Kung fu panda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2019
- 748
- 785
kwaiyo mambo yaiyotokea enzi za hitler yanakuumiza wewe mpaka unawapangia watu wavae nini kwenye biashara zao za muziki,s h e n z i
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pia kwenye kitabu chake alisema juu ya kuchanganyika kwa watu ndani ya germany hivyo kuona taifa likipoteza identity yake.Nimesoma kitabu alichoandika Adolf Hitler chote kinaitwa ,,mein Kampf “. My fight, ambacho ndiyo kama road map ya aliyonuia kuyafanya, na humo ndani sikuona neno, Afrika, yeye maadui zake wakubwa walikuwa ni communist ambao walikuwa wameshamiri Ulaya na tayari walishachukuwa Urusi, hata hiyo Vita ilikuwa ni kuzuia Communism isichukuwe Ulaya, Vita ambayo hata leo hii USA wanaipigana hawataki communism.
Kuhusu mambo ya race, Wazungu wote waliamini wao ni superior, ngoja nikuulize ni nani alianzisha apartheid huko AK? Unajua kwamba Mandela alikuwa kwenye list ya terrorist kama vile Osama bin Laden? Mpaka Reagan anaondoka Mandela alikuwa ni terrorist kwa USA, unajua kuhusu all white policy ya Australia? Mpaka miaka ya 70’ Australia walikuwa hawaruhusu non white kuhamia, je ni Hitler alitawala Australia? USA mpaka miaka ya 60’ walikuwa hawaruhusu non whites kuhamia huko, waliruhusu only arian white european, je, ni Adolf Hitler alitawala USA? Kanada ni hivi juzi tu ndo iliruhusu non whites kuhamia na kuishi huko mwanzo ilikuwa ni aryan white european only, je, ni national socialist ya Adolf Hitler iliyotawala Kanada?
Unajua kwamba Wayahudi na Wazungu wote wa Ulaya walisapoti apartheid? Je, huyo ni Adolf Hitler?
Je, unajua kwamba immigrants wa Afrika huko Israel wenye asili ya Ethiopia ( ethiopian Jews) wametolewa kizazi kwa nguvu na Serikali ya Kiyahudi ili wasiendeleze kizazi huko Israeli? Je, ni Adolf Hitler amefanya hivyo? Ni nani aliyefanya lynching ya black people in USA? Ni Adolf Hitler?
Pia kwenye kitabu chake alisema juu ya kuchanganyika kwa watu ndani ya germany hivyo kuona taifa likipoteza identity yake. Sasa mnakuwa na kiongozi ambaye anakupangia mtu wa kumwoa na kuwa na watoto kisa anataka watu wenye mwonekano fulani. Hivi kweli binadamu apangiwe azalishwe kama tunavyowafanyia kuku, ngombe. Sasa kuna maana gani ya kuwa na utashi sisi kuwa tofauti na wanyama. Yatupasa kujua ya kuwa hakuna mwanadamu mwenye solution juu ya namna gani tuishi. Hivyo basi ni vyema kutokuingilia mambo ambayo yapo ndani ya haki za msingi za binadamu.
Ndugu au unaungana na sera za kinazi
Kuhusu wazungu kubagua hii ilitokana na kutokuelewa kwa nadharia za darwin (zilikua bado hazijakomaa) hata hivyo wengi wamekiri makosa na binadamu tunaenda mbele .
Mwenzako akinyolewa yapaswa ufanye niniNimeshaiongelea hiyo, nimesema Afrika pekee ambayo iluathiriwa na Vita kuu ilikuwa ni Misri Afrika ya Kaskazini, lkn Afrika yetu Kusini mwa Sahara hatuna uhusiano na hiyo vita, hakuna bomu wala risasi hata moja iliyofika kwetu, hivyo haituhusu ni Vita ya Ulaya, Asia Japani huko.
Mwenzako akinyolewa yapaswa ufanye nini
Nakataa sio wazungu wote waliokuwa wanaaminiNi lazima kwanza utambue hicho kitabu kiliandikwa lini, kipindi hicho Wazungu wote walikuwa wanaamini hiyo, na ndo maana USA kulikuwa na segregation laws, USA ilikuwa hairuhusiwi kisheria Mtu mweusi kuoa/olewa na aryan Mzungu, na siyo USA tu, Ulaya yote ilikuwa hivyo.
Unafikiri apartheid maana yake nini?
Adolf Hitler hakuanzisha Ubaguzi au superiority ya Wazungu, ilikuwepo kabla ya Hitler, na ndo maana nikakwambia USA, Australia, Kanada na New Zealand na Paraguay, Chile, Argentina ilikuwa hauruhusiwi kisheria kuhamia huko kama wewe siyo ,,aryan stock”, yaani asili ya Ulaya.
Nothern afrika
Nakataa sio wazungu wote waliokuwa wanaamini
Ukija ufaransa unataka kuniambia walikuwa wanaamini hilo unalolikazania
Ukija northern amerika u anafikiri kulikuwa kuna mambo hayo. Katika mifano mibovu ni huu wa america coz amerika waliingia kwenye civil war kuhusu chain zifunguliwe kwa mtu mweusi.
Abrahamu Lincoln great american leader mungu amrehemu. Na ni miaka arobain baada ya kupata uhuru mwafrica marekani alikombolewa.
Kutokana na mambo ya kitamaduni siku zote yanaenda taratibu sana ndio maana kulikuwa na matukio ya hapa na pale ya ubaguzi. Ata kwetu mambo ya kitamaduni ni ngumu kuisha haraka cheki mabinti wavyokeketwa na serikali inavyopambana.
