Najuta kuhamia kwangu Kerege

Magari yatatumia gesi itakuwa rahisi tu
sawa kabisa lkn Kiwanja au nyumba havitumii gesi vitapanda tu bei
enzi zetu awanu ya kwanza ilikuwa marufuku kuwa na gari, ni L/Rover 109 ya GT
ikaja marufuku Luxury car ni pick up tu tukaziona na KIA chai maharage
leo LEXUS, Noah Boxer mpaka Kerege bado mnataka kuuza nyumba, anunue hata bodaboda itajatumia gesi
lk ardhi haibadiliki
 
Yaan ukijenga huko ukiwa kijana ni lazima utarudi tu mjini!

Huyo sista angu, nilijisemea moyoni tu hivi huyu du, atapaweza kweli[emoji16]

Maana mwanzo anahamia mbwembwe kibao, miezi 6 kageuza, yuko K' nyama, nyumba kaachia mlinzi[emoji87]
Huwezi hata kupata mpangaji labda mpangaji wa elf 20 Lakini wa Malaki hawapo
 
Unaamua kulala dukan [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] life hili bana
 
Hata mpangaji kakosa, kaweka familia ya masai wanaishi bure!

Sio Siri anajuuta!
Hana sababu za kujuta, pamoja na kuwa nyumba ni asset ambayo return yake ni lifetime, mji huu unakuwa kwa kasi sana. Huko mnakodhani ni mbali leo, ndani ya 15yrs mtashangaa na huyo sister hatajuta.
 
πŸ˜…πŸ˜…..mie nimechakaa balaa...kwakweli bora ukae kimya! Tuna kauvivu kakutoka nje uone unataka tafuniwa tu..hela haiwez mfata mtu wa aina hii kamwe..!never!

Yaani ukisoma hizi nyuzi za taabu wanazopata hawa watu wanaoishi dar hadi utawaonea huruma! Mtu unaishije KILOMETA 50 kutoka unapofanyia kazi? Halafu kazi yenyewe ya mshahara duuuh hapana aisee bora ata iwe ni biashara yako. Hapo ukifika ofisini kwanza umechokaaaa balaa! Ukichelewa ukutane na bosi tena akuwakie daah aisee maisha ya dar sio kabisa..! Sema sasa uwakute watu wa dar walivyo na mashauzi wakija mikoani kumbe mtu huko dar anaishi porini πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kweli kila mtu anawaza ajuavyo yeye...yaan nipewe laki 2 kwa mwezi??hapana...!ila kuna biashara kichaa sana...labda ujenge nyumba ukopee mkopo mzuri benk...mwee huyo laki 2 mm naipata kwa siku 1!nah!
Mimi nafeli wapi kupata hiyo 200k daily 😒😒😒
 


Hhahaa kerege sio porini..sema kuna kaumbali..ukipanda mwenge ukiamua kulla unalala had unaota kbs.. I knw the place vilivyo!
 
Kujenga nje ya mji kuna kanuni zake zitazokufanya ufurahie maisha hayo.

1. Hakikisha una eneo la kubwa kutosha ujasiriamali si unakaa nje ya mji then umejibana kama unakaa Tandale.

2. Fanya uzalishaji mdogo mdogo, hakikisha hela ya kula na mafuta inatokea eneo unaloishi mf. unafuga mifugo mbali mbali kama kuku, bata, mbuzi na hata kanga na njiwa.

Pia, lima lima kwa kutumia mbolea za mifugo unayozalisha mf. mboga mboga, mazao ya muda mfupi madawa kama mlonge na matunda na uyoga na pia kufuga kambale kwenye mifuko.

3. Tumia usafiri utaokuzalishia, wengine wanalalamikia gari inachoka lakini amini usiamini hutagharamikia mafuta na hata shida ndogondogo zitatuliwa na mapato yatokanayo na usafiri huo huo hasa ukitumia gari zenye siti nyingi kama noah, alphard, hiace, etc. Usitumie gari ndogo kama sienta, cube cubic au spacio hizo zinakufa haraka sababu zinaelemewa mno.

4. Ishi kwa kusoma timing ya foleni ya barabara unayotumia, mfano unaweza kutoka kazini saa kumi jioni lakini ukakuta barabara haipitikia kwa foleni ila ukitoka kumi na moja kamili tu unakuta ishafunguka.

5. Hakikisha unajenga nyumba kiuchumi, ili kadiri mji unavyokua unaweza kubalisha na kuweka appartments ( kuna Mzee anajuta katika hili, katawanya mjumba ambao hauna kazi kwa sasa wala faida kama angejenga kiuchumi katika lile eneo na kipindi hiki angeweka appartments)

Huwa nakaa na kuongea na waliomudu maisha ya aina hii, nimejikuta nayaelewa sana!
 
Kama unao uwezo wa kuendelea kupanga rudi sinza, shida ni nini. vinginevyo shukuru hata kupata kwako pa kujihifadhi bila bughudha za kudaiwa kodi
 
Kama hivi mkuu me nirudi kupanga tena sinza si Dish litakuwa limeyumba!


Angalizo kama wewe sio mpokea rushwa ni mfanyakazi,mfanyabiashara, kama bado unahitaji kunywa pombe kila siku utajuta!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…