Nakemea mavazi ya kinazi aliyovaa Mr Blue kwenye video ya Mawe

Nakemea mavazi ya kinazi aliyovaa Mr Blue kwenye video ya Mawe

bahati93

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
1,334
Reaction score
2,463
Habari ya asubuhi wanajamii.

Kuna mambo mengi sana ya kuiga hapa duniani lakini kuna mengine siyo ya kuiga kabisa kama jambo ambalo amefanya Mr Blue kuvaa mavazi ya kinazi kwenye video ya music inayokwenda kwa jina MAWE akiwa kashirikishwa yeye pamoja na RayVanny na msanii wa kitaa ambaye [kitaa kinamwamini kama kiongozi wa Dini] Nyandu Tozi.

Na yeye sio wa kwanza kwa vijana wa kitanzania kuonyesha kufurahishwa sana na Adolf Hilter bila kujua zaidi juu ya mtu huyu.

Kwanza kabla ya yote yapaswa kujua ya kwamba NAZI walikuwa watu walioamini katika falsafa ya kutokuwepo usawa baina ya binadamu. Waliamini binadamu hatujaumbwa sawa na muumba, waliona baadhi ya binadamu ni bora kuliko wengine hivyo binadamu walio bora ndio wapate malazi malezi bora pasipo kujali binadamu wa mataifa mengine.

Katika mpangilio wao wa ubora wa binadamu waliona wazungu wenye nywele blonde, warefu wenye asili ya Aryan ndio bora wakifuatiwa na wazungu wengine huku watu wa mwisho kwa ubora wakiwa ni Waafrika, Wahindi na Waisrael inasikitisha kuona msanii mkubwa kuvaa mavazi ya watu hawa.

Mbali na sera hizo za kibaguzi za NAZI jambo lingine kubwa la kuzingatia ni kiongozi wao mkatili Adolf Hilter. Ipo wazi endapo nchi ikiongozwa na kiongozi katili basi na nchi inakuwa katili kwa raia waishio ndani yake.

Huyu dubwana Adolf Hilter alikosa kabisa heshima kwa binadamu wengine wenye asili tofauti na Germany aliona binadamu wengine ni kama sisimizi ambapo angeweza kuwa flush mara moja kwenye uso wadunia.

Mtu kama huyu sio wa kuigwa wala kushabikiwa kabisa kwani kila mmoja anajua ambavyo anajisikia vibaya akidharauliwa sasa huyu anakunyima na haki ya kuishi kabisa ni uovu kiasi gani.

Hata hivyo yeye mwenyewe hakuwa pure Aryan lakini bado akasababisha uharibifu mkubwa (kama sio ukichaa ni nini sasa)

WATU WA KUBEBA LAWAMA
Designer wa mavazi katika shooting hiyo yawezekana mr blue siye aliyechagua hayo mavazi bali alivalishwa na mshauri wa mavazi. Na kutokana na ujinga wao kuhusu historia wakajikuta wanatenda jambo ambolo limeniudhi sana.

Yapaswa kutokushadadia jambo bila kufanya uchunguzi wa kutosha kuepuka fedhea kama hizi. Ona sasa Mr Blue anaonekana vibaya.

Mwenye wimbo (NYANDU TOZI). Hii ni ngoma kali ambapo ulikuwa unamrudisha tena Nyandu kwenye charti ilibidi amake sure kila jambo linaenda sawa. Sasa ona na yeye anaonekana vibaya kwa kuruhusu mavazi ya Mr Blue kupoteza dira kabisa ya ngoma yake.

Na sidhani kama stesheni kubwa zinazojielewa zinawezaa kuweka uchafu wa fikra katika mavazi Mr Blue. Hii ngoma itaishia hapa tuu nchini na sidhani kama hilo ndio lilikuwa wazo la bwana Nyandu MAKO kweli kweli.

BASATA hawa naona wamekalia kuzuia maungo ya kike tu yasionekane mambo ya msingi kama kuchafuliwa kwa picha mgando na mavazi kuashiria UNAZI wapo kimya hata hawaelewi majukumu yao yapaswa wapigwe MAWE. Hizi ndio ilikuwa pointi ya kuchukua kuonyesha ukomavu wao katika kulea wasanii wetu.

Ona sasa na wao wanakuwa na makosa, BASATA yapaswa kustopisha mara moja video ya wimbo huu.