Hitler hakuuwa jews peke yake,alichochea hate ya jews ambayo ilikuepo toka mwanzo,alihalalisha mateso,mauaji ya jews hivo kupelekea jews kuuliwa na kunyanyaswa na raia wenzaoThe Jews Holocaust was a hoax . You guys have been misled by the main stream media . It's true that Hitler was a mad fanatic in bizarre beliefs like aryanism an he truelly hated non white individuals but he didn't kill the Jews in such massive scale
Sent using Jamii Forums mobile app
Habari ya asubuhi wanajamii.
Kuna mambo mengi sana ya kuiga hapa duniani lakini kuna mengine siyo ya kuiga kabisa kama jambo ambalo amefanya Mr Blue kuvaa mavazi ya kinazi kwenye video ya music inayokwenda kwa jina MAWE akiwa kashirikishwa yeye pamoja na RayVanny na msanii wa kitaa ambaye [kitaa kinamwamini kama kiongozi wa Dini] Nyandu Tozi.
Na yeye sio wa kwanza kwa vijana wa kitanzania kuonyesha kufurahishwa sana na Adolf Hilter bila kujua zaidi juu ya mtu huyu.
Kwanza kabla ya yote yapaswa kujua ya kwamba NAZI walikuwa watu walioamini katika falsafa ya kutokuwepo usawa baina ya binadamu. Waliamini binadamu hatujaumbwa sawa na muumba, waliona baadhi ya binadamu ni bora kuliko wengine hivyo binadamu walio bora ndio wapate malazi malezi bora pasipo kujali binadamu wa mataifa mengine.
Katika mpangilio wao wa ubora wa binadamu waliona wazungu wenye nywele blonde, warefu wenye asili ya Aryan ndio bora wakifuatiwa na wazungu wengine huku watu wa mwisho kwa ubora wakiwa ni Waafrika, Wahindi na Waisrael inasikitisha kuona msanii mkubwa kuvaa mavazi ya watu hawa.
Mbali na sera hizo za kibaguzi za NAZI jambo lingine kubwa la kuzingatia ni kiongozi wao mkatili Adolf Hilter. Ipo wazi endapo nchi ikiongozwa na kiongozi katili basi na nchi inakuwa katili kwa raia waishio ndani yake.
Huyu dubwana Adolf Hilter alikosa kabisa heshima kwa binadamu wengine wenye asili tofauti na Germany aliona binadamu wengine ni kama sisimizi ambapo angeweza kuwa flush mara moja kwenye uso wadunia.
Mtu kama huyu sio wa kuigwa wala kushabikiwa kabisa kwani kila mmoja anajua ambavyo anajisikia vibaya akidharauliwa sasa huyu anakunyima na haki ya kuishi kabisa ni uovu kiasi gani.
Hata hivyo yeye mwenyewe hakuwa pure Aryan lakini bado akasababisha uharibifu mkubwa (kama sio ukichaa ni nini sasa)
WATU WA KUBEBA LAWAMA
Designer wa mavazi katika shooting hiyo yawezekana mr blue siye aliyechagua hayo mavazi bali alivalishwa na mshauri wa mavazi. Na kutokana na ujinga wao kuhusu historia wakajikuta wanatenda jambo ambolo limeniudhi sana.
Yapaswa kutokushadadia jambo bila kufanya uchunguzi wa kutosha kuepuka fedhea kama hizi. Ona sasa Mr Blue anaonekana vibaya.
Mwenye wimbo (NYANDU TOZI). Hii ni ngoma kali ambapo ulikuwa unamrudisha tena Nyandu kwenye charti ilibidi amake sure kila jambo linaenda sawa. Sasa ona na yeye anaonekana vibaya kwa kuruhusu mavazi ya Mr Blue kupoteza dira kabisa ya ngoma yake.
Na sidhani kama stesheni kubwa zinazojielewa zinawezaa kuweka uchafu wa fikra katika mavazi Mr Blue. Hii ngoma itaishia hapa tuu nchini na sidhani kama hilo ndio lilikuwa wazo la bwana Nyandu MAKO kweli kweli.
BASATA hawa naona wamekalia kuzuia maungo ya kike tu yasionekane mambo ya msingi kama kuchafuliwa kwa picha mgando na mavazi kuashiria UNAZI wapo kimya hata hawaelewi majukumu yao yapaswa wapigwe MAWE. Hizi ndio ilikuwa pointi ya kuchukua kuonyesha ukomavu wao katika kulea wasanii wetu.
Ona sasa na wao wanakuwa na makosa, BASATA yapaswa kustopisha mara moja video ya wimbo huu.
WANA WA ISRAELI
Maskini namwonea huruma Mr Blue wana wa vita wakiamua kumshukia, kutokana na ujinga wake. Watu wengi sana walikuwa wahanga wa sera za kinazi amboko Israel walipoteza ndugu zao yapata million sita huku kwa ujumla vita vilivyosababishwa na huyo dubwana Hilter vikileta jumla ya vifo million arobaini.
Usione hizi number za vifo ni rahisi kuzichapa na kuzitamka machungu yake hayaelezeki ni machozi kiasi gani wamelia watoto ambao walipoteza wazazi wao kaka zao dada zao katika vita vile ? Ni huzuni kiasi gani waliyopata wahanga wa sera hizo kipindi hicho.
Tuache ujinga wa kushabikia mambo pasipo kujua undani wake.
Dah nasikitika sana unavoniambia hivo,mimi ni kama wewe bro,source yangu ya information haiwezi kua mainstream media.Ndo maana nimekwambia mainstream media imemislead watu wengi including you
Sent using Jamii Forums mobile app