Naenda Kanisani lakini naenda kwa Shekhe kuloga ili mambo yangu yaende sawa

Naenda Kanisani lakini naenda kwa Shekhe kuloga ili mambo yangu yaende sawa

Yer 17:5 SUV​

BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.

SI Mimi ni biblia ndio inasema hivyo.
Biblia ni kinywa Cha Mungu.
Mwenye neno na aseme neno Tena kwa ujasiri.
NENO LA MUNGU NI MOTO ULAO
Kwahiyo unavyomtegemea boss wako ambaye ni binadamu kama wewe umeshalaaniwa..??
 
Acha uendelee kuwa mtumwa wake,akihitaji kula kuku anachomoa waya tu anajua utarudi tu na ukifika anaconnect tena.....anakuvizia tena baada ya miezi kadhaa akiwa hana hela...... utakuwa mtumwa miaka nenda rudi
Mwache aangamie maana hana maarifa[emoji116]

HOSEA 4:6.
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.

Kashaingia kwenye maagano(mikataba) na shetani na kamwe hatakaa afanikiwe maishani.

Yani mganga wa kienyeji akitamani tu kuku wa kienyeji na pesa atakuwa anabonyeza tu kitufe cha jini mikosi limvae, itabidi aende kwa mganga wa kienyeji akachanjwe machale, kupewa mihirizi na kunyweshwa midawa ya kuzimu...[emoji847]
 
Mkuu kaweke vitu sawa,hao wanaokupinga hpa ni hatari,sana wengi wao wanashirki ngono ya kinyume na sehemu halali,pia nn wazinifu...bora ww mwenye nia ya kutaka kupiga hatua na ulishe familia yako kila la kheri.
Huo ndio ukweli
 
Ukiwa Mkristo kuna namna ya kuilinda biashara yako bila hata kwenda kwa Shekhe au mganga.

Iko hivi :
Mshirikishe BWANA MUNGU kwenye biashara yako kwa kumpa hisa au gawio la asilimia 10% tu kila mwezi kutoka kwenye faida unayopata.

Kwa kufanya hivyo moja kwa moja unakuwa umemfanya BWANA MUNGU kuwa mmiliki halali wa biashara yako hivyo akiwa kama mmiliki atailinda na kuibariki biashara yako.

Namna ya kumlipa BWANA MUNGU ni wewe kutoa "fungu la kumi" kanisani kwako kila mwezi na kwa uaminifu.

Angalizo :
  • hakikisha biashara yako ni halali kabisa na haina kona kona.
  • hakikisha unaishi kwa kuzishika Amri zote kumi za MUNGU na imani ya KRISTO.
(Mwanzo 14:18-20) (Mwanzo 28:20-22) Malachi 3:10-12
"Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi. Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema BWANA wa majeshi".

Hivi imani ya kristo ni ipi?
 
Ndugu yangu mpaka mapadre wanaendaga kuongeza materials kwa paleee vatcani kwa papa😃😃😃
 
Sijui kwanini hawakuelewi hawa jamaa [emoji23][emoji23]
Jamaa hawamuelewi , kimsingi mafungu yote ya biblia anayajua Ila ameamua kustep aside kimtindo , waajiriwa na watu wa mishahara hawawezi kuelewa intensity ya jamaa , ila wanaharakati wa mtaa exactly wanaelewa ni kivipi mwamba anatokota 😁😁😁 haya mambo acha kabisa
 
"Amelaaniwa amtegemeayae mwanadamu"

Haijalishi itachukua miaka mingapi ila unachokifanya Sasa kina implications zake, Utapata matokeo Yako unayoyatafuta.
wanaohudumu huko makanisani nao ni binadamu tu kama huyosheikh au mganga yoyote wa kienyeji.
 
Mkuu huwezi kufanikiwa bila kujihusisha huko! So big up kwa kujitambua mapema!

Ila usimsahau Sana Mungu!
Yani kufanikiwa kwa uwezo wa Mungu kupo Ila unahitajika effort.