WANA WA ISRAELI
Maskini namwonea huruma Mr Blue wana wa vita wakiamua kumshukia, kutokana na ujinga wake. Watu wengi sana walikuwa wahanga wa sera za kinazi amboko Israel walipoteza ndugu zao yapata million sita huku kwa ujumla vita vilivyosababishwa na huyo dubwana Hilter vikileta jumla ya vifo million arobaini.

Usione hizi number za vifo ni rahisi kuzichapa na kuzitamka machungu yake hayaelezeki ni machozi kiasi gani wamelia watoto ambao walipoteza wazazi wao kaka zao dada zao katika vita vile ? Ni huzuni kiasi gani waliyopata wahanga wa sera hizo kipindi hicho.

Tuache ujinga wa kushabikia mambo pasipo kujua undani wake.

 
Ajabu tuna waisrael weusi......ndio falasha Jews sijui ... Japokuwa hata wale walioletwa Israel from Ethiopia wanatengwa Kama mizoga na wengi wamefungwa vizazi .....

.........Heil Hitler..........
 
Mh imebidi niende cheki nadhan blue alitaka kua controversial ila hajui jinsi hii jamii ilivyoishika entertainment industry.na kibaya zaidi ni kuwekwa kwenye youtube channel ya so called international artist rayvanny....its career suicide...sijui lakin ngoja mda uwe hakimu
 

Attachments

  • Screenshot_2019-12-12-10-01-14.png
    Screenshot_2019-12-12-10-01-14.png
    84.2 KB · Views: 7
bahati93,
Kwa sisi Hitler hajafanya lolote baya, kama huzuni inapaswa kutoka kwa kile King Leopold na Cecil Rhodes walichofanya kwetu Waafrika. Ila kw sababu hatujafanya documentation ya history zetu ndio maana tunaona ubaya wa Hitler ambae kwa Leopold anasoma.
 
Nazi praising ni offensive kwa nchi za magharibi. Sisi wengine tunajipendekeza tu.

Kibongo bongo we dont n shouldnt giv a shit!

Maana mtu mweusi alichukuliwa/ anachukuliwa inferior sio tu na Hitler bali hata na hao waliochakatwa na kuuwawa nae.

Kwa hiyo mwisho wa siku, wazungu, waarabu, waisrael, wa-asia, wooote walituchukulia hivyo hivyo tu kama hitler.
Sasa kwa nini tuomboleze kwa ajili ya watu ambao walituona tu sawa na Nazi walivyotuona.

Kwetu sisi dunia nzima haikuwa tofauti na NAZI.

Sent using LF Electromagnetic Waves
 
A
Ajabu tuna waisrael weusi......ndio falasha Jews sijui ... Japokuwa hata wale waliotolewa Israel from Ethiopia wanatengwa Kama mizoga na wengi wamefungwa vizazi .....

.........Heil Hitler..........
Acha uongo nani amefungwa vizazi
 
Adolf Hitler hakuwahi kutarget Afrika, na wala katika sera zao Afrika yetu haimo, yeye alikuwa anawapambania watu wake huko Ulaya, sasa wewe magomvi ya watu wengine yanakuhusu nini? Waachie wenyewe Wazungu na Wayahudi walumbane, ugomvi wao unatoka mbali na una historia ndefu.
Kwa taarifa yako tu, Wayahudi walifukuzwa Uingereza, Uispania, Ufaransa na Ulaya nzima Wayahudi walikuwa ni maadui, kwanza Uingereza na Ufaransa walikuwa ni second class citizen.

Mambo ya nazism sisi hayatuhusu, isitoshe usichokijua labda A.Hitler alikuwa ana sapoti kubwa ya English monarchy, wote ni nazi.

Malkia wa England na Adolf Hitler
1576135479184.jpeg



English monarchy Malkia Elizabeti akiwa mtoto wakipiga nazi salute.

1576135629972.jpeg

Huyo hapo Malkia wenu wa English commonwealth akisalute Adolf Hitler!

1576135715314.jpeg
 
We mzee hivi unajua wanachofanywa waafrika walioenda bahati mbaya Israel? Afu mbona wayahudi hawana shobo na Afrika. Nishatazama channels kibao za Israel miaka miwili mfululizo kipindi cha uharibifu wa Gaza. Mpaka leo nasoma Haaretz na machapisho yao, kote uko hawajawahi itaja Afrika labda Misri tu

Sent from my PBCM30 using Tapatalk
 
A

Acha uongo nani amefungwa vizazi
Soma Brother....vitu vipo online hivi ..

