Nakubaliana na hoja ya Spika: Serikali iajiri walimu wengi wa kiume kuliko wanawake

Nakubaliana na hoja ya Spika: Serikali iajiri walimu wengi wa kiume kuliko wanawake

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Juzi spika aligusia kidogo suala la ajira kwa walimu na kuishauri serikali kutoa kipaumbele cha ajira kwa walimu wengi wa kiume kuliko wanawake.

Hoja ya spika ina mashiko kwa sababu nature 'asili' ya wanawake wengi hupenda raha na sio wavumilivu wa mazingira magumu.

Kwakuwa uhitaji wa walimu kwa sasa ni maeneo ya vijijini, serikali inapowaajiri walimu wa kike katika maeneo hayo baada ya muda huyakimbia kwa kuomba uhamisho wa kufuata wenza wao ambao wanafanya kazi mijini.

Kwakuwa rate ya walimu wa kike wanaohama ni kubwa ndio maana shule za vijijini zinakosa walimu wa jinsia hiyo kwa sababu asilimia kubwa wamerundikana shule za mjini ambako walihamia kwa kisingizio cha kufuata wenza wao.

Si hivyo Tu, hali hii pia huleta usumbufu kwa walimu wa kiume wanaofanya kazi vijijini kwani hukataliwa na walimu wa kike kwa kuamini kuwa endapo watawakubalia na kuishi kama wana ndoa wataendelea kuishi kijijini. Hivyo walimu wengi wa kike hulazimika kutafuta wenza walioko mjini ilikusudi wahame hali inayopelekea walimu wa kiume walioko vijijini kukosa fursa ya kuoa walimu wenzao.

Kumbe ni sahihi kabisa serikali ikatoa kipaumbele kwa walimu wa kiume kwa sababu ni wavumilivu wa mazingira ya vijijini kuliko wanawake ambao wakiajiriwa baada ya muda wanahama na hivyo kusababisha tatizo la uhaba wa walimu kwa shule za vijijini kubaki pale pale
 
Upo sahihi na ukifuatilia walimu waliopo vijijini huko vijiji vigumu ni wanaume unakuta shule ina wanafunzi 500+ walimu wanaume shule nzima wapo wanne ajira mpya hizi wapewe kipaumbele walimu wakiume waende huko kwenye uhaba wa walimu. Tutashangaa TAMISEMI kupanga ajira za walimu shule za mijini na sehemu nzuri zenye walimu wengi kuliko shule za pembezoni zenye uhitaji mkubwa wa walimu. Pelekeni hao wanaume wakapige kazi.
 
Ubaguzi kwenye ajira dhidi ya Wanawake si suluhisho bali Serikali iboreshe mazingira ya vijijini ili kurahisisha maisha. Na mtu akitaka kuhama kituo cha kazi ni haki yake na ziko sababu nyingi tu za kumfanya muajiriwa aamue kuhama kutoka kituo A na kwenda kituo B.
Juzi spika aligusia kidogo suala la ajira kwa walimu na kuishauri serikali kutoa kipaumbele cha ajira kwa walimu wengi wa kiume kuliko wanawake.

Hoja ya spika ina mashiko kwa sababu nature 'asili' ya wanawake wengi hupenda raha na sio wavumilivu wa mazingira magumu.

Kwakuwa uhitaji wa walimu kwa sasa ni maeneo ya vijijini, serikali inapowaajiri walimu wa kike katika maeneo hayo baada ya muda huyakimbia kwa kuomba uhamisho wa kufuata wenza wao ambao wanafanya kazi mijini.

Kwakuwa rate ya walimu wa kike wanaohama ni kubwa ndio maana shule za vijijini zinakosa walimu wa jinsia hiyo kwa sababu asilimia kubwa wamerundikana shule za mjini ambako walihamia kwa kisingizio cha kufuata wenza wao.

Si hivyo Tu, hali hii pia huleta usumbufu kwa walimu wa kiume wanaofanya kazi vijijini kwani hukataliwa na walimu wa kike kwa kuamini kuwa endapo watawakubalia na kuishi kama wana ndoa wataendelea kuishi kijijini. Hivyo walimu wengi wa kike hulazimika kutafuta wenza walioko mjini ilikusudi wahame hali inayopelekea walimu wa kiume walioko vijijini kukosa fursa ya kuoa walimu wenzao.

