ASIWAJU
JF-Expert Member
- Nov 18, 2022
- 1,938
- 1,632
Habari za saa wanachama wote.
Siku ya leo ningependa kufahamishana nanyi moja ya jambo ambalo serikali ya China katika miaka ya 1970s ilifanya ili taifa lao liweze kupata maendeleo ya kasi.
Katika miaka ya 1970s baada ya serikali ya China kuweza kurejesha ushirikiano mkubwa na mataifa ya magharibi ndipo serikali yao ilipo chukua jukumu la kuanza kupeleka wanafunzi wake bora katika mataifa ya magharibi kwa ajili ya kuweza kupata ujuzi na elimu bora katika vyuo bora vya magharibi.
Mwaka 1979 aliekuwa Rais wa China kwa wakati huo Deng Xiaoping alimpigia simu Rais wa U.S.A kwa wakati huo Jimmy Carter ili kumuomba nafasi ya vijana 5,000 wakichina kwenda kusoma U.S.A, naye Rais wa U.S.A akampatia nafasi kubwa zaidi ya vijana 100,000 wakichina kusoma U.S.A
Lengo kuu la serikali ya China kwa wakati huo ilikuwa ni kuweza kupata elimu bora sehemu mbalimbali duniani ili kuweza kulisaidia taifa lao kukua kwa kasi kutokana na kuwa nyuma na uduni mkubwa wa maendeleo walio kuwa nao kwa wakati huo.
Njia pekee walio kuwa nayo ni kupeleka wanafunzi wao bora katika mataifa yenye elimu bora na maendeleo bora kuliko wao kwa wakati huo, hii inasaidia wao kama taifa kuwa na mtaji mkubwa wa wasomi watakao rejea nchini na kuweza kutoa ile elimu bora waliopata ng'ambo na kuwa nufaisha wachina walio ndani ya nchi yao jambo linalo saidia wao kwa pamoja kupata ukuaji wa maendeleo ya kasi katika ngazi zote.
China inafanya hii mbinu hadi sasa na kwa asilimia kubwa imeleta matunda makubwa katika nchi yao kama walivyo tarajia.
Hii ni nukuu ya Rais Deng Xiaoping kuhusu hili suala.
" When our thousands of Chinese students abroad return home, you will see how China will transform itself ".
Swali:
Je Tanzania tuna yapi ya kujifunza juu ya hili jambo walilo fanya China ?
Siku ya leo ningependa kufahamishana nanyi moja ya jambo ambalo serikali ya China katika miaka ya 1970s ilifanya ili taifa lao liweze kupata maendeleo ya kasi.
Katika miaka ya 1970s baada ya serikali ya China kuweza kurejesha ushirikiano mkubwa na mataifa ya magharibi ndipo serikali yao ilipo chukua jukumu la kuanza kupeleka wanafunzi wake bora katika mataifa ya magharibi kwa ajili ya kuweza kupata ujuzi na elimu bora katika vyuo bora vya magharibi.
Mwaka 1979 aliekuwa Rais wa China kwa wakati huo Deng Xiaoping alimpigia simu Rais wa U.S.A kwa wakati huo Jimmy Carter ili kumuomba nafasi ya vijana 5,000 wakichina kwenda kusoma U.S.A, naye Rais wa U.S.A akampatia nafasi kubwa zaidi ya vijana 100,000 wakichina kusoma U.S.A
Lengo kuu la serikali ya China kwa wakati huo ilikuwa ni kuweza kupata elimu bora sehemu mbalimbali duniani ili kuweza kulisaidia taifa lao kukua kwa kasi kutokana na kuwa nyuma na uduni mkubwa wa maendeleo walio kuwa nao kwa wakati huo.
Njia pekee walio kuwa nayo ni kupeleka wanafunzi wao bora katika mataifa yenye elimu bora na maendeleo bora kuliko wao kwa wakati huo, hii inasaidia wao kama taifa kuwa na mtaji mkubwa wa wasomi watakao rejea nchini na kuweza kutoa ile elimu bora waliopata ng'ambo na kuwa nufaisha wachina walio ndani ya nchi yao jambo linalo saidia wao kwa pamoja kupata ukuaji wa maendeleo ya kasi katika ngazi zote.
China inafanya hii mbinu hadi sasa na kwa asilimia kubwa imeleta matunda makubwa katika nchi yao kama walivyo tarajia.
Hii ni nukuu ya Rais Deng Xiaoping kuhusu hili suala.
" When our thousands of Chinese students abroad return home, you will see how China will transform itself ".
Swali:
Je Tanzania tuna yapi ya kujifunza juu ya hili jambo walilo fanya China ?