Namna nzuri ya kuingia kwenye Siasa na Uongozi

Namna nzuri ya kuingia kwenye Siasa na Uongozi

Joined
Sep 18, 2022
Posts
10
Reaction score
2
Nawasalimia kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania........

Naamini wengi wetu tuko salama na tunaendelea kupambana na maisha. Karibuni kwenye mada tusaidiane mawazo ikiwa ni elimu kwangu mleta mada, lakini pia fundisho kwa wengi wetu tunaopenda kujishugulisha na siasa na uongozi.

Mimi ni kijana mwenye miaka 30+. Elimu yangu ni shahada ya uzamili, nimesoma nje ya nchi degree ya kwanza na ya pili. Familia yangu ni familia zile za kawaida sana. Nilisoma kwa udhamini (Scholarship). Tangu nimalize elimu yangu sijafanikiwa kupata kazi ya kueleweka. Napambana hapa na pale kujikimu na maisha. Kitaaluma ni Muikolojia (Ecologist), mwenye machapisho kadhaa ya kitaama.

Ninapenda sana siasa na naamini ninao uwezo wa kuongoza. Kwa sasa sina direct affiliation na Chama cha siasa moja kwa moja. Lakini ni "active and concerned citizen" kwa maana nafuatilia kwa karibu siasa za nchi yetu. Nahisi muda umefika niingie moja kwa moja kuhudumia watu kwa njia hii.

Nimeleta mada hii hapa ili tusaidiane yafuatayo;

1. Sina network wala mtu yeyote nayemfahamu anajihusisha na siasa moja kwa moja kwenye vyama vya siasa. Naanzia wapi kufanikisha malengo yangu?

2. Je nianze kwa kujiunga na chama kimojawapo cha siasa au nianze kama mwanaharakati?

3. Namna gani naweza kujuana na wanasiasa wakubwa na nikapata mentor (kiongozi mwelekezi) kwenye siasa akanielekeza njia na kunishika mkono kuelekea kufikia malengo yangu?

4. Kama kuna marafiki humu ndani wenye network ya kisiasa naomba sana njooni PM mnishike mkono mwenzenu nipate pakuanzia.

5. Naweza kujitolea kufanya kazi either kwenye chama cha siasa au/na mwanasiasa mzoefu/mkongwe ili kujifunza siasa za field bila malipo. Hivyo kama kuna msamalia mwema wakufanikisha hili na yupo hapa au unamfahamu asisite kuja PM.

N:B. Uzoefu wangu mdogo kwenye siasa nimefanya nje ya nchi kama kiongozi kwenye serikali za wanafunzi. Siasa za nje ya nchi vyuoni hazina nguvu kama Tanzania.

Karibuni kwa mawazo na namna yoyoye nzuri kufanikisha hili.

Asante.
 
Siasa sio kazi kiongozi na wala haipo kwenye category za kazi (decent jobs)

Siasa ni SAYANSI kama sio unaijua hiyo Sayansi kiongozi nakushauri endelea kulima ngogwe (nyanya chungu) ukae kwa amani

Siasa ni hatare na ina 'up' na 'downs' zake ambazo sio discussable kama hivi na kumbuka siasa sio rahisi kama unavyodhani
 
Network anzia hapo ulipo kwa diwani wako. Hudhuria mikutano ya hapo mtaani kwako changia hoja, hoji usipoelewa, tekeleza au fatilia utekelezaji wa maazimio ya vikao hapo mtaani au kijijini ulipo[emoji16][emoji16][emoji16]. Utakuja kunishukuru baadae[emoji448][emoji448]
 
Nawasalimia kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania........

Naamini wengi wetu tuko salama na tunaendelea kupambana na maisha. Karibuni kwenye mada tusaidiane mawazo ikiwa ni elimu kwangu mleta mada, lakini pia fundisho kwa wengi wetu tunaopenda kujishugulisha na siasa na uongozi.

Mimi ni kijana mwenye miaka 30+. Elimu yangu ni shahada ya uzamili, nimesoma nje ya nchi degree ya kwanza na ya pili. Familia yangu ni familia zile za kawaida sana. Nilisoma kwa udhamini (Scholarship). Tangu nimalize elimu yangu sijafanikiwa kupata kazi ya kueleweka. Napambana hapa na pale kujikimu na maisha. Kitaaluma ni Muikolojia (Ecologist), mwenye machapisho kadhaa ya kitaama.

