Nahisi kama nimeingizwa chaka

Sawa mkuu nashukuru kwa maoni yako, ngoja nivumilie nione mwisho wake.
 
Kuna mimba zinafika miezi 11,angewahi kujifungua unge doubt Ila Kama kachelewa Kuna pocbility kubwa mimba Ni yako..
 
Ila wajameni tuwe makini na hawa wanawake hasa ambao sio wake zetu na wamebeba mimba wanayodai kua ni ya kwetu.

Huyu ndgu anajaribu kujiridhisha kwa kupiga hesabu saiv wakati mtu anakaribia kujifungua ilhali mimba aliikubali kabisa.

Ulichokosea kijana ni kuikubali bila kufabya tathmini ya kujiridhisha, ukakurupuka tu halafu saivi unataka ushauri, vipi kama umekosea hesabu na mimba ni yako kweli??
Kipindi kilie kakwambia ana mimba ndo ilibidi upige hesabu kali, siku mliyokutana , siku aliyogundua ana mimba na utaestimate siku ya kujifungua.

Enewei akijifungua kaa nae umuulize vizuri, kwasasa utamletea matatizo maana atawaza sana na kumuathiri chalii.
 
.. na hapo katikati hajakutana na yeyote.

Unamuamini sana huyo manzi ndomana kakupiga na kitu kizito, hiyo mimba imenasa kati ya mwezi 8 na 9 hivyo anatarajia kujifungua mwezi huu au ujao.

Unajua nn? Lea tu mbegu ya kidume mwenzio.
 
Sawa mkuu ahsante kwa hilo, bado sijamwambia kitu chochote, na kwa sasa anaukataa mwezi tuliokutana, anadai tulikutana mwezi wa 8. Na wakati tulikutana mwezi wa 7 kwenye tarehe 25.
 
Unamuamini sana huyo manzi ndomana kakupiga na kitu kizito, hiyo mimba imenasa kati ya mwezi 8 na 9 hivyo anatarajia kujifungua mwezi huu au ujao.

Unajua nn? Lea tu mbegu ya kidume mwenzio.
Nilikutana nae tarehe 25/07 na tarehe 30/08 ndo akaniambia anaujauzito wangu.
 
Kuna ex wangu alikuja getto juzi kati hapa akalala,Ila kwa hali nilomuona nayo (alikua amefubaa sana) sikuuza mechi. Alinilazimisha sana twende kavu nilimgomea. Kesho yake mchana nipo nae getto naona mtu mate yanamjaa sana mdomoni mixer kwenda kutema na toka amekuja alikua anakula chakula kingi kunishinda mm. Nikaunganisha dots nikagundua Ana mimba changa,nikambananisha na kumuuliza kwann anataka kunibambikia mimba sio yangu? (Kumbuka kipindi chote namchakata sijauza mechi). Alikosa majibu na kuishia kujikanyaga kanyaga huku akinikatalia hana mimba.

Jioni nilimpa nauli na kumshauri akakae chini na baba kijacho wajue hiyo mimba wanaileaje.

Mkuu kwenye swala la ujauzito ukicheza tu faulo, umelea mbegu ya kidume mwenzio.

NB: Faulo nazozungumzia Ni pamoja na kutokujua mzunguko wa hedhi wa mpenzi wako pamoja na kuuza mechi ovyo ovyo. Kila lenye kheri[emoji1423]
 
na kwa sasa anaukataa mwezi tuliokutana, anadai tulikutana mwezi wa 8. Na wakati tulikutana mwezi wa 7 kwenye tarehe 25.

Kwa hayo maneno yako niloquote ni dhahiri kua UMELIWA KICHWA mkuu. Pole Sanaa...
 
1. Mimba haihesabiwi miezi unahesabu week piga hesabu za week.
2. Angalia kadi ya clinic imeandikwa week ngapi na makadirio ya kujifungua ni lini...
3. Mimba huwa zinapitiliza muda kama mtoto hayupo tayari kutoka.
 
Mkuu hapa nashindwa nimwambie kitu gani maana nahisi nitamchanganya kabsa. Acha nitulie ajifungue tutajua kitakachofata atarudisha gharama zangu mshezi huyu.
 
Sawa mkuu ahsante kwa hilo, bado sijamwambia kitu chochote, na kwa sasa anaukataa mwezi tuliokutana, anadai tulikutana mwezi wa 8. Na wakati tulikutana mwezi wa 7 kwenye tarehe 25.
Ndio maana nakwambia kosa ulilifanya kipindi kile mkuu, si wewe tu wanaume wengi hufanya hilo kosa na mwisho kulea kwa kupenda au kutopenda mtoto asie wake, anahisi sio wake lakini ndo hana ushahidi.

Hamna namna subiri ajifungue tu mlee huyo mtoto, la sivyo akikupeleka ustawi wa jamii we hoja zako zinaonekana kabisa ni dhaifu.
Ponapona yako mtoto azaliwe mwarabu wakati we mndengereko au mweupe pee wakat nyie wote ni blacks ila kama kanaendana na ww UMEISHA ni yako hiyo.
 
1. Mimba haihesabiwi miezi unahesabu week piga hesabu za week.
2. Angalia kadi ya clinic imeandikwa week ngapi na makadirio ya kujifungua ni lini...
3. Mimba huwa zinapitiliza muda kama mtoto hayupo tayari kutoka.
Sawa mkuu ngoja nimwambie nione ni wiki ngapi..
 
Nilikutana nae tarehe 25/07 na tarehe 30/08 ndo akaniambia anaujauzito wangu.
Unasema hakukutana na mwingine toka ulivyomchakata, ulikua unaishi nae? Ulikua unaongozana nae kwenye mitoko yake binafsi? Ulikua nae 24/7? HUSIWAAMINI SANA WANAWAKE.

Ila kwakua alikwambia tarehe 30/08 inawezekana ikawa ni wako ila KUMBUKA wakati anakueleza mimba ilikua na mwezi mmoja tayari na ishapita miezi 10 sasa. Fanya kuonana na daktari wa wajawazito muulize inawezekana mimba kwenda zaidi ya miezi 10 na nn usababisha inatokea case kama hiyo?

Pia janja akizaliwa kuna namna yakufanya kujua kama Ni wako kiasili na kisayansi.
 
Nina ushahidi wa sms wa siku tuliyokutana. Akinipelekea ustawi nitajitetea kwa ushahidi wangu wa sms.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…