Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

Chitemo ndio nani?
We jamaa kweli ulikua hupendi kiswahili
10153879_871067866240966_1728007651_n.jpeg
 
Umenikumbusha hiyo ya kuangalia picha kwenye box la condom mie na wenzangu enzi tuko wadogo tumezifanya sana..
Ilikuwaga "salama condom", inaonesha hatua za uvaaji condom, kunjunjana na namna ya kuivua na kui-dump baada ya tendo.
Kwenye kunjunjana jamaa na bibie wamejifunika na ka-shuka nusu mgongo.. [emoji3][emoji16]
Nyingine ilikuwaga condom tunaijaza maji au tunaifanya puto/ pulizo. Afu yalikuwaga magumu kupasuka tofauti na zile puto nyingine za kawaida..
Basi ilikuwa tunazirusha hewani then tunafurahi. Msala wake mkutwe sasa.. Apo ndo ilikuwa ishu...
Nway hongera kwa ku-hustle..
We are waiting for muendelezo
 
Sehemu ya 4:

.... Ikabidi nianze kufanya kazi kwa malengo ya kusaka nauli na hela ya kuanzia. Nikafanya sana vibarua tofauti tofauti, kwa maeneo tofauti tofauti. Kipindi hicho chote hakuna mtu yoyote ninayemuamini pale Dar, kila mtu namuona mwizi. Sasa kuna kipindi fulani nilikuwa nafanya kibarua cha ujenzi maeneo fulani kule kibaha. Wakati natoka mishe narudi ghetto (nilikuwa nalala kwa fundi mmoja ambae alikuwa bachela),njiani nikakuta lundo la watu wametengeneza umbo la duara. Nikasogea nione nn kinaendelea. Nakuta jamaa wanachezesha nyoka, mara waseme nyoka anawika, mara anapiga mluzi. Kila nikisubiria awike hawiki, mluzi hapigi. Nikasema ngoja nisepe. Yule mchezeshaji nae ghafla akasema "Hiki ninachoenda kukifanya hapa, mchawi hawezi kukaa lazima aondoke" moyo ukalia pa! Nikaona hapa nikiondoka nitaonekana mchawi, ikabidi niendelee kubaki. Huyo nyoka bora angewika basi, hawiki. Mpaka kigiza kinataka kuingia. Wale jamaa wahuni sana, ukiwa na wasi wasi wanakujua. Wakati naondoka ghafla mmoja akaja, akachota mchanga ile sehemu niliyotoa mguu, alafu akataka kuuweka kwenye kikapu huku akisema "Nimmalize?" Kuna washenzi wengine wakajifanya kuniombea msamaha, kumbe lao moja.

Kiongozi wao akaendelea kusema. Kijana umekanyaga sehemu mbaya sana, nisipokusaidia unapotea mazima. NIKAPANIKI. Jamaa akatoa amri, hebu mpelekeni kilingeni mumsaidie. Wakanizungusha sehemu waliyopaki gari lao eti wanaenda kunifanyia dawa. Kufika kule wakanitaitisha, wakanisachi hadi kwenye viatu. Sema waliambulia posho ya siku hiyo tu, maana hela zangu nilikuwa nazificha kwenye ukuta wa chooni kule ghetto kwa jamaa.

Walivyoniachia nikarudi mdogo mdogo hadi kwa jamaa, sema sikumwambia chochote kuhusiana na yaliyonikuta. Siku zikaenda, ujenzi ukaisha. Nikaondoka kibaha. Hapo malengo yangu ilikuwa nifike Songea, maana yule jamaa aliyenipa habari za dhahabu na migodi kwa ujumla alisema kipindi ambacho anakuwa nje ya migodi huwa anapatikana mkoa ule, hivyo aliniachiaga namba ya simu nikifika nimtafute. Kwa vibarua nilivyoshakuwa nimefanya, hela niliyokuwa nayo ingeweza kunifikisha moja kwa moja hadi Songea, ila sikupenda kufanya hivyo. Badala ya kupanda mabasi yaendayo kule, me nikapanda bus lililonifikisha sehemu moja wanaita Mafinga. Lengo la kwenda Mafinga, ni kwasababu wakati nasoma, kuna wadau wazawa wa kule walikuwa wananipa story za biashara za mbao na jinsi zilivyokuwa na hela.

