Naishi na Mwanaume, tatizo nikimgusia suala la ndoa anadai nisubiri hayuko tayari kwa sasa

Naishi na Mwanaume, tatizo nikimgusia suala la ndoa anadai nisubiri hayuko tayari kwa sasa

Pole sana moyo wa mtu ni kichaka hujui ana waza nini moyoni mwake, Mungu akusaidie uweze kutimiza haja yako ya kufunga ndoa.

Kweli i wish nijue anawaza nini juu ya mahusiano yetu maana niko kwenye mahusiano ambayo sijui malengo yake ni nini

Japo anaplay party kubwa sana kwenye maisha yangu kiujumla ananifanyia mambo mengi na makubwa ambayo sikuwahi kufanyiwa before

Nimemwambia tufanye hata simple tu ndugu kiasi basi tuweke dinner tu ilimradi tupunguze dhambi ya uzinzi
 
Let me be very honest with you,kwanza hujafunga mkuu,mmekuwa mkishinda njaa.Zinaa ni haramu mkuu,uliyezini mchana mwezi wa ramadhan au usiku wa ramadhan,ukizini mchana wa ramadhan adhabu yake ufunge miezi miwili mfululizo au kuwalisha maskini 60.Na ukizini usiku wa ramadhan kabla ya kuanza wakti wa kuanza kufunga,inaweza swaumu yako isiswihi na mwenyezi Mungu ndiye anayewatakabalia watu na amesema anawatakabalia tu wacha Mungu,je Mzinifu ni mcha Mungu?Hakika Mzinifu sio Mcha Mungu.
 
Habari zenu wanajf

Waislam wenzangu A’alaykum (eid inanukia[emoji39])


Niko na mtu tuna miaka mitatu hadi sasa tumepitia changamoto nyingi furaha na huzuni, kiukweli ni mtu ambaye hajawahi kuniacha hata hatua moja

Swala lililonileta kwenu

Huyu mtu ni muislam mwenzangu hamna changamoto zingine zozote isipokua kwenye swala la sisi kuhalalisha anakua mgumu mno (ndoa) ukimwambia tu basi tuhalalishe ni yuko muwazi yeye kwasasa hataki

Huduma zote anatoa kuanzia matumizi (pesa) na huduma za chumbani[emoji3059][emoji3059] hajaoa, tunaishi wote

Shida ni hiyo tu hataki tuhalalishe ndugu zangu nifanyaje na kuachana nae siwezi japokua mwenyewe alinambia kama naona ananichelewesha basi anipe space ndani ya muda flani ikiwa bado sijaipata hiyo ndoa turudiane

Hata funga yangu naona haiswihi kabisa maana tunaishi wote then tunafunga eti

Kwenye kila kitu mnakubaliana ila swala la ndoa hapo hataki anasema nivumilie

Simuelewi!!! Au ana miiko[emoji848] Niko hoves nimechoka kuzini
Moja ya msingi mkuu wa dini ya kiislamu ni subira,vuta subira
 
Zinaa inahalalishwa kwa kufunga ndoa?

Acheni kumchezea Muumba wenu ninyi. Mnakaa kwenye zinaa na kuishi maisha ya zinaa, hamjui kuwa mmeambiwa "ikimbieni zinaa"?

Kwanini usiache zinaa kwanza kisha ndio uitafute hiyo ndoa. Kama unajitambua na una hofu ya MUNGU, basi ondoka kwa huyo Mwanaume, jitenge na zinaa. Kama ana nia na wewe atakuja kuleta mahari kwenu na atakuoa.
Lakini kama hauna hofu ya MUNGU, basi wewe endelea na zinaa yako. Utavuna unachokipanda sasa hivi.
 
Let me be very honest with you,kwanza hujafunga mkuu,mmekuwa mkishinda njaa.Zinaa ni haramu mkuu,uliyezini mchana mwezi wa ramadhan au usiku wa ramadhan,ukizini mchana wa ramadhan adhabu yake ufunge miezi miwili mfululizo au kuwalisha maskini 60.Na ukizini usiku wa ramadhan kabla ya kuanza wakti wa kuanza kufunga,inaweza swaumu yako isiswihi na mwenyezi Mungu ndiye anayewatakabalia watu na amesema anawatakabalia tu wacha Mungu,je Mzinifu ni mcha Mungu?Hakika Mzinifu sio Mcha Mungu.

