Nafikiri hii ndiyo sababu ya matajiri kuitwa katili wasiyo na utu

Nafikiri hii ndiyo sababu ya matajiri kuitwa katili wasiyo na utu

Mimi naona makosa mengi yako upande wako. Huyo dogo yuko sahihi kabisa kwasababu kachagua kuwa mpumbavu ila wewe unamlazimisha aache kufanya kitu anachokipenda. Kwanini unamlazimisha Nyani aamini kuwa asali ni tamu kuliko ndizi? Kimsingi makosa yako ni haya;
1. Unaleta usomi uchwara kwenye biashara. Kiswanglish chako ni ishara ya kwanza. Ingia kwenye biashara bila kuleta mbwembwe za usomi hata kama ni msomi. Acha kazi zikutambulishe.
2. Hiyo sababu namba 1 inafanya utumie gharama kubwa kuendesha biashara yako. Watu wanne wa kazi gani wakati mnaweza kuwa wawili tu mkapiga kazi? Ukitaka wengine si unawapa tu kazi za deiwaka?
3. Bado biashara yako sio kubwa. Bado unajitafuta. Hii ndo sababu umekuja kulia hapa kwasababu ya hivyo vichomi vya gharama zinazokuandama.
4. Technically umekosea sana kumlipa sales man mshahara. Hapo anachostahili ni hiyo 7000 ya nauli na commission. Halafu commission ya 40% kivipi? Ina maana huyo dogo ni shareholder? Hii kama sio chai basi wewe ni mjinga mno na inabidi utafute mtu akufundishe.
5. Unafanya show off za kujifanya ni mtu mwema. Huwa tunasema usijifanye mkristo kuliko Yesu mwenyewe.
6. Ni mwoga wa kufanya maamuzi magumu. Ukiendeleza huo uoga utafilisika. Umekubali hadi dogo akudharau.

NB: Nampongeza huyo dogo kutafuna hela zako hadi akili ikukae sawa.
🤣🤣🤣🤣 du umeamua kutoa ya moyoni kabisaa
 
Habari wanajukwaa,

Heri ya Kwaresma kwa ndugu zangu wakristo.

Ramadham Kareem kwa ndugu zangu waislam.

Kama ilivyo kwa wengi, katika harakati za upambanaji unajikuta una team up na wadau kadhaa katika kujaribu kuona ni namna gani mnaweza mkayafikia malengo kwa ukubwa, haraka na unafuu. BAsi na mimi ni mmoja wapo.

Nafanya biashara ya kuuza huduma. Nilianza alone lakin baada ya muda nikaona ni wakati muafaka kuongeza nguvu kazi tusaidiane majukumu. Nikapata kijana ambaye yeye kazi yake kama alivyoji profile ni Sales person. Nikamchukua nikamuweka ofisini tuanze maisha ya kushirikiana majukumu.

Alikua anafanya kaz kwenye moja ya miradi maarufu tu inayoendelea hapa jijini Dar es salaam, project ya wachina. Baada ya ku discuss terms na conditions tukaanza kazi. Tulikubaliana kuwa ni jukumu langu;
  • Kumuwezesha vitendea kazi
  • Nauli kila siku akiwa sokoni
  • Mshahara kwa mwezi
  • Commission (kubwa sana)
  • Bonus /nyogeza ya mshahara kulingana na anavyo perform majukum na kwakua sales is about numbers so iko waz anaweza kabisa aka predict baada ya muda gani atakua na nyongeza kiasi gani
  • Mawasiliano
Hayo ni haki yake kabisa. Sambamba na hayo tukawekana waz kabisa kuhusu wajibu wake pia ikiwemo
  • Target (ndogo sana ya kupata maximum 2 sales per month - 30 days)
  • Ku submit report (daily and weekly), nk.
Niwe mkwel kijana hakuanza vibaya lakini pia hakua vizuri kama ambavyo nilifikiri au kama vile alivyojipambanua. Nikaona sio tatizo sana, nitam coach. Na tukawa tuna kwenda vizuri kawaida.

Sasa kiasili, mimi sio wale watu ambao ni "Bossy type" japo nina u serious wangu wa kutosha tu. Napenda sana as long as work is involvesld, kuwa karibu na team players wangu. Kwakifupi huwa si entertain gap between me and my guys (ninao wa 4, office admin, tech assistant, sales guy na mmoja ambaye ni oversea sio office based).

