Nassor Elbahsany
Member
- Sep 12, 2022
- 15
- 33
Utangulizi
Ilikuwa ni majira ya saa 12 za asubuhi, baada ya kutoka zangu msalani, niliamua kusikiliza taarifa ya habari kutoka shirika la Utangaazaji la Ujerumani (DW Swahili) kama ilivyokuwa kawaida yangu. Sababu ya kupenda kwangu kusikiliza habari ni kutokana na shauku yangu ya kutaka kufahamu matokeo mbali mbali yanayotokezea ulimwenguni. Miongoni mwa habari ninazozipenda zaidi ni zile zinazohusu bara letu la Afrika, kwani ni miongoni mwa mabara yenye changamoto nyingi ulimwenguni.
Katika asubuhi hii wakati nikisikiliza habari, nilisikia habari mbalimbali, kama vile mzozo wa Urusi na Ukrain, na migogoro mengine mingi, lakini cha kushangaza, mingi ya migogoro hiyo inalihusu bara letu la Afrika. Miongoni mwa migogoro hiyo ni kama vile migogoro ya Sudani, Kongo na Somalia. Katika jambo lililonisikitisha na kunihuzunisha zaidi, ni kwa namna gani mizozo hiyo hulitafuna bara letu la Afrika kwa kiwango kikubwa. nikajiuliza kwa nini Afrika ina migogoro mingi kuliko sehemu nyengine?
Ili kuweza kujibu suali hili linahitajika jicho la tatu kwa ajili ya kuelewa, kwani wengi wetu tunaamini mabeberu pekee ndio sababu ya migogoro Afrika, ambao husababisha migogoro ili wapate kuuza silaha zao na kuzichukua rasilimali za Afrika kwa wepesi, wakati sisi tukiwa katika migogoro iliyosababishwa na mataifa hayo makubwa.
Jambo hili ni la kweli na wala halipingiki, ya kwamba mabeberu husababisha kuengezeka kwa mizozo na mivutano Afrika, lakini pia zipo sababu ambazo sisi wenyewe huwa ni chanzo cha migogoro na mivutano hiyo, miongoni mwa sababu hizo ni kukosekana kwa uwajibikaji na utawala bora katika nchi nyingi za Kiafrika, jambo ambalo husababishwa na baadhi ya viongozi wenye uchu wa madaraka. Kwa mfano kukosekana kwa uwajibikaji, uroho wa madaraka, tamaa, rushwa, visasi, nk ndivyo vilivyosababisha majenerali wawili wa kijeshi nchini Sudani kuigeuza nchi yao kuwa uwanja wa vita.
Majenerali hawa ambao hawajali utu wala thamani ya mwanaadamu, walioamua nchi yao kuifanya vifusi, mizinga na silaha nzito nzito kama kwamba ndio burudani kwa raia wake, huku vifo na mauwaji kuwa malipo kwa raia wanyonge wa Sudan. Majenerali hawa ni Abdel Fattah al-Burhan, kiongozi wa Kikosi cha Wanajeshi wa Sudan (The Sudanese Armed Forces - SAF) na Mohamed Hamdan Dagalo, anayejulikana zaidi kama Hemedti, mkuu wa Kikosi cha Dharura (RSF).
Majenerali hawa ni miongoni mwa mifano ya baadhi ya viongozi wa Afrika, kwa namna ambayo hugeuka chanzo cha migogoro, katika bara lililobarikiwa kila aina ya rasilimali lakini bado likiendelea kuwa masikini wa kutupwa. Mifano hii pia inapatikana katika nchi kama vile, Somalia, Kongo (DRC), Sudani ya Kusini, Burundi na Afrika ya Kati.
Zipo sababu za wazi zinazoonesha ya kwamba wapo baadhi ya viongozi ambao hugeuka janga katika nchi zao badala ya kuwa neema, miongoni mwa sababu hizo ni kama zifuatazo
Zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zinaweza kupunguza mizozo na umasikini Africa.
Raia na viongozi wote wa Afrika, wana dhima na kazi kubwa ili kuhakikisha nchi zao zinakuwa huru kutokana na mizozo isiyo na msingi ili kuhakikisha nchi zao zinapata maendeo endelevu. Kwani uthabiti wa nchi hupelekea kupata maendelea ya haraka na endelevu. Vile vile raia na viongozi wote kwa pamoja wajitahidi kadri ya uwezo wao kutokuingia katika mivutano na migogoro isiyo ya msingi kwa ajili ya maendeleo yao na vizazi vijavyo.
Ilikuwa ni majira ya saa 12 za asubuhi, baada ya kutoka zangu msalani, niliamua kusikiliza taarifa ya habari kutoka shirika la Utangaazaji la Ujerumani (DW Swahili) kama ilivyokuwa kawaida yangu. Sababu ya kupenda kwangu kusikiliza habari ni kutokana na shauku yangu ya kutaka kufahamu matokeo mbali mbali yanayotokezea ulimwenguni. Miongoni mwa habari ninazozipenda zaidi ni zile zinazohusu bara letu la Afrika, kwani ni miongoni mwa mabara yenye changamoto nyingi ulimwenguni.
Katika asubuhi hii wakati nikisikiliza habari, nilisikia habari mbalimbali, kama vile mzozo wa Urusi na Ukrain, na migogoro mengine mingi, lakini cha kushangaza, mingi ya migogoro hiyo inalihusu bara letu la Afrika. Miongoni mwa migogoro hiyo ni kama vile migogoro ya Sudani, Kongo na Somalia. Katika jambo lililonisikitisha na kunihuzunisha zaidi, ni kwa namna gani mizozo hiyo hulitafuna bara letu la Afrika kwa kiwango kikubwa. nikajiuliza kwa nini Afrika ina migogoro mingi kuliko sehemu nyengine?
Namna Baadhi ya Viongozi Wanavyogeuka kuwa Chanzo cha Migogoro Afrika
Ili kuweza kujibu suali hili linahitajika jicho la tatu kwa ajili ya kuelewa, kwani wengi wetu tunaamini mabeberu pekee ndio sababu ya migogoro Afrika, ambao husababisha migogoro ili wapate kuuza silaha zao na kuzichukua rasilimali za Afrika kwa wepesi, wakati sisi tukiwa katika migogoro iliyosababishwa na mataifa hayo makubwa.
Jambo hili ni la kweli na wala halipingiki, ya kwamba mabeberu husababisha kuengezeka kwa mizozo na mivutano Afrika, lakini pia zipo sababu ambazo sisi wenyewe huwa ni chanzo cha migogoro na mivutano hiyo, miongoni mwa sababu hizo ni kukosekana kwa uwajibikaji na utawala bora katika nchi nyingi za Kiafrika, jambo ambalo husababishwa na baadhi ya viongozi wenye uchu wa madaraka. Kwa mfano kukosekana kwa uwajibikaji, uroho wa madaraka, tamaa, rushwa, visasi, nk ndivyo vilivyosababisha majenerali wawili wa kijeshi nchini Sudani kuigeuza nchi yao kuwa uwanja wa vita.
Majenerali hawa ambao hawajali utu wala thamani ya mwanaadamu, walioamua nchi yao kuifanya vifusi, mizinga na silaha nzito nzito kama kwamba ndio burudani kwa raia wake, huku vifo na mauwaji kuwa malipo kwa raia wanyonge wa Sudan. Majenerali hawa ni Abdel Fattah al-Burhan, kiongozi wa Kikosi cha Wanajeshi wa Sudan (The Sudanese Armed Forces - SAF) na Mohamed Hamdan Dagalo, anayejulikana zaidi kama Hemedti, mkuu wa Kikosi cha Dharura (RSF).
Wanajeshi wa sudani (picha kwa hisani ya mtandao)
Majenerali hawa ni miongoni mwa mifano ya baadhi ya viongozi wa Afrika, kwa namna ambayo hugeuka chanzo cha migogoro, katika bara lililobarikiwa kila aina ya rasilimali lakini bado likiendelea kuwa masikini wa kutupwa. Mifano hii pia inapatikana katika nchi kama vile, Somalia, Kongo (DRC), Sudani ya Kusini, Burundi na Afrika ya Kati.
Sababu hasa ni zipi zinazopelekea baadhi ya viongozi kuwa ni chanzo za migogoro?
Zipo sababu za wazi zinazoonesha ya kwamba wapo baadhi ya viongozi ambao hugeuka janga katika nchi zao badala ya kuwa neema, miongoni mwa sababu hizo ni kama zifuatazo
- Ruswa: miongoni mwa sababu kubwa ambazo husababisha migogoro ni kukithiri kwa rushwa kwa baadhi ya Viongozi. Jambo hili huwafanya matajiri na viongozi kufanya watakavyo kwani hawaguswi na sheria, amesema Eunice Ajabo, mtalaam wa Kamisheni ya Uchumi ya Afrika, ECA, wakati wa uzinduzi wa ripoti kuhusu utawala bora barani Afrika, mjini Kigali, Rwanda."Ili kupambana na rushwa, Afrika inahitaji tasisi na sera za utawala bora ambazo haziangalii tu makosa yanoyofanyika ndani kwa sababu siyo waafrika tu ambao wanatenda rushwa barani humo."
- Utawala mbaya na utumiaji wa mabavu. Zipo nchi ambazo zimewahi kuongozwa kwa kupitia mkono wa chuma, hali ambayo ilipelekea kuibuka kwa mizozo na mauwaji ya watu wasiokuwa na hatia. Mfano mzuri ni Sani Abacha ambaye aliwahi kuwa dikteta wa kijeshi wa Nigeria kutoka mwaka 1993 hadi 1998.
- Uvunjifu wa haki za binaadamu kwa watawala. Baadhi ya viongozi huwa hawajali juu ya haki za binaadamu kwa raia wao. Mfano mzuri ni nchini Guinea Bissau mnamo mwaka 1998 kuliibuka mzozo mkubwa ambao uligharimu maisha ya watu wengi kutokana na viongozi na maafisa wengine wa serekali kutokujali juu ya haki za binaadamu, kama vile haki ya kuishi, haki ya kutoa maoni, na haki ya kujumuika pamoja.
- Umasikini amabo husababiswa na baadhi viongozi. Nchi nyingi za kiafrika raia wake wanaishi katika umasikini wa kutupwa huku viongozi wake wakiishi katika maisha ya kifahari na anasa za hali ya juu, na huku wakitumia mamilioni ya dola kwa mambo yao binafsi na kuwaacha wananchi wao wakishindwa kumiliki hata mlo mmoja kwa siku.
Ni kwa vipi tatizo hili linaweza kuondoka?
Zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zinaweza kupunguza mizozo na umasikini Africa.
- Uongozi imara wenye kufuata sheria. Jambo hili litasababisha wananchi kuwa huru katika kutoa maoni yao kwa serekali yao.
- Ugawaji mzuri wa rasilimali za taifa. Suala hili litapelekea wananchi wote kufurahia usawa na maendeleo katika nchi zao.
- Kuwepo na kutekelezwa kwa utawala wa sheria na haki za binaadamu. Suala la haki za binadmu litapelekea viongozi kutokuongoza kwa mkono wa chuma au kutawala kwa namna wanavyopenda wao.
- Upunguzaji wa umasikini. Miongoni mwa mambo muhimu na ya msingi ni kuhakikisha serekali inatengeneza sera mazubuti, na za uhakika kwa ajili ya kupunguza umasikini, mfano mzuri ni MKUZA kwa Tanzania.
Raia na viongozi wote wa Afrika, wana dhima na kazi kubwa ili kuhakikisha nchi zao zinakuwa huru kutokana na mizozo isiyo na msingi ili kuhakikisha nchi zao zinapata maendeo endelevu. Kwani uthabiti wa nchi hupelekea kupata maendelea ya haraka na endelevu. Vile vile raia na viongozi wote kwa pamoja wajitahidi kadri ya uwezo wao kutokuingia katika mivutano na migogoro isiyo ya msingi kwa ajili ya maendeleo yao na vizazi vijavyo.
Ramani ya Africa inayoonesha nchi ambazo zipo katika mizozo mnamo mwaka 2022 (chanzo MSNBC)
Upvote
18