Namna China ilivyoweza kujiendeleza, Tanzania tuna yapi ya kujifunza?

Sera ya nchi kula kwa urefu wa kamba.
Ukiweza kula za plea bargaining haya,
Ukiweza kula za ukarabati wa feri haya,
Wakurugenzi wa halmashauri wanajichotea.
62 years after independence wanafunzi Dar wanakaa chini kwenye vumbi.
Fomtuu huko ukerewe hawajui kusoma na kuandika.
Kila mkubwa anatembelea V8 inakula Lita kwa kilomita tano.
 
Duuuh! Hatari sana. bado tuna mambo mengi ya kuya tatua kwanza.
 
Zamani kulikua na five year dev plan.
Siku hizi hakuna, infact we don't know our goals in the next two years.
Unajua Ni Bora MTU ukawa na plan/lengo hata Kama Ni plan mbaya.

Sisi hatuna plan yoyote, hata plan ya lini kila mtoto wetu atakalia dawati shuleni, angalau hata kwa mikoa miwili. We don't have that plan. Watu wako kwenye viyoyozi vya v8 mchana kutwa.
Rwanda iliyo start from scratch 1996 kila mtoto ana kishkwambi, sisi watoto wanakaa chini kwenye vumbi.

Sio kwamba hatuna hela, Ila hatuna priorities. Feri inakarabatiwa kwa SEVEN POINT FIVE BILLION WAKATI BEI YAKE NI 8 B.

UTASEMA TUNATUMIA AKILI?
 
Kwetu wakipelekwa wanazamia na kuchana passport kabisa na majina wanabadilisha ili wasirudi Tz...[emoji23]
Wa bongo tulivyo wabinasfi, tukipata hizo nafasi tunahamishia na familia zetu kabisa ughaibuni..[emoji1787]
Hatuna mkakati kama taifa na ndiyo maana wanafanya hivyo
 

Hiyo pekee haikuisaidia China kupata maendeleo ya haraka. Ndiyo maana miaka ya 1990, ikaamua kuja na mbinu mpya, ya kubadilisha sera zake za uchumi, na kufanya ushawishi mkubwa kwa makampuni makubwa ya America na Ulaya kwenda kuwekeza nchini China.

Uwekezaji wa mataifa ya Magharibi nchini China ulibadilisha kila kitu, na kuupandisha ukuuaji wa uchumi wa China mpaka kufikia 12%. Mpaka leo, China ndiyo inayoongoza Duniani katika kuvutia wawekezaji wa nje ya nchi yao. Uwekezaji wa mataifa ya nje nchini China, kwa mwaka ni zaidi ya dola billion 80 (linganisha na uwekezaji wa dola bilioni 3 kwa mwaka, wa juu kabisa ambao Tanzania imewahi kuupata).

Makampuni ya nje yanafurahia uwekezaji wake nchini China kutokana na sera madhubuti zisizobadilikabadilika za kulinda uwekezaji.

Mpaka sasa, nchini China kuna makampuni zaidi ya milioni moja kutoka mataifa ya kigeni.

By the end of 2020, a total of 1,040,480 foreign companies were registered in Mainland China, the Official data was provided by the Ministry of Commerce (MOFCOM).2 Nov 2021.

Kwa hiyo kilichowasaidia sana China kubadilika kwa haraka, ni uwekezaji mkubwa wa makampuni ya nje. Mpaka leo, viongozi wa China, wakati wote wapo mataifa ya kigeni kutafuta wawekezaji wa kwenda kuwekeza nchini China.
 

Hiyo pekee haikuisaidia China kupata maendeleo ya haraka. Ndiyo maana miaka ya 1990, ikaamua kuja na mbinu mpya, ya kubadilisha sera zake za uchumi, na kufanya ushawishi mkubwa kwa makampuni makubwa ya America na Ulaya kwenda kuwekeza nchini China.

Uwekezaji wa mataifa ya Magharibi nchini China ulibadilisha kila kitu, na kuupandisha ukuuaji wa uchumi wa China mpaka kufikia 12%. Mpaka leo, China ndiyo inayoongoza Duniani katika kuvutia wawekezaji wa nje ya nchi yao. Uwekezaji wa mataifa ya nje nchini China, kwa mwaka ni zaidi ya dola billion 80 (linganisha na uwekezaji wa dola bilioni 3 kwa mwaka, wa juu kabisa ambao Tanzania imewahi kuupata).

