Zanzibar 2020 Namba 5: Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi achukua fomu kuwania Urais wa Zanzibar

Zanzibar 2020 Namba 5: Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi achukua fomu kuwania Urais wa Zanzibar

maji hufuata mkondo, huyu ndiye rais ajaye wa Zanzibar.
 
Sawa lakini huyu hana tone la uarabu sasa zamu hii tulitaka mwenye asili ya uarabu tumechoka na waswahili tu.. Nakumbuka kuna yule mmoja shemeji yake alikuwa rais kule alishawahi kujigamba tena bungeni kwamba yeye ni mwarabu tena wa Oman wakati baba yake alikuwa Mnyamwezi tena mweusi kuliko hata mimi
Uyu ndo rais sasa
 
Dr. Hussein Mwinyi ni kiongozi wa pekee aliyeonyesha umahiri wa ajabu na nidhamu isiyo na mfano hata baada ya kukaa kwa muda mrefu sana kwenye nafasi za juu za uongozi. Kwakweli kwa mtu mwenye dhamira njema atakubaliana nami kuwa hicho ni kipaji. Very humble, obidient, understanding, asiye jikweza pamoja na kutoka kwenye familia ambayo imepata previllage ya kutoa Rais wa awamu ya pili, yet he maintained his composure...Siyo rahisi na ni wachache wa namna yake.

All the best kiongozi na Mungu akutangulie katika adhma yako hii njema ya kuwania nafasi ya juu zaidi huko Zanzibar, naamini Mungu hatakuacha wala kukupungukia.

huko Zanzibar labda akawe raisi wa kuteuliwa na Magufuli, hana uwezo hata wakupata 20% YA KURA
 
Haki wanayo, kwani wamekatazwa kugombea? Au hao ambao baba zao walikua viongozi katiba haiwaruhusu kugombea?

kugombea sio tatizo, tatizo ni kukamatwa mkono na kupitishwa kwa kupitia nguvu za familia zao.
 
Choice yangu mimi ni Prof Mbarawa.
Huyu baba ni jembe jmani. Wazanzibar wamshawishi huyu baba achukue form. Anaju kazi na pia hajikwezi.. Yuko simple and humble... Ataipeleka Zanzibar mbali..

Wazanzibari hawana habari na CCM mkuu
 
Ni miaka mitano then ataswitch kuja URT kama amiri jeshi mkuu wa URT from 2025-2030, like father like son. Bonge la Rais, amepikwa na akapikika.Kudos Daktari
Nimefurahi sana. Aje arejeshe umoja wa kitaifa. Ninaamini hatakuwa anagawa watu kikanda na kuwabagua na kuwatusi na kuwasimanga hadharani. Vyeo atatoa kwa watu wote bila kubagua kanda fulani. Inshallah Hussein uliyekuzwa kimaadili.
 
Wanamuogopa au? huyu si mzaliwa wa Tanganyika? Lile sharti la Awe mkaazi za Zanzibar na awe na Kitambulisho cha Mzanzibari mkaazi
Kifupi anacho kitambulisho na ana makazi Zanzibar na huwa wanakuwa huko pia. Kikubwa hana showoff hivyo yatakuwa Zanzibar hutadikiakelele. Anakuja mara kibao tu na familia hasa mkek wake kwa sasa maana watoto wanasoma nje.
 
Mkuu Bora huyu awe raisi, amekulia kwenye mazingira ya uongozi, hawa wengine akina kajambakoti wakipewa madaraka ni wasumbufu sana, nadhani mifano unaijua.
You hit the nail. Halafu siyo mbwembwe kwake maana uongozi alishauzoea. Na busara tele. Ninaamini hawezi kuwa mtu wa vinyongo na visasi.
 
Huyo ndio mbadala wa shein
Zanzibar kwa umwinyi ni balaa next time atakuw mtoto wa shein
Akitulia atakuwa Ally Karume ila kwa sasa Mwinyi ndiyo atakuwa Rais kwa sababu ya utulivu wake watoto wa Karume amewachafulia sana dada yao Fatuma kwa umalaya wake na kubwabwaja hovyo kila uchao utadhani hakulelewa na Mzee Karume.
 
mtakuja kushangaa huyu hussein mwinyi anakoso nafasi ya urais anachaguliwa na magufuli kuwa mgombea mwenza wake (makamo wa rais )
 
Mbunge wa Kwahani na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa katika serikali ya awamu ya Tano Dkt. Hussein Mwinyi achukua fomu kwa lengo la kuwania nafasi ya Urais wa Zanzibar katika ofisi za chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui mjini Unguja.

Vipi Makame Mbawala Kachukua Form?
 
KWA TAARIFA YAKO TUU

Rais wa Zimbabwe Mh Emmerson Dambudzo Mnangagwa na Rais wa Zambia Edgar Lungu waliwahi kushika wadhifa wa WAZIRI WA ULINZI kwenye nchi zao

Kila la kheri #DrHusseinMwinyi

Vitalis Konga(Mwana Vasamwenda)
Njombe Mjini
IMG_20200618_023036_452.jpg
 
Back
Top Bottom