Nahitaji rafiki wa kike ambaye atakuwa mke wangu ziku za baadaye

Nahitaji rafiki wa kike ambaye atakuwa mke wangu ziku za baadaye

APPELLANT

Member
Joined
Oct 10, 2020
Posts
73
Reaction score
90
Habari za jioni ndugu zangu wana MMU.

Bila kupoteza muda ni kwamba nina miaka 30, mkiristo, nina elimu ya chuo, nimejiajiri mwenyewe, nina urefu wa wastani.

Hivyo basi, kutokana na hizo sifa hapo zilizotajwa hapo juu napenda kuwataarifu kwamba nahitaji rafiki wa kike ambaye siku za mbeleni atakuwa mke wangu kama tutakuwa na maridhiano.

Nitafurahi sana kama nitampata rafike mwenye sifa zifuatazo:- awe na umri wa miaka 24-29, awe mwanasheria/daktari/mwalimu/mhasibu, awe ni mcha mungu, asiwe mweupe sana wala mweusi sana, pia awe mrefu wa wastani.

Kadhalika, sipendi rafiki mwenye mtizamo hasi na usio sahihi (uongo, lawama, chuki, kununa bila sababu, unafiki,gubu na umbea) bali napenda rafiki ambaye atakuwa na mawazo chanya, mazuri na yenye kujenga na mwenye ustaarabu mwingi na staha.

Aidha, napenda rafiki ambaye ni muwazi sana nikimaanisha kwamba ambaye yupo tayari kueleza makosa yangu au kuniambia ukweli mtupu bila kupepesa macho pale ambapo nitakosea.

Mwisho, nina dhamira nzuri na nimedhamiria katika jambo hili kwa lugha nyepesi nipo tayari kujenga huo urafiki ambao utakuwa imara kuelekea katika maisha ya ndoa.

Karibuni sana PM.

Ahsanteni.
 
Una elimu ya chuo na umejiajiri, unamtaka mwanamke ambaye ni Daktari, Mwanasheria, Mwalimu au Muhasibu,

Umeshindwa nini kusema upo level gani ya chuo na umejiajiri kwenye sekta ipi,

Pia weka picha zako mbili,
Moja Passport size na ingine iwe full picture.
 
Una elimu ya chuo na umejiajiri, unamtaka mwanamke ambaye ni Daktari, Mwanasheria, Mwalimu au Muhasibu,

Umeshindwa nini kusema upo level gani ya chuo na umejiajiri kwenye sekta ipi,

Pia weka picha zako mbili,
Moja Passport size na ingine iwe full picture.
Thank you for your comment.

I hold a bachelor's degree in law (Bachelor of Laws, LL.B), also a Private Practitioner Attorney in Tanzania.

I don't think if JF rules permit members to append pictures in here, however, regarding passport sized & full picture, I would like to respond that if you're KE and wished to be the one, I'm ready to do what you have recommended.
 
Thank you for your comment.

I hold a bachelor's degree in law (Bachelor of Laws, LL.B), also a Private Practitioner Attorney in Tanzania.

I don't think if JF rules permit members to append pictures in here, however, regarding passport sized & full picture, I would like to respond that if you're KE and wished to be the one, I'm ready to do what you have recommended.
Kwanini umejibu kwa kiingereza wakati tangazo lako umelileta kwa kiswahili?
 
Kwanini umejibu kwa kiingereza wakati tangazo lako umelileta kwa kiswahili?
Aisee. Samahani mkuu ingawa nina imani kubwa sana kwamba watumiaji wengi wa JF ni wasomi na wanaimudu hii lugha vizuri hata kama siyo sana ila wanaielewa kwa kiasi fulani.
 
Aisee. Samahani mkuu ingawa nina imani kubwa sana kwamba watumiaji wengi wa JF ni wasomi na wanaimudu hii lugha vizuri hata kama siyo sana ila wanaielewa kwa kiasi fulani.
Basi ungeleta mada kwa lugha ya kiingereza tangu mwanzo,

Turudi kwenye picha, uongozi wa Jamii forum haumkatazi mtu kuweka picha yake halisi,

Ila wanasisitiza ukiweka tangazo uweke na picha.
 
Duuh nimekosa bahati...Miaka yangu 18[emoji125][emoji125][emoji125]
 
Kwanini umejibu kwa kiingereza wakati tangazo lako umelileta kwa kiswahili?
Aisee. Samahani mkuu ingawa nina imani kubwa sana kwamba watumiaji wengi wa JF ni wasomi na wanaimudu hii lugha vizuri hata kama siyo sana ila wanaielewa kwa kiasi fulani.
Basi ungeleta mada kwa lugha ya kiingereza tangu mwanzo,
Sawa ingawa matumizi ya lugha ya Kiingereza haijaathiri haki yako yoyote mkuu.
Turudi kwenye picha, uongozi wa Jamii forum haumkatazi mtu kuweka picha yake halisi,
Sawa nimekuelewa mkuu.
Ila wanasisitiza ukiweka tangazo uweke na picha.
Kuweka picha hapa sipo tayari kwa sababu ya kulinda twasira yangu katika jamii ingawa atakayekuja PM tutabadilishana mawasiliano na kama atahitaji picha nitamtumia bila kipingamizi chochote.
 
Aisee. Samahani mkuu ingawa nina imani kubwa sana kwamba watumiaji wengi wa JF ni wasomi na wanaimudu hii lugha vizuri hata kama siyo sana ila wanaielewa kwa kiasi fulani.

Sawa ingawa matumizi ya lugha ya Kiingereza haijaathiri haki yako yoyote mkuu.

Sawa nimekuelewa mkuu.

Kuweka picha hapa sipo tayari kwa sababu ya kulinda twasira yangu katika jamii ingawa atakayekuja PM tutabadilishana mawasiliano na kama atahitaji picha nitamtumia bila kipingamizi chochote.
Namna hiyo... Watamseyin man 😀

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom