Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

hapana mkuu mimi pia ninahali hiyo, ni miguu yote eneo lote la unyayo. sikumbuki chochote kinacholeta hali hiyo,

mara kwanza /kupata joto kuwaka moto miguuni ni 2002.

Kutoka hapo hadi leo hii miguu inawaka moto nikiw nimepujipunzisha, au usiku nikiwa nimelala.

nikiwa busy sipati hii hali.

naisaidieni

Ulitumia dawa yoyote kabla ya hapo?Nakushauri ukacheki kisukari!Jichunguze pia miguu yako ina muonekano gani?imevimba?kuna mishipa imejitokeza?

Kunavitu tofauti vinavyoweza kusababisha hali hio kama atheroscleorisis on exermites n.k
 
Nikemeza hedex au dicloper navimba macho,tatizo ni nini?
 
Sasa doctor kunasiku ulisema kwamba wanawake wajisafishe uken kwa kutumia sabuni zenye low pH hzo sabuni zinaitwaje?

Na wakijisafishia sabun za kawaida madhara yake ni yapi? Naomba ufafanuzi
 
Ulitumia dawa yoyote kabla ya hapo?Nakushauri ukacheki kisukari!Jichunguze pia miguu yako ina muonekano gani?imevimba?kuna mishipa imejitokeza?Kunavitu tofauti vinavyoweza kusababisha hali hio kama atheroscleorisis on exermites n.k

asante ila nimehindua daktari wa kwanza ni mim mwenyewe.
 
Hello Dinazarde,
HSG(hysterosalpingogram) ni X-ray inayotumika kuangalia ndani ya kizazi(uterus) na mirija ya kizazi(fallopian tubes).Njia hii mara nyingi inatumika kwa wanawake wenye matatizo ya kubeba ujauzito.Unapofanyiwa procedure hii rangi maalum(inayoleta mabadiliko ya rangi na mwanga(contrast) inatumika na mrija nyembamba unaowekwa kwenye uke mpaka kwenye mfuko wa uzazi ambapo picha zinachukuliwa kwa kutumia X-ray(fluoroscopy) pale rangi inapopita kwenye mfuko wa uzazi na mirija ya uzazi.Picha zinazopigwa znaonesha majeraha yaliyopo kwenye mfuko wa uzazi na hata kama kuna mapungufu/kasoro kwenye eneo hilo.Unaweza kuona pia kama kuna kitu kinazuia mayai kufika kwenye mirija ya uzazi,hatimae kuzuia shahawa kufika kwenye mirija ya uzazi ili kupevusha yai.

IVF(In vitro fertilisation) ni njia inayotumika kurutubisha yai kwa kutumia mbegu ya kiume nje ya mwili.Njia tofauti zinatumika kusaidia kuchochea mayai ya mwanamke kuwa tayari kwa kupevushwa.Mayai ya mwanamke yanatolewa kwenye kizazi yaliyotayari kupevushwa na shahawa zinatumika kurutubisha yai kwenye maabara.Yai lilorutubishwa linaachwa lipevuke kwa siku 2-6 kisha linarudishwa ndani ya kizazi cha mwanamke kwa dhumuni la ujauzito.

Ahsante kwa kunielekeza nasikia ukifanyiwa hiyo HSG inauma sana pia kuna dawa moja kwa moja wanaingiza ili kutibu na kusafisha mirija,?je ni kweli inasaidia maana kwa sasa wengi wanahangaika kupata ujauzito au akipata unatoka

Je ni njia salama kufanya hicho kipimo?na kwa hapa Tanzania hicho kipimo kinapatikana hospital zote au baadhiii?
 
mkuu naomba kujua tiba ya "keloidi", imeota kifuani na siipendi.....
 
Sasa doctor kunasiku ulisema kwamba wanawake wajisafishe uken kwa kutumia sabuni zenye low pH hzo sabuni zinaitwaje? Na wakijisafishia sabun za kawaida madhara yake ni yapi? Naomba ufafanuzi
Jaribu kutafuta FEMINA INTIMATE WASH AU LACTACYD INTIMATE WASH.Ukitumia sabuni ya kawaida inakuwa na perfumes na pH ya juu ya ngozi ya kawaida approximately 5,5 inaweza kusababisha unbalance ya normal flora inayoweza kupeleka fungus,Kuongezeka kwa discharges kwenye uke n.k
 
Doctor mm ninampenzi wangu ila tatizo tunapokuwa tunafanya mapenzi Mara nyingi anakuwa analalamika kwamba anaumia sana.

