Naibu Waziri Deus Sangu: Tutaanza kufanya vipimo vya afya ya akili kwa vijana kabla hawajaajiriwa Serikalini

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Inakuaje vijana mmekuwa na utovu wa nidhamu kiasi hiki mpaka mnatakiwa mpimwe afya akili kabla hamjawa watumishi wa umma huko Serikalini?

Akizungumza leo Jijini Dodoma na Naibu Waziri , Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deus Sangu wakati wa akifunga kikao kazi cha siku tatu cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu katika Utumishi wa Umma amesema kuwa iko mbioni kuanzisha mchakato mpya.

Katika vigezo vipya ambavyo mtu hatahitaji kabla ya kuajiriwa Serikalini ni pamoja na kufanyiwa vipimo vya afya ya akili kabla hajaingia kuwa mtumishi wa umma.

"Sekretariati ya ajira imekuja na hiyo program ya Psychometric test ili tuweze kutambua huyu tunaempeleka kwenye utumishi wa umma ana shida mahali fulani ili tuweze kufanyia marekebisho ili akiingia aweze kutusaidia"

Your browser is not able to display this video.
 
Waanze kuwapima Mikojo na Damu watalii wanaokuja na Visonono na kaswende sugu. Dada zetu wanaenda kuharibiwa.


Nimecheka lakini.

Deus Sangu atuonyeshe results za hiyo psychometricπŸ™ŒπŸΎ zake Mwenyewe kwanza.πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Mkumbuke kupima afya ya akili kwa vijana wanao ajiriwa kwenye majeshi yetu hasa jeshi la polisi.
 
Kazi ipo yaani watoto mnawatengenezea mazingira magumu kweli kwenye ajira Watanzania sijui mna matatizo gani ninyi mmepata kazi kirahisi tu na elimu bila mkopo ila wenzenu sasa vigezo kama vile hawana Elimu..
 
Ili tuwe more practical, tutaanza na waziri mwenyewe πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ 😎😎😎😎😎😎😎
 
Nafikiri wangeanza kupima hao mawaziri, yeye mwenyewe anaweza kuwa na shida kubwa mahali fulani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…