Asante mkuu kwa kunielewa usalama wa taifa wametanda kila mahali na hasa ukizingatia unyeti wa jambo hili la kitaifa...ngoja nikupe stori moja Mimi ilinitokea..Mimi NI mtumishi wa umma taasisi flan ya Kanda flan ikiwa chini ya wizara flan Sasa Kuna siku bhana moja ya wakala zetu wakatupa kazi tuwafanyie lengo pasu kwa pasu nadhani unaelewa mambo ya kufunga mwaka wa fedha,kosa nililofanya NI kumwambia TU rafiki yangu juu ya pesa ambayo ningeipata it was around 3 M.. huwezi amini rafiki yangu alilewa siku iliyofuata Mimi kwenda bar kumfuata ile kuniona TU kaanza kuropoka oya ndege week ijayo unapiga hela blah blah za kilevi unajua...kumbe usalama umetanda Sana huwezi amini jumatatu yake tulipata shida balaa Mara takukuru waje watukague mpk dakika ya mwisho kazi ikaingia nongwa na wakanionya Sana juu ya kutoa Siri za ofisi just imagine rafiki yangu kuropoka Tena sio bar kubwa NI kwenye ka grocery TU ndo maana nakwambia usichukulie poa kutoa Siri Kama hizi...nasema yote haya kwa kuwa umeweka picha yako katika avatar hivyo NI rahisi Sana wazee wa kitengo kupitia pitia Uzi huu na ukapata shida.