Sasa baada ya muda kupita naona kijana amekua haeleweki na performance yake honestly hainiridhishi kabisaaa and inside my heart am deeply dissapointed amd am really thinkimg of what to do.

Kijana wa sales
  • Ja meet target. Yan ni 0%
  • mchelewaji ofisini
  • Hapokei simu hata iweje na anajua simu zangu ni strictly ni za kazi, ukitaka kuwasilana nae ni text tu kama yuko nje ya ofisi
  • Hatoi taarifa kama atachelewa, kwakifupi anaweza ondoka leo jion kaniacha ofisin (maana ninkawaida yangu kufanya kaz mpaka late hours) na akaja kesho akanikuta (ni kawaida yangu saa 12 asubh niko ofisni) , na hapo yeye kaja kachelewa but hakuna maelezo anakupa, ofcz huwa siulizi.
  • Hatumi report za kazi, kuna time nakua na kaz nje ya ofisi au nje ya Dar hata kwa week 1, hivyo hatuonani lakin hutaona report mpaka upige kelele kwamba nataka report.
  • Na unapokua mkali (kitu ambacho sikipend japo nakiweza) , basi dogo sio muoga kabisaa anabishana na wewe kana kwamba wewe ni mtoto au mfanyakazi mwenzie tu, huna la kumwambia.
Sasa nimekaa sana nikawaza namfanyaje huyu kijana, ni mdogo tu around 23 years (maana ndivyo wadogo zetu wa leo hujiona, kwamba ni watoto).

Nimeshafanya juhudi sana za kujaribu kumsaidia nijue anashindwa wapi kufanya kaz akapata wateja, nampa maelezo na maelezo na maelezo lakin wapi.

Nilipoona labda maelezo hayatoshi nikaamua kufanya kwa vitendo ili aone kwamba haya ninayomueleza sio tu naongea toka hewan, yanafanyika ndio maana namsisitiza afanye hivyo.

Nikawa natenga siku 3 kila week naingia sokoni kufanya marketing, mpaka mwez unaisha mimi nikifeli sana naimgiza wateja wawil lakin huwa namba inasoma mpaka 3 au 4 sometimes. Yeye hana anacholeta ofisin zaid ya stori na maelezo.

Nikaona bado labda message yangu hajaipata vizuri, nikabadil utaratibu, badala ya kwenda sokoni /marketing kivyangu na yeye kivyake ,nikaamua kwamba acha tushiriki pamoja. So nika mwambia kila unapokwenda kwa mteja wako kama una meeting, nijulishe twende pamoja.

Lengo hapa nilitaka kujua na kuona, ana engage vipi, nijue pa kumrekebisha, na pia nikataka nimfanya ANIONE MIMI the way na engage na hao hao watu wake ili ajifunze.

Mwisho wa siku nikienda nae marketimg, tunapata sales na tukirud ofisn naendelea kumpa shule na mambo mengine ili ajue namna ya ku improve.

UKUMBUKE HAPO MIMI SIO SALES PERSON BY PROFFESION, am purely a technical person. ni mtaa tu na harakat za ujasriamali zinanibidiisha kujifunza mambo mengi nisije kufa njaa.

Wakuu, nimefanya yooooote hayo lakin wapi!!!! Bila bila Na kitu kinacho ni irritate zaidi ni lack of morals kwake, hiv sasa naona hali inazid kuwa mbaya, kijana hana heshima kabisa.

Ujue mimi kama mtu ambaye nilishafanya ajira pia huwa najaribu kumtazama kijana kama mdogo angu ambaye anatafuta maisha na hili hunifanya kusita kuchukua hatua za haraka kimaamuzi nikiwa namatumain huemda ata change ila wapi!!.

IKabid niende hatua ya mbali zaid kwa kuongea nae kibiashara zaidi. Hii siku nikamuita nje ya ofisi.
  • Nikamueleza ni muda kiasi gani yupo hapa ofisin kwangu
  • Nikamkumbusha ni mshahara kias gani namlipa
  • Nikamuonyesha record za ni gharama kiasi gani ambazo nazi invest kwake katika masuala ya kazi nje ya mshahara.
  • Nikamuonyesha statements za bank ni jinsi gani income yetu as a companya ima flow
  • Nikamuuliza kwa hii comparison mdogo angu umafikiri hii pesa nayolulopa kama salary na marketing transport na ofisin unakula lunch na internet za bure, UNADHAN HIZ COSTS mimi nazi recover vipi kama wewe huna unachoingiza katika mzunguko? HANA MAJIBU.
Nikafikiri baada ya hii discussion ndefu sana labda anaweza pata akil atabadilika, WAAAAPI!