Ninapenda sana siasa na naamini ninao uwezo wa kuongoza. Kwa sasa sina direct affiliation na Chama cha siasa moja kwa moja. Lakini ni "active and concerned citizen" kwa maana nafuatilia kwa karibu siasa za nchi yetu. Nahisi muda umefika niingie moja kwa moja kuhudumia watu kwa njia hii.

Nimeleta mada hii hapa ili tusaidiane yafuatayo;

1. Sina network wala mtu yeyote nayemfahamu anajihusisha na siasa moja kwa moja kwenye vyama vya siasa. Naanzia wapi kufanikisha malengo yangu?

2. Je nianze kwa kujiunga na chama kimojawapo cha siasa au nianze kama mwanaharakati?

3. Namna gani naweza kujuana na wanasiasa wakubwa na nikapata mentor (kiongozi mwelekezi) kwenye siasa akanielekeza njia na kunishika mkono kuelekea kufikia malengo yangu?

4. Kama kuna marafiki humu ndani wenye network ya kisiasa naomba sana njooni PM mnishike mkono mwenzenu nipate pakuanzia.

5. Naweza kujitolea kufanya kazi either kwenye chama cha siasa au/na mwanasiasa mzoefu/mkongwe ili kujifunza siasa za field bila malipo. Hivyo kama kuna msamalia mwema wakufanikisha hili na yupo hapa au unamfahamu asisite kuja PM.

N:B. Uzoefu wangu mdogo kwenye siasa nimefanya nje ya nchi kama kiongozi kwenye serikali za wanafunzi. Siasa za nje ya nchi vyuoni hazina nguvu kama Tanzania.

Karibuni kwa mawazo na namna yoyoye nzuri kufanikisha hili.

Asante.
Japo na mimi sio mwanasiasa lakini nichangie kidogo:

Kabla ya kuambatana na,mwanasiasa au chana jiidentify wewe mwenyewe mrengobwako je unataka kuingia katika siasa kana ajira au unasimamia values fulani?

Pili kumbuka kuwa ingawa nchi yetu kikatiba ni ya vyama vingi lakini kiuhalisia vyama vingi haviruhusiwi isipokuwa vyama maslahi tu. Vyombo vyote vya kusimamia mfumo huo pamoja na vyombo vya dola vinafanya kazi kichinichini vya kusaidia chama tawala na kuwaandama wale wanaoonekana wapinzani wa kweli ; hivyo misukosuko mbalimbali, jela,/ rumande, kufukuzwa ndani ya chama au kunyimwa fursa ndani ya hicho chama utakachojiunga tegemea yatakupata..

Kama ingekuwa,mgombea binafsi anaruhusiwa na wewe kweli unataka kupigania haki basi hiyo fursa, ingekufaa.

Lakini kama nia yako ni ajir ,kupitia siasa jiunge na chama chochote, uwe mnafiki utapeta.
 
Siasa sio kazi kiongozi na wala haipo kwenye category za kazi (decent jobs)

Siasa ni SAYANSI kama sio unaijua hiyo Sayansi kiongozi nakushauri endelea kulima ngogwe (nyanya chungu) ukae kwa amani

Siasa ni hatare na ina 'up' na 'downs' zake ambazo sio discussable kama hivi na kumbuka siasa sio rahisi kama unavyodhani
Asante kwa ushauri wako mkuu. Nimekusoma vizuri sana. Actually siingii kwenye siasa kama kazi/ajira, japo nafikiri siasa za uongozi kiuhalisia ni ajira pia maana unalipwa ujira. Japo kwa muhusika/kiongozi ili ufanikiwe unatakiwa drive yako isiwe malipo bali kuhudumia watu. Lengo langu kuu ni kuhudumia watu, ninajiona ninao huo uwezo toka moyoni.
 
Network anzia hapo ulipo kwa diwani wako. Hudhuria mikutano ya hapo mtaani kwako changia hoja, hoji usipoelewa, tekeleza au fatilia utekelezaji wa maazimio ya vikao hapo mtaani au kijijini ulipo[emoji16][emoji16][emoji16]. Utakuja kunishukuru baadae[emoji448][emoji448]
Noted kaka, nachukua ushauri kama ulivyo. Asante sana!
 
