Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua aondolewa madarakani

Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua aondolewa madarakani

Valencia_UPV

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2016
Posts
6,974
Reaction score
8,750
Pole Rigathi Gachagua, Former Deputy President.

=====

Hii ni baada ya seneti kupiga kura kupitisha mashtaka 5 kati ya 11 misingi yake ya kuondolewa kwake madarakani.

Spika Amason Kingi: Seneti imeamua kumng'oa madarakani kwa hati ya mashtaka, Naibu Rais Rigathi Gachagua. Hivyo basi, anakoma kushika wadhifa huo rasmi.

Kati ya mashtaka 11, kupatikana na hatia kwenye shtaka lolote kunapelekea kuondolewa madarakani.





Pia soma:
 
Technical mistake ,watamuongezea huruma ambayo hata kama haitamsaidia yeye ....ila itaumiza Serikali ya Ruto ....Ruto ni Rais wa msimu mmoja tu!
ni ngumu kufikia hitimisho kwa hili tu, maana hatuwezi jua huwenda DP ajae akatokea Mlimani na akawa better zaidi ya Riggy G
 
Bunge la Seneti nchini Kenya limeamua kumuondoa Naibu Rais wa nchi hiyo Rigathi Gachagua madarakani kufuatia zoezi la siku mbili lililojumuisha ushahidi mwingi na saa kadhaa za kumuuliza maswali.

Gachagua, ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Karen, ameondolewa madarakani baada ya maseneta 53 kupiga kura kuunga mkono shtaka la kwanza la ukiukaji mkubwa wa vifungu 10, 27, 73, 75, 129 vya Katiba ya Kenya.

Ni Maseneta 13 pekee waliopiga kura kupinga shtaka hilo kama ilivyobainishwa katika hoja ya kumuondoa madarakani iliyowasilishwa na mbunge wa Kibwezi, Mwengi Mutuse.
 
#BREAKING: The Senate has voted to impeach Deputy President Rigathi Gachagua, making him the first Deputy President in Kenya's history to be removed from office through impeachment.
In a significant development, at least 53 senators supported the charge of gross violation of key constitutional articles, including Articles 10, 27, 73, 75, and 129.
Na huku kwetu wangeleta kama hii unadhani tungeanza na nani?
 
Hata hivyo amepambana sana, lakini bila shaka rafiki yake Ruto ndio ameamla kumtosa ili kulinda kiti cha uRais.
Na kunyume chake sinto shangaa ikawa ndio political milage ya Righathi Gachagua kwa mwaka wa uchaguzi akagombea kiti ya Presidency
 
Back
Top Bottom