Namna ya kupunguza upweke nyumbani

Namna ya kupunguza upweke nyumbani

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Binadamu yeyote anahitaji kuwa na furaha, pamoja na kuzungukwa na watu mbali mbali ambao watamfanya achangamke na kuondoa au kupunguza tatizo la msongo wa mawazo.

Hii imekuwa ikitokea kwa baadhi ya familia, baada ya kukuza watoto wao na kwenda kujitegemea, na hatimaye kuwaacha wazazi wao wakiwa wapweke huku wakizungukwa na majengo au vyumba visivyokuwa na watu.

Njia ninazoweza kuwashauri jamii ya namna hii, kugawa kiwanja au jengo katika sehemu tatu; sehemu ya kwanza inaweza kutumiwa kama karakana ya kutengeneza vitu fulani n.k.

Sehemu ya pili itakuwa makazi ya familia, na sehemu ya tatu unaweza kuweka biashara yoyote iwe ni ya vinywaji n.k

Hii itasaidia kuwa na mzunguko mkubwa wa watu, na itapunguza uwezo wa mtu kukaa pekee yake pamoja na kuwepo kwa msongo wa mawazo.

Karibuni kwa hoja
 
Huo utakuwa umejitakia tu mwenyewe; kwa mwanaume ni rahisi sana kupata mwenza wa kuishi naye na kumpa kampani kuliko mwanamke.
Kwa hiyo huo upweke wako ni wakujitakia.
Sikatai ni kweli kabisa,
Mazingira na maisha kwa ujumla yanafanya niwe hivi maana ninaweza kutoonekana mazingira ya nyumbani hata mwaka 1/2 na nikirejea nitakaa kwa 2/3 months.
 
Sikatai ni kweli kabisa,
Mazingira na maisha kwa ujumla yanafanya niwe hivi maana ninaweza kutoonekana mazingira ya nyumbani hata mwaka 1/2 na nikirejea nitakaa kwa 2/3 months.
Muhimu ni malengo, baada ya muda fulani unatakiwa utulie sehemu moja; hatukuumbwa ili tuteseke kwenye utafutaji tu.
 
Binadamu yeyote anahitaji kuwa na furaha, pamoja na kuzungukwa na watu mbali mbali ambao watamfanya achangamke na kuondoa au kupunguza tatizo la msongo wa mawazo.

Hii imekuwa ikitokea kwa baadhi ya familia, baada ya kukuza watoto wao na kwenda kujitegemea, na hatimaye kuwaacha wazazi wao wakiwa wapweke huku wakizungukwa na majengo au vyumba visivyokuwa na watu.

Njia ninazoweza kuwashauri jamii ya namna hii, kugawa kiwanja au jengo katika sehemu tatu; sehemu ya kwanza inaweza kutumiwa kama karakana ya kutengeneza vitu fulani n.k.

Sehemu ya pili itakuwa makazi ya familia, na sehemu ya tatu unaweza kuweka biashara yoyote iwe ni ya vinywaji n.k

Hii itasaidia kuwa na mzunguko mkubwa wa watu, na itapunguza uwezo wa mtu kukaa pekee yake pamoja na kuwepo kwa msongo wa mawazo.

Karibuni kwa hoja
unakuta jamaa kajenga bonge ya nyumba na kwasasa anaishi yeye na mkewe tu, hadi anaogopa nyumba yake mwenyewe 🐒
 
Back
Top Bottom