Namna China ilivyoweza kujiendeleza, Tanzania tuna yapi ya kujifunza?

Namna China ilivyoweza kujiendeleza, Tanzania tuna yapi ya kujifunza?

ASIWAJU

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2022
Posts
1,938
Reaction score
1,632
Habari za saa wanachama wote.

Siku ya leo ningependa kufahamishana nanyi moja ya jambo ambalo serikali ya China katika miaka ya 1970s ilifanya ili taifa lao liweze kupata maendeleo ya kasi.

Katika miaka ya 1970s baada ya serikali ya China kuweza kurejesha ushirikiano mkubwa na mataifa ya magharibi ndipo serikali yao ilipo chukua jukumu la kuanza kupeleka wanafunzi wake bora katika mataifa ya magharibi kwa ajili ya kuweza kupata ujuzi na elimu bora katika vyuo bora vya magharibi.

Mwaka 1979 aliekuwa Rais wa China kwa wakati huo Deng Xiaoping alimpigia simu Rais wa U.S.A kwa wakati huo Jimmy Carter ili kumuomba nafasi ya vijana 5,000 wakichina kwenda kusoma U.S.A, naye Rais wa U.S.A akampatia nafasi kubwa zaidi ya vijana 100,000 wakichina kusoma U.S.A

Lengo kuu la serikali ya China kwa wakati huo ilikuwa ni kuweza kupata elimu bora sehemu mbalimbali duniani ili kuweza kulisaidia taifa lao kukua kwa kasi kutokana na kuwa nyuma na uduni mkubwa wa maendeleo walio kuwa nao kwa wakati huo.

Njia pekee walio kuwa nayo ni kupeleka wanafunzi wao bora katika mataifa yenye elimu bora na maendeleo bora kuliko wao kwa wakati huo, hii inasaidia wao kama taifa kuwa na mtaji mkubwa wa wasomi watakao rejea nchini na kuweza kutoa ile elimu bora waliopata ng'ambo na kuwa nufaisha wachina walio ndani ya nchi yao jambo linalo saidia wao kwa pamoja kupata ukuaji wa maendeleo ya kasi katika ngazi zote.

China inafanya hii mbinu hadi sasa na kwa asilimia kubwa imeleta matunda makubwa katika nchi yao kama walivyo tarajia.

Hii ni nukuu ya Rais Deng Xiaoping kuhusu hili suala.
" When our thousands of Chinese students abroad return home, you will see how China will transform itself ".
quote-when-our-thousands-of-chinese-students-abroad-return-home-you-will-see-how-china-will-de...jpg
20579839-quote-when-our-thousands-of-chinese-students-abroad-return-home-you-will-see-how-chin...jpg


Swali:
Je Tanzania tuna yapi ya kujifunza juu ya hili jambo walilo fanya China ?
 
Kwetu wakipelekwa wanazamia na kuchana passport kabisa na majina wanabadilisha ili wasirudi Tz...😂
Wa bongo tulivyo wabinasfi, tukipata hizo nafasi tunahamishia na familia zetu kabisa ughaibuni..🤣
 
Kwetu wakipelekwa wanazamia na kuchana passport kabisa na majina wanabadilisha ili wasirudi Tz...😂
Wa bongo tulivyo wabinasfi, tukipata hizo nafasi tunahamishia na familia zetu kabisa ughaibuni..🤣
Hili jambo, ili hayo yote yasitokee ina hitaji usimamizi mkubwa wa serikali kwa idadi ya wanafunzi wanao enda ng'ambo kupata elimu.
 
Kwanza kbs ni kuweka sheria kali zitazokua ni mwiba kwa viongoz na watanzania kwa ujumla wake, huez weka mising ya maendeleo kwa Taifa kwa katiba hii ambayo mtu anaiba anahujum au kufisad na bado anadunda mtaani na kupewa madaraka!!

China wanasheria kali ni kifungo maisha au kitanzi, hiyo imefany hata raia wake wawe waoga na hofu ya sheria kali ambazo zinamshughulikia hata Rais!!

NB: huez kua na taifa lenye uzalendo wakat wananchi wanaona viongoz wao wasivyokua na uzalendo na taifa lao, that's why kila mmoja akipata nafas anapiga madili cz ni kawaida kuanzia kwa wakubwa!!!
 
Magufuli angeweza sio hawa walamba asali

USSR
Bado umelewa ile brainwashing aliyowapa watanzania, nipe muhktasar wa Mahakama ya mafisad ilifunga wangap? Wakaja na njia ya kupiga pesa plea bargain 🤣🤣🤣!! China wana uzalendo na Nchi yao aidha unafungwa maisha au unanyongwa hakuna biashara ya plea bargain!!!
 
Wakati Wachina walio wengi, wanazaliwa na roho ya uzalendo mioyoni mwao; Sisi Waafrika tunazaliwa na roho ya ubinafsi, wizi, ufisadi, uchawi, majungu, ufitini, nk!