Japo na mimi sio mwanasiasa lakini nichangie kidogo:

Kabla ya kuambatana na,mwanasiasa au chana jiidentify wewe mwenyewe mrengobwako je unataka kuingia katika siasa kana ajira au unasimamia values fulani?

Pili kumbuka kuwa ingawa nchi yetu kikatiba ni ya vyama vingi lakini kiuhalisia vyama vingi haviruhusiwi isipokuwa vyama maslahi tu. Vyombo vyote vya kusimamia mfumo huo pamoja na vyombo vya dola vinafanya kazi kichinichini vya kusaidia chama tawala na kuwaandama wale wanaoonekana wapinzani wa kweli ; hivyo misukosuko mbalimbali, jela,/ rumande, kufukuzwa ndani ya chama au kunyimwa fursa ndani ya hicho chama utakachojiunga tegemea yatakupata..

Kama ingekuwa,mgombea binafsi anaruhusiwa wewe kweli unataka kupigania haki basi hiyo fursa, ingekufaa.

Lakini kama nia yako ni ajir ,kupitia siasa jiunge na chama chochote, uwe mnafiki utapeta.
Asante sana kaka. Copied for action. Kwa maoni yako Chama kipi una recommend sasa baada ya maoni yako hapo juu?
 
Sasa Mkuu Elimu hiyo ya Ikolojia unatafuta kuingia kwenye siasa za maji taka za Tanzania ili upate nini?
Tafuta kuingia Mamlaka za Ngorongoro, Serengeti au TANAPA ili ule mema ya nchi bila kelele.Kuongoza nchi masikini ni shida sana,utarogwa ufe bure!
 
Kusaidia jamii hasa katika kutatua changamoto zao.
Kusaidia jamii sio lazima uwe mwanasiasa.
Wewe kama unataka ushauri ili upate kazi ya uanasaiasa sawa.
Siasa ni kazi sikuhizi na inawalipa sana tena kwa muda mfupi kulipo wafanyabiashara wa kawaida au waajiriwa wengine wa kawaida na watu wengi wanawekeza fedha nyingi sana ili kupata uongozi wa kisiasa.
Kama unafedha za kuhonga ingia.
Ila kuhusu suala lako la kusaidia jamii, sio lazima kuwa mwanasiasa, unaweza kianzisha NGO yako ukasaidia jamii vilevile
 
Kusaidia jamii sio lazima uwe mwanasiasa.
Wewe kama unataka ushauri ili upate kazi ya uanasaiasa sawa.
Siasa ni kazi sikuhizi na inawalipa sana tena kwa muda mfupi kulipo wafanyabiashara wa kawaida au waajiriwa wengine wa kawaida na watu wengi wanawekeza fedha nyingi sana ili kupata uongozi wa kisiasa.
Kama unafedha za kuhonga ingia.
Ila kuhusu suala lako la kupsaidia jamii, sio lazima kuwa mwanasiasa, unaweza kianzisha NGO yako ukasaidia jamii vilevile
Sahihi kabisa mkuu, siasa ni jambo nalipenda. Kila mtu anachagua kuisaidia jamii yake kwa namna tofauti na mimi ninapendelea kwa njia hii ya siasa. Ndiyo maana naomba mwongozo kwa upande huu.
 
Sasa Mkuu Elimu hiyo ya Ikolojia unatafuta kuingia kwenye siasa za maji taka za Tanzania ili upate nini?
Tafuta kuingia Mili niamlaka za Ngorongoro, Serengeti au TANAPA ili ule mema ya nchi bila kelele.Kuongoza nchi masikini ni shida sana,utarogwa ufe bure!
Asante kwa ushauri mzuri mkuu. Siasa ni kitu nakipenda tu. Ikolojia ni fani yangu na unaendelea kupambana kuingia mashirika/taasisi ulizopendekeza ili fani yangu pia niendelee kuitendea haki. Kama una namna ya kunisaidia au yeyote mwenye kuniwezesha pia nitashukuru sana. Kwa sisi ambao tunatoka familia za kawaida kuingia huko kuna ugumu sana bila kushikwa mkono.
 
Back
Top Bottom