Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi ulinikataa ww kwann uangaike dawa wakati unapendwa jinsi ulivyoMamboz,jamani kama mnakumbuka nilikua natafuta mchumba na hali yangu niliyonayo,wengi walijitokeza wakidhani natania labda,walihisi mimi ni mzuri sana ila natania.
Kusema ukweli nipo kama nilivyosema,na nimerudi tena kuomba msaada kwa anaejua dawa ya makovu tafadhali,sio ya ajali yani yanatokea tu hata nikijikuna kovu linabaki,pia nikiumwa na mdudu lazima kovu libaki,nikijikwaruza kidogo bas kovu hilo.
Wanaume pia hawaniangalii hata mara mbili,niko mpweke,sina hata mwenza.
Nachukia sana ngozi yangu na sijui shida ni nini,naomba tafadhali kwa anaejua dawa ambayo itanifaa...
Wanawake wenzangu nisaidieni,kina baba,kina kaka naombeni mnitajie dawa itakayoondoa makovu haya jamani.
Bio oil nimejaribu haifanyi kazi,aloevera hua napaka sioni matokei,limao pia hakuna kitu.
Najisikia vibaya sana,mda mwingine hua nikijiangalia nalia tu,why me?
Msaada wenu ndugu zangu tafadhali.
Mlipeni Shigongo pesa yake mnaendelea kuvaa T-shirt mkijidai kumbe deni mnadaiwa
Barikiwa mtumishi kwa ushauri huu! Injili ya Kristu na isonge mbele!Njia nyingine ya uhakika kwa wenye uhakika.
Amua kuokoka kweli kutoka moyoni, nenda kwenye kanisa la watu waliookoka KWELIKWELI kama T.A.G au E.A.G.T kisha wambie watumishi UNATAKA KUOKOKA, kisha watakuongoza kupokea wokovu.
NB: Si kila tatizo linaweza kutibiwa kwa dawa. Mengine yanasababishwa na nguvu za giza hivyo JINA LA YESU PEKEE LINAWEZA KUKUOKOA.
Kama kweli umeamua kuokoka kutoka moyoni, wambie wakuombee tatizo lako la ngozi, watakuombea utapona kama una imani kwamba Mungu anaweza pia kama umemaaishisha kumfata Mungu/kudumu katika wokovu mpaka mwisho wa maisha yako.
NB: Usiende kuokoka kama unakwenda kujaribu utapona au la! Bali nenda kaokoke kwa kumfata Mungu bila kujali kama atakuponya au hatakuponya. Kwani Wokovu utakupeleka mbinguni. Pia Ukiokoka Mungu anaweza kukuponya magonjwa na matatizo yako yote.
Wokovu si dini, bali ni mabadiliko ya NAFSI yanayofanywa na Mungu kwa yeyote anayempokea Bwana Yesu ili amuokoe na dhambi na jehanamu ya moto.
nitaachaje kujichukia akati vyote ulivotaja vinanihusu,post yangu ya nyuma nimeeleza jinsi nilivyoTatizo lako sio ngozi wala makovu, tatizo lako ni kujichukia. Unahitaji msaada katika hilo kwanza. Ukifanikiwa kumaliza hiyo shida, utakuwa na amani hata issue ya kupata mchumba itamalizika.
Jifunze kujikubali, kujipenda na kuwa positive. Kila Mtu ana challenges za aina fulani mwilini, ngozi ikiwa mojawapo. Kuna Mwenye chunusi kama kijana, kuna Mwenye oily skin akinawa tu uso kama kitumbua kilichopikwa Na moto mdogo, kuna anaebabuka. Yaani Dotnata na Yule twin wake wanapata wachumba wewe unakosaje? Kuna Mwenye matege, Mwenye miguu mikubwa kama nje, kuna Mwenye kifua cha kususiwa, kuna Sony flat wega, kuna Mwenye nywele kama za paka. Mwisho wa matatizo kuna Mwenye akili za kupulizia, moja haikai, mbili haisimami! Yaani wewe ngozi yako ndio unaona mwisho wa dunia?
Nimalize kwa kusema hebu Nenda hospitali kwa ajili ya ngozi. Halafu soma kuhusu eczema. Mwisho anza kujipaka olive oil ama mafuta ya nazi tu, Na usitegemee matokeo kabla ya kumaliza Mwaka. Lakini anza kujifunza kuwa positive Na mwonekano wako huku ukihesabu Yale ambayo yako vizuri kabisa kwako. Kila la kheri.