Kwa wale wa Mahina na Mhandu-Mwanza, nadhani asubuhi mliwaasili kwenye eneo la tukio, mlijiandikisha na wakaita majina 120 kwa leo saa 4asubuhi, 120 kesho na 120 keshokutwa, huku walimu wakiombewa wawe wa kwanza kufanya usahili kwakuwa wanasimamia mitihani.
Huo ulikuwa mpango wa siku tatu, yaani kuanzia leo 19 hadi 21 kwa makarani, lakini ilipotimia saa 8:30mchana iliingia meseji kutoka kwenye namba ya mtendaji ikinitaka niende kwenye usahili ilihali mimi nilikuwa nifanye jumatano.
Nilikuwa mbali baada ya kuruhusiwa kuondoka kwa wale tusiotakiwa kufanya usahili siku ya leo, mida ya saa 10 jioni niliamua nipite hapo eneo la tukio kujua huu wito unaochanganya.
Nilifika nikakuta hata wale 120 wa leo hawakufanya usahili, bali nilikuta kamati ya sensa ikiomba radhi kwa siku ya leo, hivyo usahili utakuwa kesho, huku wakisisitiza saa moja watu wawe eneo la tukio, kwa mahina watakuwa mahina sekondari na mhandu watakuwa nyakato B, primary, hivyo kama una ndugu yako mjulishe hilo badiliko.
Ila siyo waalimu, mtendaji, meya, wana watu wao, inasikitisha sana, nilisikia waalimu wakinung'unika kwamba itakuwaje, sisi tunasimamia mock(Mkuu tusaidie), Mtendaji akisema yule ni mdau wangu lazima hata apate ya ukarani apate hela hii ya sensa, Mwisho, uhalisia zoezi linasikitisha hasa kwenye kujuana, msiokuwa na watu nendeni mkajaribu bahati yenu.