Ni kweli m mwenyewe nafsi yangu inanisuta
 
Zinaa inahalalishwa kwa kufunga ndoa?

Acheni kumchezea Muumba wenu ninyi. Mnakaa kwenye zinaa na kuishi maisha ya zinaa, hamjui kuwa mmeambiwa "ikimbieni zinaa"?

Kwanini usiache zinaa kwanza kisha ndio uitafute hiyo ndoa. Kama unajitambua na una hofu ya MUNGU, basi ondoka kwa huyo Mwanaume, jitenge na zinaa. Kama ana nia na wewe atakuja kuleta mahari kwenu na atakuoa.
Lakini kama hauna hofu ya MUNGU, basi wewe endelea na zinaa yako. Utavuna unachokipanda sasa hivi.

[emoji122][emoji122]
 
Mwanaume alazimishiwi kuoa.

Kuna vitu vitatu vinachangia mwanaume aoe na vyote ni MUHIMU sana
1. Hali ya maisha yake
Sasa hapa kipimo anacho mwenyewe kichwani.Yeye ndo anajua kwamba kwa uwezo huu wa kifedha naweza kumudu familia na sio wewe jinsi unavyompimia.

2. Mwanamke sahihi
Unaweza kuwa na mwanaume ht miaka 5 na usiwe sahihi niamini mimi kwa hili. Wanaume hatupimi ubora wa penzi kwa miaka tuliyodumu na mwanamke bali kwa ubora wa penzi hasa kwenye ishu ya ku maintain heshima yako kwake na usaliti.Unaweza kudumu nae ht miaka 8 ila km ulishawahi msaliti au mdharau jua ndoa inaweza isiwepo pamoja na miaka yenu 50 ya mahusiano
3. Umri na Utayari wa kuoa
Km hatupo tyr uwaga hatupo tayari tu.Haijalishi nina mwanamke sahihi na nina uwezo wa kumuhudumia.SIPO tayari kuvamia stress za ndoa.

Swali langu ni moja tu na ujijibu mwenyewe.Mpaka mkafikia kukaa pamoja nani hasa alitaka???Usigekuwa ni mzigo hapo hlf hujijui.Wanaume tuna huruma ni kazi kumfukuza mwanamke aliyehamia ht km hatujapenda kbs.

Mwisho kuanzia leo usizungumzie kuhusu kuolewa yaani leo ndo iwe mwisho. Pili Km huwezi kuacha kuzungumza kuhusu ndoa basi fanya jaribio kuu la kujua km wewe ni wa kuolewa nae au si😵ndoka hapo nyumbani rudi kwenu na sababu iwe ungependa uishi na mwanaume aliyekuoa kwahiyo km hayupo tayari basi unarudi kwenu mpk atakapokuwa tyr ila jiandae kujua ukweli halisi why hataki kuoa na ukweli uwaga mchungu.
 
Ni kweli m mwenyewe nafsi yangu inanisuta
Why are you wasting yourself with someone who doesn't appreciate you?Umejirahisisha Kuishi naye,thamani yako haioni,anakuona wa kawaida sasa.Kama kitu kinapatikana rahisi thamani yake inashuka.Unajua hata Roho ingekuwa inauzwa dola milioni moja thamani yake tayari inakuwa chini?kivipi?kwa sababu kuna watu wangekuwa wanazinunua na kuwa miungu watu.Ushauri wangu hautakuwa mzuri kwako au unaoupenda wewe.Ikimbieni zinaa maana niuchafu,Ushauri wangu achana naye kabisa,usichukue space yoyote,tell him its over,najua umepoteza muda,lakini hakuna guarantee kwamba hautapoteza muda zaidi kwake.Kama Mungu amepanga uolewe utaolewa na kama hajapanga zidi kumuomba utapata ndoa.
 
Back
Top Bottom