Nafasi za Ajira za muda za Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

Vipi ikiwa waombaji wote kwenye kata husika wanamakosa hayo au asilimia kubwa wapo hivyo watatumia na nafasi zipo wazi vigezo gani vitatumika ?
Umemuuliza swali zuri sana, atuletee majibu hapa kuna watu wanajifanya wajuaji sana aisee, muda ndio utakao amua ipi mbivu na ipi mbichi?
 
Kuna watu utumbo umeakata taa
 
NBS wako nyuma ya muda lolote linaweza kutokea, tuache muda uamue.
 
Bakini nazo, si lazima.
 
Daah, hapo sasa nimeelewa
 
Kamisaa wa Sensa Anna Makinda, amesema baadhi ya Watanzania wanapenda uongo kutokana na maneno ya uzushi yanayozagaa mitandaoni kwamba majina ya wasimamizi wa sensa hayatoki kwa sababu wameweka watoto wao, na kusema majina yakitoka waombaji wote wenye sifa watachukuliwa.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 7, 2022, mkoani Katavi, wakati akizungumzia suala hilo la kutangazwa kwa majina ya wasimamizi wa sensa.

"Tanzania tunapenda sana uongo, eti wameweka watoto wao nani kawaambia tumeweka watoto wetu, bado majina hayajatoka sababu tunafanya kazi kwa umakini," amesema Kamisaa Makinda

Aidha Mama Makinda, amewatoa hofu waombaji kuwa wote wenye sifa watachukuliwa kutokana na uhitaji uliotangazwa na serikali,

"Watu laki mbili na elfu tano ndio wanaotakiwa kwa ajili ya kazi ya Sensa ila mpaka sasa tumepokea maombi zaidi ya laki sita,".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…