Nahitaji mawazo yenu, nina mpango wa kununua nazi kutoka Lindi au Mtwara kwa bei ya jumla na kuuza Dar

Nahitaji mawazo yenu, nina mpango wa kununua nazi kutoka Lindi au Mtwara kwa bei ya jumla na kuuza Dar

Biashara ya kushauriwa wakati fulani siyo nzuri sana. Unatakiwa ukafanye utafiti mwenyewe ili uwe na uhakika wa kitu unachoenda kukifanya.

Ungetembelea hayo masoko ya Dar ili kujua bei ya kuuzia pamoja na usafiri, halafu ungeenda huko Lindi ili kuangalia upatikanaji wa hizo nazi. Baada ya hapo unafanya sasa tathmini kuona kama hiyo biashara itakulipa, au la.
 
Ni biashara nzuri, hakikisha zimekomaa na kukauka vizuri, hakikisha hazinyeshewi na mvua kipindi unasafirisha, hakikisha umeongea na wanunuzi wa jumla / madalali kabla ya kuleta mzigo.

All the best
 
Habarini Wana JF,

Nimepata wazo la kununua nazi Jumla na KUUZA DAR. Mwenye uzoefu au kujua bei za usafiri na masoko yapoje kwa Dar naomba mawazo YENU.

Mtaji laki tano
Nenda Kijiji kinaitwa Ng'apa pale Lindi, Kila la kheri, japo mtaji wako mdogo
 
Kumbe nazi zinapatikana kusini kwa wavivu? Inamaana kaskazini na kanda ya ziwa kuliko na wachapakazi wengi hawalimi nazi?
 
Back
Top Bottom