Na hii ya kusema Hitler hivi Mara Hitler vile......huwezi kujua ukweli wa Mambo Hadi uwe race/jamii husika.

Hitler and his Nazi party were doing what they did for reasons better knowing to themselves........

Pengine Ni sababu Kama za upinzani Hapa nchini kutaka kuondoka utawala wa CCM au Kama Black South Africans kuwatoa makaburu madarakani...............

By the way nguo Ni nguo tu.....let the youth enjoy...it is their time.
 
Hitler alifanya lipi baya kwa waafrika?
Waafrika wangapi waliteseka na hata kupoteza maisha kipindi cha utumwa amerika na ule wa waarabu?
mara ngapi waafrika wanabaguliwa hata leo ila bado unaleta chuki zako kwa Hitler ambaye hana historia dhidi ya Afrika
Ishu ya Adolf Hitler na Wayahudi kuivalia njuga nachelea kusema kuwa ni kujipendekeza tu
 
rr3,
Kwa hiyo unaamini kila ukionacho au kukisoma mtandaoni? Puuuu
 
Kwa sisi Hitler hajafanya lolote baya, kama huzuni inapaswa kutoka kwa kile King Leopold na Cecil Rhodes walichofanya kwetu Waafrika. Ila kw sababu hatujafanya documentation ya history zetu ndio maana tunaona ubaya wa Hitler ambae kwa Leopold anasoma.
Kama binadamu inabidi kushikana mkono pamoja pale binadamu wenzetu wanaponyanyaswa . Huu ndio ubinadamu sijui tafsiri yako ya ubinadamu
 
Kama binadamu inabidi kushikana mkono pamoja pale binadamu wenzetu wanaponyanyaswa . Huu ndio ubinadamu sijui tafsiri yako ya ubinadamu
Kwa ubinadamu ni sawa kabisa kukemea ila tukija katika ukweli you only feel the pain hasa kutoka kwa yule aliyekutenda.. Kama Waafrika Hitler alikua just another villain....
 
Nazi praising ni offensive kwa nchi za magharibi. Sisi wengine tunajipendekeza tu.

Kibongo bongo we dont n shouldnt giv a shit!

Maana mtu mweusi alichukuliwa/ anachukuliwa inferior sio tu na Hitler bali hata na hao waliochakatwa na kuuwawa nae.

Kwa hiyo mwisho wa siku, wazungu, waarabu, waisrael, wa-asia, wooote walituchukulia hivyo hivyo tu kama hitler.
Sasa kwa nini tuomboleze kwa ajili ya watu ambao walituona tu sawa na Nazi walivyotuona.

Kwetu sisi dunia nzima haikuwa tofauti na NAZI.

Sent using LF Electromagnetic Waves
Ina bidi kuwa concern pale haki za kuzaliwa za binadamu zinapovunjwa.
Sasa unafikiri nani ataheshimu jamii yako kama nayo haieshimu jamii nyingine
 
Adolf Hitler hakuwahi kutarget Afrika, na wala katika sera zao Afrika yetu haimo, yeye alikuwa anawapambania watu wake huko Ulaya, sasa wewe magomvi ya watu wengine yanakuhusu nini? Waachie wenyewe Wazungu na Wayahudi walumbane, ugomvi wao unatoka mbali na una historia ndefu.
Kwa taarifa yako tu, Wayahudi walifukuzwa Uingereza, Uispania, Ufaransa na Ulaya nzima Wayahudi walikuwa ni maadui, kwanza Uingereza na Ufaransa walikuwa ni second class citizen.

Mambo ya nazism sisi hayatuhusu, isitoshe usichokijua labda A.Hitler alikuwa ana sapoti kubwa ya English monarchy, wote ni nazi.

Malkia wa England na Adolf Hitler



English monarchy Malkia Elizabeti akiwa mtoto wakipiga nazi salute.


Huyo hapo Malkia wenu wa English commonwealth akisalute Adolf Hitler!
Kwanza Germany ilikuwa na plan na africa, we unafikiri vita ya pili ilukuwa juu ya mambo gani?
Pili huyo unayedai ni queen ni duke, je wajua tofauti ya queen na duke?
Mambo yanayohusu haki za binadamu ni ya wote labda kama wewe ni mbuzi
 
Back
Top Bottom