Nafasi za kazi Jeshi la Polisi Tanzania

Pamoja kaka....polisi kuna idara nyingi. Mkikaribia kumaliza mafunzo kamishen zinakuja kuchagua vijana wao...so mwisho wa siku unaweza ukaingia... Intel, au FFU, au forensic bureau(FB)...na zinginezo. Ila FB kwa polisi ndio naikubali sana
Mkuu tupe elimu kidogo kila uliyoitaja apo ukiacha ffu ambayo tunaijua
 
Pamoja kaka....polisi kuna idara nyingi. Mkikaribia kumaliza mafunzo kamishen zinakuja kuchagua vijana wao...so mwisho wa siku unaweza ukaingia... Intel, au FFU, au forensic bureau(FB)...na zinginezo. Ila FB kwa polisi ndio naikubali sana
Mzee tupe mauelewa ya kutosha..FB inakuaje kuaje
 
Tukipata kwann tuwanyime jamani
Kaka mambo yakifunguka huwa yanafunguka kweli kweli..kuna jamaa mmoja ni askari na pia anafanya kazi kwenye taasisi fulani ya umoja wa mataifa ..jamaa kule pia analipwa mchuzi mzuri tu na usisahau ana degree kazini anakula mchuzi wake mtamu


Mambo yakifunguka bwanaaa
 
Kweli mkuu,Tuombe kheri mkuu
 
Mkuu tupe elimu kidogo kila uliyoitaja apo ukiacha ffu ambayo tunaijua
Intel ni kifupi tu cha intelijensia- mambo ya upelelezi na hawa Mara nyingi huwakuti wakivaa gwanda...wao wanaishi kikawaida tu kukusanya taarifa zinazohusiana na mambo ya kihalifu. Huwa wana posho ya mavazi hawa coz kazi zao hawavai gwanda na hata ile low cut ya polisi na kunyoa ndevu wanaweza wasinyoe ili tu wasitambulike kirahisi.

FB ni forensic bureau ambao inahusiana na uchunguzi wa makosa ya jinai kwa njia za kisayansi. Huku utakuta wataalamu mbalimbali kama wa finger print, chemicals, sumu, wataalamu wa uchunguzi wa mabaki ya binadamu, wataalamu wa kugundua forgery na wengineo.

Idara ziko nyingi na zingine unapelekwa kutokana na taaluma
 
Mzee tupe mauelewa ya kutosha..FB inakuaje kuaje
FB ni Forensic bureau. Inajihusisha na uchunguzi wa makosa ya jinai kwa njia za kisayansi. Humu utakutana na watu wenye utaalamu mbalimbali. Wataalamu wa finger print, wataalamu wa milipuko na mabomu(ballistics), wataalamu wa kuchunguza mabaki ya mifupa( anthropologists), wataalamu wa kugundua forged documents, chemical and poison experts, doctors wa kudetermine the cause of deaths zenye utata...nakadhalika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…