Makampuni ya nje yanafurahia uwekezaji wake nchini China kutokana na sera madhubuti zisizobadilikabadilika za kulinda uwekezaji.

Mpaka sasa, nchini China kuna makampuni zaidi ya milioni moja kutoka mataifa ya kigeni.

By the end of 2020, a total of 1,040,480 foreign companies were registered in Mainland China, the Official data was provided by the Ministry of Commerce (MOFCOM).2 Nov 2021.

Kwa hiyo kilichowasaidia sana China kubadilika kwa haraka, ni uwekezaji mkubwa wa makampuni ya nje. Mpaka leo, viongozi wa China, wakati wote wapo mataifa ya kigeni kutafuta wawekezaji wa kwenda kuwekeza nchini China.

Nchini China, ukihujumu uwekezaji, adhabu yako ni kifo. Mwekezaji nchini China analindwa kwa nguvu zote. Na bila hiyo China ingekuwa na shida kubwa ya unemployment.

Hapa kwetu, mkurugenzi wa kiwanda cha kusindika tumbaku pale Morogoro, RCO, kwa sababu za kijinga kabisa, alimweka ndani kwa masaa 8. Alipotoka tu, akaanza utaratibu wa kufunga kiwanda. Ndipo Rais Magufuli akaanza kuhangaika na kumtuma waziri kwenda kumbembeleza asifunge kiwanda, na akamtimua RCO wa mkoa wa Morogoro. Lakini hata hivyo, pamoja kutofunga, alipunguza sana uwekezaji wake, kiasi cha kuifanya tumbuka zaidi ya 50% mwaka ule ikose mnunuzi.

Wawekezaji ni wachache, Dunua nzima wanatafutwa. Ni yule mwenye mazingira mazuri ndiye anayewavuta wengi.
 
Tulipata kiongozi wa kutufikisha mbali tukamtupia mawe ya lawama hadi MUNGU kamchukua. Sasa sijui mnatakaje enyi majuha watanzania.
 
Kwanza tuachane na demokraia. Hakuna nchi ya kidemokrasia inayoweza kuendelea.
 
Tuwe na sera za kitaifa za muda mfupi na mrefu na si sera za vyama vya siasa. Chama kikishashinda uchaguzi kitakuta sera zipo tayari kwa utekelezaji, chama kitakachoshindwa kutekeleza kinapigwa chini kinaingia kingine.
 
Kwetu wakipelekwa wanazamia na kuchana passport kabisa na majina wanabadilisha ili wasirudi Tz...😂
Wa bongo tulivyo wabinasfi, tukipata hizo nafasi tunahamishia na familia zetu kabisa ughaibuni..🤣
Ni kweli lakini ingekuwa vizuri tukajiuliza sababu ya kufanya hivyo ni nini? Sababu kubwa ni kwamba mazingira ya nyumbani kiajira siyo mazuri. Na mazingira ya kiajira yanakuwa siyo mazuri kwa sababu ya uongozi na siasa mbovu. Tunatakiwa tuwe na malengo na mikakati mizuri ya uongozi ili kuvutia wale wanaokwenda kusoma. Siyo mwanafunzi anarudi baada ya kupata utaalam, anapewa eg cheo wizara ya fedha au benki kuu, rais anatoa amri fedha za uchaguzi zichotwe na mtaalam anapokataa anapelekewa watu wasiojulikana ku-deal naye.
 
Kwanza tuachane na demokraia. Hakuna nchi ya kidemokrasia inayoweza kuendelea.
You dont know what is democracy. Hujui ni nini maana ya demokrasia. Huu msomo wa ''hakuna nchi yenye demokrasia inayoweza kuendelea'' ni dhana potofu inayotumiwa na viongozi wasiotaka kukosolewa. Wengi wanadhani demokrasia ni kuachia mambo yaende msaragambo na kila mtu ajifanyie analodhani ni sahihi. Hell, no! Demokrasia ni kuwashirikisha wananchi kwenye kila hatua za uongozi na kumpa kila mtu nafasi na uwanja sawa kwenye kufanya kazi na kugawana mapato. anayefanya kazi na apate haki na asiyefanya kazi apate haki yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…