HAKUNA mtu ambae anapenda mafanikio yako!
Kuna mtaalamu katoka mwanza anaenda Oman mwezi ujao Ni hatari Sana..

Pia anauza majini ya kutafuta na kukutengenezea Bahati kwa gharama mdogo tu.

Changamka pambana kwenye ushirikina kujiimalisha mwenyewe na sio kumuumiza mtu.

Mtu akikuroga uvunjike mguuu wewe vunja kiuno

Maisha Ni kutafuta sio kutafutana
 
Wewe unakwenda kuroga kwa wachawi, usitaje Masheikh. Wanaoroga ni wachawi. Na uchawi katika Uislam ni haramu.
 
Kuna mwingine huku mitaa ya kwetu..yeye anauza nyumba toka mwaka huu mwenzi wa tano..nyumba ipo eneo zuri tena mitaa ya vizito...... Toka atangaze mauzo wateja wameenda wengi tena wazito lakini bado hawajaafikiana.... Bei inacheza kwenye m 800 mpaka 700

Sasa kawaamishia waganga kwake eti nyumba imefungwa!!! Sasa mganga ana uwezo wa kumvuta mteja wa kufikia dau la m 800 kweli au? Naye mwenye nyumba anasema kama mtoa mada...akisha weka mambo sawa atarudi kanisani!!!
 
Kuna mwingine huku mitaa ya kwetu..yeye anauza nyumba toka mwaka huu mwenzi wa tano..nyumba ipo eneo zuri tena mitaa ya vizito...... Toka atangaze mauzo wateja wameenda wengi tena wazito lakini bado hawajaafikiana.... Bei inacheza kwenye m 800 mpaka 700

Sasa kawaamishia waganga kwake eti nyumba imefungwa!!! Sasa mganga ana uwezo wa kumvuta mteja wa kufikia dau la m 800 kweli au? Naye mwenye nyumba anasema kama mtoa mada...akisha weka mambo sawa atarudi kanisani!!!
Aise Yani Kuna Dawa hata akisema anauza hiyo nyumba 5B Kama mtu anayo anajikuta kapata tamaa na hamu ya kununua hiyo pesa
Kwa Tabora tunaita KIPANDE.
Hata muuzaji anaweza kuuza kitu kwa pesa ndogo hata aftatu
 
Hii ndo kwa namna gani!!
Mungu Hawai Wala hakawii...! Ukiamini katika Mungu Basi unatakiwa kuwa na sifa mbili.
Uvumulivu
Subira

Yani ili kuona God miracle unahitaji time frame....!! Na juhudi kubwa.

Ila Kama unataka overnight success Basi shetani ndio Habari ya mjini.... So usiwe mtu wa ushirikina Sana Yani kuwa mshirikina kwenye Mambo ya nyota na kipato....! Usimdhuru mtu
 
Aise Yani Kuna Dawa hata akisema anauza hiyo nyumba 5B Kama mtu anayo anajikuta kapata tamaa na hamu ya kununua hiyo pesa
Kwa Tabora tunaita KIPANDE.
Hata muuzaji anaweza kuuza kitu kwa pesa ndogo hata aftatu
Kwahiyo kumbe inawezekana!!! Haya ngoja tuone
 
Mungu Hawai Wala hakawii...! Ukiamini katika Mungu Basi unatakiwa kuwa na sifa mbili.
Uvumulivu
Subira

Yani ili kuona God miracle unahitaji time frame....!! Na juhudi kubwa.

Ila Kama unataka overnight success Basi shetani ndio Habari ya mjini.... So usiwe mtu wa ushirikina Sana Yani kuwa mshirikina kwenye Mambo ya nyota na kipato....! Usimdhuru mtu
Acha tu nichelewe nibaki kwa Mungu... Mungu hana mashart...nitalala nitaamka kwa amani...nitaomba muda wote ajibu asijibu sawa tu.
 
Back
Top Bottom