Hii hali inasababishwa na nini? Tafadhar naomba unisaidie
 
Ahsante kwa kunielekeza nasikia ukifanyiwa hiyo HSG inauma sana pia kuna dawa moja kwa moja wanaingiza ili kutibu na kusafisha mirija,?je ni kweli inasaidia maana kwa sasa wengi wanahangaika kupata ujauzito au akipata unatokaJe ni njia salama kufanya hicho kipimo?na kwa hapa Tanzania hicho kipimo kinapatikana hospital zote au baadhiii?
Rangi inayowekwa na mrija ili kuwekwa kwenye kizazi na mirija ya uzazi ni IODINE X-RAY DYE kwa lugha sahihi inatakiwa iweze kupita kwenye mirija ya uzazi kama hakuna kitu kinachofunga mirija hio, na kama kuna kitu kinazuia/kufunga mirija hio hio dye haitoweza kupita.

Nadhani ndio unamaanisha kusafisha mirija.Hii iodine dye haifungui njia kma imefungwa au kuna matatizo kwenye mirija.Ni kawaida kuhisi maumivu kama ya siku za hedhi ukifanyiwa kipimo hiki lakini unaweza kupatiwa ibuprofen au sedative ili ikusaidie urelax.

Kiwango cha maumivu kinatokana na matokeo daktari aloyapata na jinsi process nzima ilivyokwenda. Kuna risk tofauti ambazo zinaweza kutokea.Kabla ya procedure hii unaweza uombwe usaini mkataba ambao unaafiki kukubaliana risk ya procedure hii na kukubali matokeo yake.
  • Kuna asilima ndogo ya cells au tissue kuwa damaged ambazo zinazoanikwa kwenye mionzi ya X-ray.Asilimia hio ni ndogo sana ukilinganisha na faida za procedure hii.
  • Kuna chances za kupata pelvic infection,endometritis(infection/inflammation kwenye mji wa uzazi),Salpingitis(infection/inflammation kwenye mirija ya uzazi,na hali hii huwatokea zaidi wanawake ambao walishawahi kupata Pelvic infection awali.Daktari anaweza kukupatia antibiotic akiwa na hofu juu ya hili.
  • Kuna chances za kupata majeraha kwenye mfuko wa uzazi au kwenye mirija ya uzazi during procedure
  • Kuna chances ya kupata allergic reaction ya Iondine X-ray dye.
 
Nikemeza hedex au dicloper navimba macho,tatizo ni nini?
Hakuna athari ya macho kuvimba inajulikana inawezekana ni athari mpya mojawapo ya dawa au inawezekana una tatizo jingine ambalo halihusiani na dawa.

Nakushauri uangalie expiry date ya dawa kabla hujazitumia!
 
mkuu naomba kujua tiba ya "keloidi", imeota kifuani na siipendi.....
Tiba zipo nyingi na tofauti lakini zinazoweza kupatikana Tanzania ni monthly steroid(bethamethasone) injections au upasuaji.

Njia nyingine zinazoweza kutumika ni-Laser therapy -Radiation therapy-silicon plasters-compression bandages n.k
 
Tiba zipo nyingi na tofauti lakini zinazoweza kupatikana Tanzania ni monthly steroid(bethamethasone) injections au upasuaji.Njia nyingine zinazoweza kutumika ni-Laser therapy -Radiation therapy-silicon plasters-compression bandages n.k

Thanks Doctor
 
Hakuna athari ya macho kuvimba inajulikana inawezekana ni athari mpya mojawapo ya dawa au inawezekana una tatizo jingine ambalo halihusiani na dawa.Nakushauri uangalie expiry date ya dawa kabla hujazitumia!

Asante sana ndugu.Naomba unisaidie mwanangu joto limepanda sana meno ya mwisho yanaota,nilimpima damu yupo okey,tatizo nini? Nimempa panadol linatulia kidogo then linazidi.Naomba ushauri.
 
Asante sana ndugu.Naomba unisaidie mwanangu joto limepanda sana meno ya mwisho yanaota,nilimpima damu yupo okey,tatizo nini? Nimempa panadol linatulia kidogo then linazidi.Naomba ushauri.
Endelea tu kumpima joto akivusha 39 degrees mpe tena panadol.Homa ikivuka 40 degrees centigrade muwashishe hosp!
 
Hellow doctor, pole na majukumu na ahsante kwa kutupa elimu nzuri kuhusu masuala ya afya.

Mimi ni mwanaume, nina miaka ishirini na kitu; nimekuwa nikisumbuliwa na tatizo la chunusi muda mrefu.

Nimetumia sabuni kadhaa zenye viwatilifu (medicated soap) km Ayu, Give, Family na Rungu. Si hivyo tu nimetumia pia baadhi ya dawa zinasosadikiwa zinaondoa chunusi km Eskino. Zote hizo hazijanisaidia kwani ndo km ziliongeza tatizo.

Naomba unisaidie kunijuza km kuna dawa zingine ambazo zinaweza kuniondolea tatizo la chunusi. Nitaomba kujua pia km zitakuwa na side effects.
 
Back
Top Bottom