Najuta kumtia umasikini Mama yangu

Amesoma darasa Moja na mama yangu. Huko kijijini Kwao singida.

Napambana sana ndugu yangu ila Kila siku naanza upya. maisha ni magumu...sana😭😭😭​
 
Sema tu una tafuta kazi ili uweze msaidia mama Kwa namna ambayo unaweza

Kama wewe anaweza kukwambia mcheki fulani basi nawe mpe jukumu amcheki Hugo CEO wa Bank Ili upate kupunguza ukali wa maisha

Endelea kupambana bila kuchoka, sali sana, usijifungie ndani, tafuta watu na marafiki sahihi, Kazi zipo nyingi ila ajira ni chache
 
ndio atakua anaumia uchumi wako hauko vizuri, ila hakutakii mabaya

wewe endelea kupambana tu unadhani anataka ukate tamaa?
 
Kwani kusoma usekretare kuna uhusiano gani na mimba? Usektretare sio shule ya msingi au sekondari. Angeendelea kusoma na mimba yake
Aliesoma na cheti alipata ila mfadhiri wake aligoma kumtafutia kazi kwakuwa alikuwa na mimba. Ikaonekana kuwa amewatia aibu kupata ujauzito akiwa na umri mdogo.​
 
Sijaelewa umemtia umasikini vipi mama yako?

Kimsingi kauli hiyo ingetoka kwa baba yako ama mama yako mwenyewe ingemake sense...wao ndio wamefanya mchakato wa wewe kupatikana

Enwei,endelea kupambana,kujuta haikusaidii kitu
 
Walipotezana muda sana tokea miaka ya 80 huko juzi hapa ndio amemuona kwenye simu yake smart phone. Ndio akanipa historia Yao yeye na mh. Ruth Zaipuna kuwa walikaa dawati Moja kipindi wanasoma.

Hivyo Hana ata mawasiliano yake.​
 
Badili fikra zako sasa hivi.
Badilisha mindset yako.

Akli yako inachokiamini mara nyingi ndicho kinachokwenda kutkutokea.. mana mawazo yako yana athiri maamuzi yako...

Huwezi ukawaza kufeli maisha yako yote harafu ukafaulu, ni ngumu sana ...

Jitahidi ubadili sana mawazo yako, mtazamo wako, na fikra zako kuhusu maisha ya kimasikini unayoishi... na maisha unayoyafikiria kuishi hapo baadaye..

Tafuta connection za kutengeneza wee mwenye , sehemu zote kwenye flows ya pesa.. pesa utaipata tu..
Connection ya kufahamiana na watu muhimu itachangia sana kubadili hali yako, tabia yako, mawazo yako(unyonge, umasikini)
Ukiwa na marafiki mwizi, au tapeli, kwa namna mmoja ama nyingine kama una ambatana sana na watu hawa... kuna uwezekano mkubwa na wewe mfumo wako wa maisha uka athiriwa nao..!

Mambo yanayotutokea yanachangiwa pia na aina ya wtu tunaofahamiana nao!!!

Punguza maisha ya lawama, malalamiko, unyonge na huzuni..

Usilaumu mtu yyte kuhusu maisha yako kwasasa.

Usiwe mtu wa kulalamkia kila kitu.

Amini kwamba wewe ndio unatake control ya maisha yako vile unavyotaka kuwa...
Usiishie tu kutamani kuishi maisha fulani bali hakikisha unapambana uishi maisha uyatakayo..

La msingi zingatia mindseti yako inawaza nini muda wote usiruhu mawazo hasi yakutawale muda wote ... hayana faida na wala hayabadilishi chochotekatika maisha yako .. zaidi ya kukuathiri tu katika mamuzi yako ya mambo katika maisha na kukuanda kufei kwasababu ndivyo akili yako inavyowaza.
 
Kujitoa akili kunalipa, tena kunalipa hasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…