Nilifika Mafinga jioni sana, inaelekea usiku. Kitu kimoja ninachokipenda kwa upande wa mikoani, jamaa ni wasikivu, pia wakiona mtu ni mgeni basi wanamsaidia tofauti na Dar. Sikutaka niingie kichwa kichwa kwenye biashara nisiyoijua, alaf pia baada ya kupata maelezo ya hapa na pale nikagundua mtaji unaohitajika uwe wa kutosha. Nikaachana na biashara ya uuzaji mbao, ila nikaanza vibarua vya upangaji wa mbao pamoja na kuzitreat. Hapa ndio niliamini ule msema wa akili mjini, nguvu peleka bushi. Hii kazi ni ngumu. Maana ndani ya wiki moja nilikuwa nimechubuka mabega yote mawili, yani pametoka sugu. Mwanzoni kazi ilikuwa poa, ikiisha tunapewa chetu, ukilala hoi.

Kuna siku nilichoka kupita maelezo, kiasi kwamba nilivyojiegesha ile jioni baada ya kupewa posho, nikasinzia mazima pale nilipokuwa. Kilichonishtua ni baridi lilizidi kuwa kali pamoja na sauti za watu. Nikajinyanyua kusogea walipo watu, nikaona jamaa wanapakia mbao kwenye toyo. Akili yangu inawaza hela tu, nikawafata nikijua ni jamaa zangu walau nipate kibarua. Walivyoniona wakashtuka. Kuwahoji naona wanababaika. Nikajua hawa ni wezi tu. Hapo ndio niliona umuhimu wa simu, ningekuwa nayo ningempigia Boss kumpa taarifa.

Wale jamaa wote wakakimbia, akabaki mwenye usafiri tu. Uzuri akatokea masai wa godown la jirani. Akampigia boss. Boss akawaka, sina mteja wa usiku, washikeni wasitoke hao. Alikuja mpaka pale usiku ule ule, mwenye toyo akalazwa polisi, kesho yake akasaidia wakapatikana wale wengine. Tokea siku hiyo boss akanifanya kuwa foreman wake, cheo kikapanda. Niliendelea kukomaa pale hadi ilipofika msimu wa mvua, pale shughuli nyingi za miti huko porini zikasimama, na sisi huku mbao zikapungua. Hela ikapungua pia. Sikuona haja ya kuendelea kuwa foreman sehemu isiyo na hela. Rasmi nikaenda Songea.

***** ***** ***** ***** ***

Sikutaka kupoteza muda sana, hela ambayo nilikuwa nayo ilikuwa ni mwanzo mzuri. Kwavile nilikuwa tayari nina simu, nikampigia yule jamaa, hakawa hapatikani. Usiku hapatikani, asubuhi na mchana hivyo hivyo . NIKAWA MPOLE.

.....
 
Pia natamani niweke baadhi ya vielelezo maana bado ninavyo, mfano barua ya kusimamishwa shule wakati nipo primary, au ile ya kufukuzwa shule seminary, joining instructions n.k . Ila nataka kuendelea kuhide my ID , ndio maana nashindwa. Pengine huko mbele ntaangalia baadhi na kuviweka hapa.
 
Umenikumbusha hiyo ya kuangalia picha kwenye box la condom mie na wenzangu enzi tuko wadogo tumezifanya sana..
Ilikuwaga "salama condom", inaonesha hatua za uvaaji condom, kunjunjana na namna ya kuivua na kui-dump baada ya tendo.
Kwenye kunjunjana jamaa na bibie wamejifunika na ka-shuka nusu mgongo.. [emoji3][emoji16]
Nyingine ilikuwaga condom tunaijaza maji au tunaifanya puto/ pulizo. Afu yalikuwaga magumu kupasuka tofauti na zile puto nyingine za kawaida..
Basi ilikuwa tunazirusha hewani then tunafurahi. Msala wake mkutwe sasa.. Apo ndo ilikuwa ishu...
Nway hongera kwa ku-hustle..
We are waiting for muendelezo
Thanks man. We still do.
 
Back
Top Bottom