Inatia huruma sana kuona baadhi ya Mataifa yaliyokuwa na uchumi unao endana na wa kwetu, leo hii yanafikia mpaka hatua ya kutukopesha na kutusaidia katika nyanja mbalimbali.
 
Kwanza kbs ni kuweka sheria kali zitazokua ni mwiba kwa viongoz na watanzania kwa ujumla wake, huez weka mising ya maendeleo kwa Taifa kwa katiba hii ambayo mtu anaiba anahujum au kufisad na bado anadunda mtaani na kupewa madaraka!! China wanasheria kali ni kifungo maisha au kitanzi, hiyo imefany hata raia wake wawe waoga na hofu ya sheria kali ambazo zinamshughulikia hata Rais!! NB: huez kua na taifa lenye uzalendo wakat wananchi wanaona viongoz wao wasivyokua na uzalendo na taifa lao, that's why kila mmoja akipata nafas anapiga madili cz ni kawaida kuanzia kwa wakubwa!!!
Kwa hiyo tatizo ni sheria kali tu ndicho tunakosa ?
 
Wakati Wachina walio wengi, wanazaliwa na roho ya uzalendo mioyoni mwao; Sisi Waafrika tunazaliwa na roho ya ubinafsi, wizi, ufisadi, uchawi, majungu, ufitini, nk!
Kwani mkuu hivi ni vitu vya kuzaliwa navyo au ni malezi tu ya kifalsafa ?
 
Inatia huruma sana kuona baadhi ya Mataifa yaliyokuwa na uchumi unao endana na wa kwetu, leo hii yanafikia mpaka hatua ya kutukopesha na kutusaidia katika nyanja mbalimbali.
Mwarobaini ni sera na mipango inayo tekelezeka tu mkuu.
 
Habari za saa wanachama wote.

Siku ya leo ningependa kufahamishana nanyi moja ya jambo ambalo serikali ya China katika miaka ya 1970s ilifanya ili taifa lao liweze kupata maendeleo ya kasi.

Katika miaka ya 1970s baada ya serikali ya China kuweza kurejesha ushirikiano mkubwa na mataifa ya magharibi ndipo serikali yao ilipo chukua jukumu la kuanza kupeleka wanafunzi wake bora katika mataifa ya magharibi kwa ajili ya kuweza kupata ujuzi na elimu bora katika vyuo bora vya magharibi.

Mwaka 1979 aliekuwa Rais wa China kwa wakati huo Deng Xiaoping alimpigia simu Rais wa U.S.A kwa wakati huo Jimmy Carter ili kumuomba nafasi ya vijana 5,000 wakichina kwenda kusoma U.S.A, naye Rais wa U.S.A akampatia nafasi kubwa zaidi ya vijana 100,000 wakichina kusoma U.S.A

Lengo kuu la serikali ya China kwa wakati huo ilikuwa ni kuweza kupata elimu bora sehemu mbalimbali ili kuweza kulisaidia taifa lao kukua kwa kasi kutokana na kuwa nyuma na uduni mkubwa wa maendeleo walio kuwa nao kwa wakati huo.

Njia pekee walio kuwa nayo ni kupeleka wanafunzi wao bora katika mataifa yenye elimu bora na maendeleo bora kuliko wao kwa wakati huo, hii itasaidia wao kama taifa kuwa na mtaji mkubwa wa wasomi watakao rejea nchini na kuweza kutoa ile elimu bora waliopata ng'ambo na kuwa nufaisha wachina walio ndani ya nchi yao jambo litakalo saidia wao kwa pamoja kupata ukuaji wa maendeleo ya kasi katika ngazi zote.

China inafanya hii mbinu hadi sasa na kwa asilimia kubwa imeleta matunda makubwa katika nchi yao kama walivyo tarajia.

Hii ni nukuu ya Rais Deng Xiaoping kuhusu hili suala.
" When our thousands of Chinese students abroad return home, you will see how China will transform itself ".View attachment 2520467View attachment 2520468

Swali:
Je Tanzania tuna yapi ya kujifunza juu ya hili jambo walilo fanya China ?
Penye Hawa mafisadi wa kila kitu na Kupeana nafasi unatarajia wajifunze aau kuleta mabadiliko chanya!
 
Tanzania hatuna la kujifunza. Hapa Ni wizi wa mchana. Feri ya bilioni nane inakarabatiwa kwa bilioni Saba na ushee. Na hakuna kitu waziri anaweza fanywa.
Takukuru wanahangaika na walimu wanaopiga picha watoto wa shule wanaokaa chini kwenye vumbi.
 
Kuna bwana mmoja kwenye nyuzi mfanano wa hii alisema (Huezi fananisha Kinyesi na chakula)

👆🏿
 
Tanzania hatuna la kujifunza. Hapa Ni wizi wa mchana. Feri ya bilioni nane inakarabatiwa kwa bilioni Saba na ushee. Na hakuna kitu waziri anaweza fanywa.
Takukuru wanahangaika na walimu wanaopiga picha watoto wa shule wanaokaa chini kwenye vumbi.
Daaah! hatari sana, mambo bado magumu hapa nchini.
 
Back
Top Bottom