Wakuu huyu dogo sio ndugu yangu, sio jirani yangu, simjui hata ndugu yake mmoja, hapa tuko kikazi tu.

Nisaidieni, kwa haya yooote nimefanya, kuna kipi ambacho sijatimiza wajibu?

UNAWEZA KUJIULIZA KWANINI NIMEFANYA YOOTE HAYA?

Jibu ni simple kabisa, HIKI NDICHO NILIFANYIWA PIA japo mimi sikufika mbali hiv. Ajira yangu baada ya kutoka chuo, nilikua sijui chochote kuhusu kazi. Nakumbuka boss wangu ali dedicate sana muda wake kujifunza kuhsu kaz na majukumu maana hata mimi nilianza kufanya kazi kwenye kampuni ikiwa ndogo sana mpka inakua kubwa kufikia hatua ya kufanya total project sum ya 1B kwa mwaka by that time, toka 150M total project kwa mwaka wakati mimi ndio naingia hapo ofisin, kampuni ikiwa na boss na muhasibu tu.

Boss ndio kila kitu. So nilipoingia mimi cheap labour na degree yangu, boss alinifundisha sana sana sana kaz kwa moyo ili nimpunguzie majukum. That was 2014. Tofauti yangu na huyu dogo ni kwamba, nilikua nazingatia sana mafunzo.

Sasa hii ndio imenifanya kumvumilia kipindi hiki chote lakin kwasasa wakuu nahisi nimefika tamati.

Kwakua yuko kwenye mfungo wa Ramadhani, nime plan nitamuacha mpaka mwez wa Ramadhani uishe kisha nitam expell,

Nitamuondoa kazini, kuangalia namna nyingine.

Nakaribisha ushauri.

Wasalaam.
Hauna unachodaiwa hapo kama binadamu mwenzetu umemaliza kila kitu kama inavyotakiwa angalia future yako na familia sasa.
 
2013 nilishafanya kaz chini boss namba 1 muhindi halaf chini yake bos namba 2 Mkenya sisi ndio wafanyakazi, ule mziki wake huwa siusahau. Ndio hapa nafikiri pakanifanya kuwa na huruma probably. Ujue mimi ni muumini wa "usichokipenda, usimfanyie mwenzio" [emoji23]
Unatakiwa kuwa na "No nonsense" approach ,kamwe usiintertain upuuzi ,fukuza huyo fala
Tafuta mtu mwingine
Wakenya na wahindi hii approach ndio wanatumia , hutakiwi kusumbuka na mpumbavu kama huyo

