Nafasi za kazi shambani Mufindi iringa. Mashamba ya Chai

Nafasi za kazi shambani Mufindi iringa. Mashamba ya Chai

Njoo Iringa kwenye machai. Tunza tiketi YA BASI nauli unarudishiwa ukifika.
1.nyumba bure
2.maji ya uhakika

Vigezo
1. Miaka 18+
2. Uwe na NIDA namba au cheti cha kuzaliwa au kadi ya mpiga kura au namba ya NSSF AU leseni ya udereva

Kazi ni kuchuma kipato ni kutokana na juhudi ya uvunaji lakni kuna kazi zingine za utunzaji wa mashamba ambazo ni sh 7,000/= kwa siku. Kazi ni saa moja kamili hadi saa nane mchana.

Kima cha chini cha mshahara ni 179,000/= kwa mwezi ila ukizidisha juhudi basi utapata zaidi ya hapo. Mimi mwenyewe ni shahidi maana nipo humuhumu shambani.
Hakuna rushwa yoyote na kazi uhakika.

Kampuni inaitwa Lipton teas and Infusion zamani Unilever.

Pm me na karibu sana.

Wanahitajika wafanyakazi kwa idadi yoyote hata mkiwa 20 nauli mnarudishiwa.
Mshahara wa 179,000/=,Kwa Maisha ya sasa ni Mdogo sana,huu ni unyonyaji.Sasa huyu atawezaje kumudu gharama za Maisha?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Yaani wachuma chai wa hayo maeneo ndiyo wamekuwa adimu kiasi cha kuja kutafuta wachuma chai wengine humu jukwaani!!

Au mtakuwa mnanyonya sana wachuma chai wazawa wa hayo maeneo, ambao miaka nenda wamekuwa wakifanya hiyo shughuli kwa uaminifu mkubwa! Na hivyo wameona bora wafanye shughuli zao binafsi!
Ndio hivyo mkuu,Yaani umegusa mle mle,Wachuma chai wananyonywa sana.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Mshahara wa 179,000/=,Kwa Maisha ya sasa ni Mdogo sana,huu ni unyonyaji.Sasa huyu atawezaje kumudu gharama za Maisha?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Kalime wewe hiyo chai halafu kauze uone bei utakayopata ndipo utajua huyu mleta tangazo anacholipa ni kama tu kusaidia jamiii tu

Tusiandikie mate Wakati wino upo kalime ,kavune mwenyewe chai Kisha ipeleke sokoni ndio uje na hizo theory zako Koko desktop writing

Ngoma uingie ucheze ndio utajua kalime
 
Mshahara wa 179,000/=,Kwa Maisha ya sasa ni Mdogo sana,huu ni unyonyaji.Sasa huyu atawezaje kumudu gharama za Maisha?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Maisha ya kule ni simple sana mkuu, kwa sababu utafikia kambini..
. Nyumba bure
. Umeme bure
. Maji bure....
. Hata mahitaji madogo madogo ukiwa huna hela kuna maduka ya kampuni, unakopa ikifika mwisho wa mwenzi unakatwa juu kwa juu.
. Mademu unajitegemea.. 🤒🤒.

Akili ndo inahitajika Zaidi, wengi wao wamezeekea kule, hata mia mbovu hawana.... Wanasubilia kufa tu.
 
Kuna watu hawajui kilimo kilivyo Hadi kuuza sokoni nashangaa Mtu anakebehi mshahara wa elfu saba Kwa siku mvuna chai
Kati kazi rahisi ukiifanya kwa wiki tu ni hiyo.

Na siku hizi wanatumia mashine, na chakula wanapewa, malazi unapewa.

Usipoendekeza anasa, unasave kipato chako ni rahisi kutoboa ukiwa huko. Labda kama utake kuishi mjini.
 
Mshahara wa 179,000/=,Kwa Maisha ya sasa ni Mdogo sana,huu ni unyonyaji.Sasa huyu atawezaje kumudu gharama za Maisha?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Ungejua Dunia ilivyo na ubepari ,viwanda Vingi wafanyakazi wanalipwa chini ya elfu 8 kwa siku na usipo kuwepo huna chako,ulizia viwanda vya MO au Wachina.
Kama n kweli wao wanajitahidi unless kazi n ngumu
 
Mbona mishahara kama anayolipa MO wafanyakazi wake? Yaani upo mkoa alafu unalipwa buku 7 kwa siku?
mkuu usiseme hvyo kuna watu wanatafuta kaz ya hata buku 5 kwa siku hawapati.nimewaambia nillpo hapa watu kuna kaz mufindi sahv nasumbuliwa sna.ningemwomba jamaa mawasiliano yake ili waende.mm pm yangu inazingua haifungiki ningemtumia pm
 
Kati kazi rahisi ukiifanya kwa wiki tu ni hiyo.

Na siku hizi wanatumia mashine, na chakula wanapewa, malazi unapewa.

Usipoendekeza anasa, unasave kipato chako ni rahisi kutoboa ukiwa huko. Labda kama utake kuishi mjini.
mkuu Kuna jamaa zangu wanahitaji wananisumbua sna naombeni conection yenu ili niwaelekeze waje.km hamtajali mnicheki kwa namba 0752317974.
 
Si tulikubaliana JF kila mtu ni tajiri kazi za kuvuna chai za nini sasa humu[emoji849]
 
mkuu Kuna jamaa zangu wanahitaji wananisumbua sna naombeni conection yenu ili niwaelekeze waje.km hamtajali mnicheki kwa namba 0752317974.
Mbona mleta uzi kabwaga manyanga hapo mkuu.
Fuata maelekezo yake, mfate PM.
 
mkuu usiseme hvyo kuna watu wanatafuta kaz ya hata buku 5 kwa siku hawapati.nimewaambia nillpo hapa watu kuna kaz mufindi sahv nasumbuliwa sna.ningemwomba jamaa mawasiliano yake ili waende.mm pm yangu inazingua haifungiki ningemtumia pm
Nachozungumzia hapa kwamba jamaa anawalalia wafanyakazi,lipa mishahara ambayo ina mantic kulingana na mazingira.
 
Mbona mishahara kama anayolipa MO wafanyakazi wake? Yaani upo mkoa alafu unalipwa buku 7 kwa siku?
Tena wengi wa dar pale ni buku 4!
Wambieni watu wenye shida na kazi hiyo ni fursa….kulipwa 7000 uko iringa inalipa zaidi kuliko uku dar…..

Watu wenye shida ya kazi na wasio wavivu hiyo ndio fursa sasa
 
Back
Top Bottom