Naibu Waziri Masanja aongoza kikao cha taasisi za wizara ya maliasili na utalii

Naibu Waziri Masanja aongoza kikao cha taasisi za wizara ya maliasili na utalii

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

NAIBU WAZIRI MASANJA AONGOZA KIKAO CHA TAASISI ZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja ameongoza kikao cha kimkakati cha kufanya mapitio ya taarifa mbalimbali za utendaji kazi za Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na hatimaye kukuza utalii na kuimarisha usimamizi wa Uhifadhi wa Maliasili nchini.

Kikao hicho kimefanyika leo Machi 6, 2023 katika Ukumbi wa Ofisi za Ngorongoro zilizopo Jijini Arusha.

Mhe.Masanja ametumia fursa hiyo kuwataka watendaji wa Taasisi kuwa wabunifu kwa kutumia historia ya taifa na elimu ya viumbe hai kuwa fursa ya kujifunza na kuiongezea Serikali Mapato na kuongeza ajira na kipato kwa Mwananchi mmoja mmoja.

Aidha, kikao hicho kilijadili namna ya kutumia Makumbusho za Taifa kama eneo mojawapo la kuiongezea Serikali mapato kwa kuwa wana wigo mpana zaidi kuliko Taasisi nyingine katika kuibua fursa zilizopo nchini.

Katika hatua nyingine, Mhe.Masanja amekielekeza Chuo cha FITI kuandaa mpango utakaokiwezesha Chuo hicho kuwepo na miradi mbalimbali itakayokiwezesha kuongeza mapato kwa njia ya Mafunzo.

Taasisi zilizoshiriki kikao hicho ni Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI), Makumbusho ya Taifa ( NMT) pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-03-06 at 16.54.03.jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-06 at 16.54.03.jpeg
    55 KB · Views: 6
  • WhatsApp Image 2023-03-06 at 16.54.05.jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-06 at 16.54.05.jpeg
    85.6 KB · Views: 8

NAIBU WAZIRI MASANJA AONGOZA KIKAO CHA TAASISI ZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja ameongoza kikao cha kimkakati cha kufanya mapitio ya taarifa mbalimbali za utendaji kazi za Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kuboresha utendaji kazi na hatimaye kukuza utalii na kuimarisha usimamizi wa Uhifadhi wa Maliasili nchini.

Kikao hicho kimefanyika leo Machi 6, 2023 katika Ukumbi wa Ofisi za Ngorongoro zilizopo Jijini Arusha.

Mhe.Masanja ametumia fursa hiyo kuwataka watendaji wa Taasisi kuwa wabunifu kwa kutumia historia ya taifa na elimu ya viumbe hai kuwa fursa ya kujifunza na kuiongezea Serikali Mapato na kuongeza ajira na kipato kwa Mwananchi mmoja mmoja.

Aidha, kikao hicho kilijadili namna ya kutumia Makumbusho za Taifa kama eneo mojawapo la kuiongezea Serikali mapato kwa kuwa wana wigo mpana zaidi kuliko Taasisi nyingine katika kuibua fursa zilizopo nchini.

Katika hatua nyingine, Mhe.Masanja amekielekeza Chuo cha FITI kuandaa mpango utakaokiwezesha Chuo hicho kuwepo na miradi mbalimbali itakayokiwezesha kuongeza mapato kwa njia ya Mafunzo.

Taasisi zilizoshiriki kikao hicho ni Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI), Makumbusho ya Taifa ( NMT) pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.
Naibu Waziri huwa ana shundu
 
Back
Top Bottom