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
BRaza ahsante kwa ushauri japo umetumia lugha kali sana isivyo lazima.
kwanza kabisa nikiri mpaka kulileta hapa ni dhahiri linaniumiza sana kichwa ndio maana hapa nikaona ni mahala sahihi kabisa.
Mimi naona makosa mengi yako upande wako. Huyo dogo yuko sahihi kabisa kwasababu kachagua kuwa mpumbavu ila wewe unamlazimisha aache kufanya kitu anachokipenda. Kwanini unamlazimisha Nyani aamini kuwa asali ni tamu kuliko ndizi? Kimsingi makosa yako ni haya;
1. Unaleta usomi uchwara kwenye biashara. Kiswanglish chako ni ishara ya kwanza. Ingia kwenye biashara bila kuleta mbwembwe za usomi hata kama ni msomi. Acha kazi zikutambulishe.
sio kwamba nafanya mbwembwe, hapana. Najaribu tu kufuata taratibu za kazi na pia ku apply proffesionalism kwakua hii ni biashara ya tofauti kidogo mkuu wangu, una deal na institutions so watu wako wanafanya kaz kuna namna wanapaswa kuwa na kuna namna wanapaswa kuwa treated.
2. Hiyo sababu namba 1 inafanya utumie gharama kubwa kuendesha biashara yako. Watu wanne wa kazi gani wakati mnaweza kuwa wawili tu mkapiga kazi? Ukitaka wengine si unawapa tu kazi za deiwaka?
Hii uko sahihi, na moja wapo ya njia niliamua ku come up baada ya kuumiza kichwa ni kuwa na sort of dayworker lakin kwangu imekaa tofauti. I started with an oversea person ambaye yeye ana kaz zake lakin anafanya pia kaz na mimi kwa namna tulivyo arrange na njia hii nimeanza kuona matokeo yake
3. Bado biashara yako sio kubwa. Bado unajitafuta. Hii ndo sababu umekuja kulia hapa kwasababu ya hivyo vichomi vya gharama zinazokuandama.
SIkupingi kabisaa mkuu. Ndio maana nikaleta hoja mezani
4. Technically umekosea sana kumlipa sales man mshahara. Hapo anachostahili ni hiyo 7000 ya nauli na commission. Halafu commission ya 40% kivipi? Ina maana huyo dogo ni shareholder? Hii kama sio chai basi wewe ni mjinga mno na inabidi utafute mtu akufundishe.
SIo chai.
40% ni one time sale commision, analipwa mara 1 tu. Mfano amefanya sale kwa mteja ambaye tunaingia mkataba wa kufanya nae kasz kwa gharama ya 100,000/= kwa mwezi, kama ofisi namlipa 40,000/= kama commision. Yeye sio share holder japo katika hii sale ya 100k aliyo fanya nitapa icrememt ya 5% kama nyongeza ya mshahara wake kwa miaka mi 3 as long as mteja huyo haitatokea kuvunja mkataba
5. Unafanya show off za kujifanya ni mtu mwema. Huwa tunasema usijifanye mkristo kuliko Yesu mwenyewe.
sifanyi show off chief. Kama umekwazika nisamehe sana maana sio lengo. Kumbuka pia tumetofautian, ulivyo sivyo mwingine anaweza kuwa. Tusaidiane kupeana mawazo badala ya kutoleana lugha zisizofaa
6. Ni mwoga wa kufanya maamuzi magumu. Ukiendeleza huo uoga utafilisika. Umekubali hadi dogo akudharau.
inaweza kuwa kwel. Moja ya kitu ambacho nakiri nakosa ufanisi ni katika suala zima la managent. Nature yangu ni kwamba napendelea kufanya kaz na watu wenye akilo wanaojua nini wanatafuta ili kupunguza kufuatiliana sana. Huo muda nikiri huwa naona kama bora ni invest katika kufanya mambo ya msingi zaidi kuliko kukufuatilia wewe. Nafikiri kaz yangu ya kwanza ilini athiri, sipendi kufuatiliwa katika kaz na matokeo yake ndio haya sasa huwa na assume mtu hatakiwi kusimamiwa kwenye majukumu yake ambayo mwisho wa siku analipwa kuyafanya. Kwann nikulipe na bado nikufuate nyuma nyuma?
NB: Nampongeza huyo dogo kutafuna hela zako hadi akili ikukae sawa.
Sawa.
 
Nimekusoma mkuu
Fanya hivyo mkuu ,lasivyo unaua biashara hiyo ,
Ndio maana wajasiriamali na biashara za Wa TZ wengi zinarudi nyuma na kudumaa ,na matokeo yake uchumi unaishia kuendeshwa na wageni , weka huruma pembeni kaka
Anakurudisha nyuma huyo dogo ,na uzuri ushamsoma kwamba hawezi badilika
"UKICHEKA NA NYANI UNAVUNA MABUA "
Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
wenzetu sijui hela wanatoa wapi mpk kuwa na makampuni anyway ngj huenda na sisi tutafka huko tupambane
Kufungua kampuni hizi za kijasiriamali kaka haumalizi hata 1,500,000/= pale brella. Na hapo umetumia ma agents watakaolufuatilia kila kitu wewe umekaa tu kungoja certificates zoote mpaka za Mamlala ya mapato.


Hivyo suala sio kuwa na kampuni, suala ni uendeshaji utakaoi sustain kampuni ibaki hai napia ikupe manufaa mkuu.

Hapo ndio ishu ilipo. Na trust me, unaweza na utafika bila shaka.
 
Back
Top Bottom