Kumbe ni sahihi kabisa serikali ikatoa kipaumbele kwa walimu wa kiume kwa sababu ni wavumilivu wa mazingira ya vijijini kuliko wanawake ambao wakiajiriwa baada ya muda wanahama na hivyo kusababisha tatizo la uhaba wa walimu kwa shule za vijijini kubaki pale pale
 
Ubaguzi kwenye ajira dhidi ya Wanawake si suluhisho bali Serikali iboreshe mazingira ya vijijini ili kurahisisha maisha. Na mtu akitaka kuhama kituo cha kazi ni haki yake na ziko sababu nyingi tu za kumfanya muajiriwa aamue kuhama kutoka kituo A na kwenda kituo B.
Hili limesababisha baadhi ya vijiji kukosa walimu kwa miongo kadhaa wakipelekwa wanachomoa
 
Wakati mwingine kuwa najiuliza kama wachangiaji wengine kweli walizaliwa na wanawake? Na mtazamo wao kwa mama, shangazi, dada na/au wake zao ukoje? Wanatia sana aibu na wanasikitisha sana pia. Ikiwa mawazo ya wanaume wengi ni kama hayo basi tuendako kama taifa ni kubaya.

Amandla...
 
Wa kulaumiwa ni Serikali Rais mshahara wake ni zaidi ya milioni 400 kwa mwaka hakatwi kodi, Mawaziri na Wabunge wana mishahara mikubwa nao na marupurupu manono hawalipi kodi, kila baada ya miaka mitano wanalipwa zaidi ya milioni 300 kama kiinua mgongo hawakatwi kodi. Fikiria wangepunguza hii mishahara yao, marupurupu na viinua mgongo na kuanza kulipa kodi ni kiasi gani kama nchi tungeweza kuboresha maisha kule vijijini na kufanya maisha kuwa rahisi kwa Watanzania wengi? Lakini wapi! Wahuni wachache wanaendelea kufaidi cake ya Taifa huku wakijiita eti SERIKALI YA WANYONGE! 😳
Hili limesababisha baadhi ya vijiji kukosa walimu kwa miongo kadhaa wakipelekwa wanachomoa
 
Kuna watu wana chuki na wanawake hadi inatisha Mkuu.
Wakati mwingine kuwa najiuliza kama wachangiaji wengine kweli walizaliwa na wanawake? Na mtazamo wao kwa mama, shangazi, dada na/au wake zao ukoje? Wanatia sana aibu na wanasikitisha sana pia. Ikiwa mawazo ya wanaume wengi ni kama hayo basi tuendako kama taifa ni kubaya.

Amandla...
 
Ubaguzi kwenye ajira dhidi ya Wanawake si suluhisho bali Serikali iboreshe mazingira ya vijijini ili kurahisisha maisha. Na mtu akitaka kuhama kituo cha kazi ni haki yake na ziko sababu nyingi tu za kumfanya muajiriwa aamue kuhama kutoka kituo A na kwenda kituo B.
Kama serikali bado inaendelea kuboresha mazingira ya vijijini unafikiri ni suluhisho gani kwa sasa linatakiwa lifanywe angalau shule za vijijini nazo zipate walimu wa kutosha kwa sababu kila serikali ikizipangia walimu wa kike baadaye huzikimbia na kurudi mijini. Katika kutatua hii changamoto nimeshauri waajiriwe walimu wengi wa kiume ila wewe unasema ni ubaguzi. Je unafikiri ni kipi kifanyike kwa wakati huu ambao mazingira ya vijijini sio rafiki kumaliza tatizo la walimu shuleni???
 
Nchi hii ina miaka 60 tangu tupate uhuru, kwa miaka 60 kipi kimefanywa ili kuboresha hali ya maisha vijijini? Kundi la wahuni wachache linaendelea kufaidi cake ya Taifa na kuwa mamilionea na mabilionea wakati hali ya mazishi vijiji vyote nchini inazidi kudidimia.
Kuboresha mazingira sio suala la siku moja sasa kwa kipindi hiki ambacho mazingira bado hayajaboreshwa unafikiri nini kifanyike kutatua tatizo la uhaba wa walimu shule za vijijini???
 
Wa kulaumiwa ni Serikali Rais mshahara wake ni zaidi ya milioni 400 kwa mwaka hakatwi kodi, Mawaziri na Wabunge wana mishahara mikubwa nao na marupurupu manono hawalipi kodi, kila baada ya miaka mitano wanalipwa zaidi ya milioni 300 kama kiinua mgongo hawakatwi kodi. Fikiria wangepunguza hii mishahara yao, marupurupu na viinua mgongo na kuanza kulipa kodi ni kiasi gani kama nchi tungeweza kuboresha maisha kule vijijini na kufanya maisha kuwa rahisi kwa Watanzania wengi? Lakini wapi! Wahuni wachache wanaendelea kufaidi cake ya Taifa huku wakijiita eti SERIKALI YA WANYONGE! [emoji15]
Very sad, Alafu mwisho wa siku wanasema tatizo la elimu duni ni mtaala.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom