huwezi kufanikiwa bila kujihusisha huko! So big up kwa kujitambua mapema!
Ila usimsahau Sana Mungu!
Yani kufanikiwa kwa uwezo wa Mungu kupo Ila unahitajika effort.
HAKUNA mtu ambae anapenda mafanikio yako!
Kuna mtaalamu katoka mwanza anaenda Oman mwezi ujao Ni hatari Sana..
Pia anauza majini ya kutafuta na kukutengenezea Bahati kwa gharama mdogo tu.
Changamka pambana kwenye ushirikina kujiimalisha mwenyewe na sio kumuumiza mtu.
Mtu akikuroga uvunjike mguuu wewe vunja kiuno
Maisha Ni kutafuta sio kutafutana
Kitendo cha kuja tu jukwaani ni kuwa haujiamini pamoja na ushirikina wako. Bahati mbaya unatafuta kuungwa mkono, na inapotokea unapingwa unajisikia vibaya. Kiufupi. Umechemka sana katika hilo.Kama wewe ungekuwa ni Mungu ndio umekomenti hii hakika ningeogopa kumbe ni binadamu tu kama mimi, Mungu afikirii kama unavyofikiria wewe, acha niendelee kuweka mambo yangu sawa simlogi mtu lakini, naweka mambo sawa binadamu wabaya sana.
Imani ya KRISTO ni yale yote aliyoamini KRISTO na aliyoamini kutoka kwa MUNGU ndio aliyoyafundisha.
Hivyo basi "imani ya KRISTO" ni yale yote aliyoyafundisha KRISTO na aliyoyaishi kwa vitendo. Ndiyo maana kwenye kitabu cha Ufunuo 14:12 utaona kuwa Watakatifu ni hao wazishikao Amri za MUNGU na imani ya KRISTO.
Kwa lugha nyepesi ni sawa na kusema, "watakatifu ni hao wazishikao Amri za MUNGU na mafundisho(imani) ya KRISTO.
YESU KRISTO aliwafundisha wanafunzi wake kile alichokiamini yeye. Na alichokiamini ni yale yote aliyoyasikia kwa BABA (MUNGU). Yohana 8:28-29
Hivyo ni vitu viwili tofauti.1 Yohana : 5 : 4 - Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.
1 Yohana : 5 : 5 - Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?
Hayo maandiko yana uhusiano na imani ya kristo?
Hivyo ni vitu viwili tofauti.
Nafikiri katika ile reply yangu ya kwanza nimekueleza ni nini maana ya "imani ya KRISTO". Hebu rudia tena kusoma kwa utulivu, utaelewa.Utofauti ni upi kaka?
Hivi Ni kibaraghashia au kibagarashia?mbona sielewi Tena?Huyo si Sheikh.
Sheikh hafundishi watu ulozi. Ni mchawi tu aliyevaa kanzu na baraghashia.
Hakuna Wala kosa Nini umesema hapaSiyo kwa ubaya ndugu zangu, misumari ni mingi sana, ukiweka japo kabiashara kako sehemu ili kakusaidie wewe na familia yako ikianza tu kuchanua kuna viherere wanajifanya kuizima.
Sasa nikasema dawa na mimi ni kutembea, simlogi mtu ila naweka mambo sawa, nailinda biashara yangu. Kwani kuna ubaya ndugu zangu?
Wewe ni mchokoziHivi Ni kibaraghashia au kibagarashia?mbona sielewi Tena?