Nampenda lakini simwamini kabisa, nifanyeje?

Nampenda lakini simwamini kabisa, nifanyeje?

Njoo PM nimesadia watu wengi tuu wenye matatizo kama yako
 
Naombeni ushauri,

Mimi ni msichana wa miaka 24, nina mchumba ana miaka 29, tatizo langu ni kwamba mchumba wangu nimekuja kugundua ni muongo sana na mpaka kumgundua uwe na akili ya ziada kabisa, nimekuja kumgundua nimeshampenda tayr, na nisingekuwa nakaa naye pamoja hakika nisingemkamata, alinidanganya ana nyumba akanionyesha kabisa kumbe sio yake, akanidangany hakuwahi kuwa na mpenzi kumbe ana wapenzi wengi t, kanidangany
Ambacho nakiona, ni kuwa, kuna siku kisu kitaingia mwilini mwako.
 
Mpenzi wangu akinitishia kuniua kwa namna yoyote ile huyu ni wa kuachana nae.

Hakuna kitu chenye thamani kubwa kama uhai. Sio mume wako, sio ndgu yako, kazi unayo na bado unakazana kubaki kwa huyo muuaji mtarajiwa.

Mimi kama Vishu Mtata nakupa mwaka tu, kama ukiendelea kukaa na huyo jamaa basi ndani ya muda huo R.I.P zitakuhusu, kwasababu anakutishia kisu wakati huna makosa kabisa ni hisia zake tu, siku akikushika na kosa lolote aisee jamaa anakuua. Usijifariji eti ww hutamfanyia kosa, mtu kama huyo hata akute text ya mwanaume kweny sim yako kakusalimia ama lah akute umeongozana/ unasalimiana na mwanaume wafwa.
 
Mapenzi gani haya mbona bado mdogo hivyo ebu toka hapo dear achana na huyo mwanaume hana cha kuchanganyikiwa chochote ni usanii tu anakufanyia
 
Najua we ni mgeni hapa, huenda mwanzo ulikua kama msomaji tu,ukaona ujiunge rasmi ili uombe ushauri, hivyo nawaomba Wana Jf wasikulaumu kutokana na uandishi wako, ispokua wakushauri juu ya matatizo yanayo kukabili.
Kwani uandishi wake umeuona una matatizo gani?
 
Hapo hakuna kujiuliza achana nae tu. Tatizo kwenye hizo ndoa za umri wako ni za ju kwa juu. Yaani ukute ndugu hawajui . Kama mmeoana na ndugu wa pande zote wanajua. Washirikishe tu kwamba hiyo ndoa imekushinda kufuatana na stuation ilivyo. Watakuelewa tu.

Muhimu waambie kabisa mimi nimewaambia tu mjue kwa mambo mawili kwanza kwamba naondoka kwa huyu mtu. Pili kwa tahadhali kwa tabia alizozionyesha bado nina wasiwasi hata nikiondoka anaweza akanifuatilia.

Kwa maana hiyo watahadhalishe,wasije wakakuambia “VUMILIA NDIO NDOA ZILIVYO”. Hiyo ilikuwa zamani. Siku hizi akikutishia mara moja tu ujue ipo siku atakuua
 
Naombeni ushauri,

Mimi ni msichana wa miaka 24, nina mchumba ana miaka 29, tatizo langu ni kwamba mchumba wangu nimekuja kugundua ni muongo sana na mpaka kumgundua uwe na akili ya ziada kabisa, nimekuja kumgundua nimeshampenda tayr, na nisingekuwa nakaa naye pamoja hakika nisingemkamata,
Anza kuandaa kaburi lako,kifo kifo kifo hakina huruma
 
Kama sio unaishi na mgonjwa wa akili bhasi huyo ni psychopath...na atakuua kweli kishaa aanze kujutia wewe ukiwa maiti..ondoka haraka,au huna pa kwenda?
 
Ukishatoroka hapo kwa huyo mgonjwa mwenzio wa akili,pitia hapa kwangu nikupe mambo mkuu.
 
Kana umri gani hako kajamaa?
Kutokana na umri wake basi itakuwa wazi kama ni kichaa kweli au anaigiza.

Mostly atakuwa anaiga.
 
Naombeni ushauri,

Mimi ni msichana wa miaka 24, nina mchumba ana miaka 29, tatizo langu ni kwamba mchumba wangu nimekuja kugundua ni muongo sana na mpaka kumgundua uwe na akili ya ziada kabisa, nimekuja kumgundua nimeshampenda tayr, na nisingekuwa nakaa naye pamoja hakika nisingemkamata, alinidanganya ana nyumba akanionyesha kabisa kumbe sio yake, akanidangany hakuwahi kuwa na mpenzi kumbe ana wapenzi wengi t, kanidangany mpaka level yake ya elimu n.k,

Siku yaliponkfika shingoni nikamwambia ukweli na nikamuaga naenda sehemu nikapitie vitu vyangu kisha nielekee nyumbani nikawasalimie, kiukweli nisiwe mnafiki nilikuwa nasepa mazima. Alikubali lkn imefika usiku wa kuamkia siku ambayo naondoka akanibadilikia na tulikuwa tunacheka kabisa, ghafla akaanza kucheka akanishikia kisu usoni akabadilika kabisa lkn anacheka sana, aliniwekea tumboni akasema bora aniue tu maana ananipenda lkn nataka niache Dah kiukweli nilijitetea mpk nilichanganyikiwa, hatimaye baada ya masaa takriban mawili aliniacha akasema nikirudia atanimaliza kabisa.

Siku moja kanikuta na simu nipo instagram naangalia comments nikawa nacheka lkn limekuwa ni tatizo kwake (hili ni la muda mrefu hataki nishike simu, hajawahi kunikuta naongea na mwanaume wala kunasa msg na yeye anajua sina hiyo tabia, nikishika simu nafanya application za kazi nikichoka naingia kujiburudisha mtandaoni sasa kinamuuma sana mm kufanya hivo), hiyo siku akaanza kunigombeza, kwa kuwa ni tabia yake siku hiyo nikamwambia laivu nimechoka na hii tabia, ghafla kaanz kunipiga anasema ko imechoka kuishi na mimi, akaniumiza sana akaona haitoshi kakimbilia kisu dah! Nilipiga kelele watu wakaja ndio akaniachia.

Asubuhi kulipokicha akanifata nilipolala akaanza kulia sana ananiomba msamaha, alijutia alichokifanya mpk leo namuona hayupo sawa, nilimwambia nimemsamehe lakini aliendelea kulia baadae akanyamaz lkn anajuta hadi leo. Tangu siku anipige na kunishikia kisu namuogopa sana, simwamini tena nikimuona nawaza kuna siku ataniua, tunaweza kuwa tunacheka kabisa ghafla hali ya hofu inanitawala, nabadilika kabisa mpaka anaanza kulia tena, hio hali inanisumbua sana, akinikumbatia nakuwa na furaha ghafla tena nashikwa hofu hapohapo,namwambia aniachie, akiniletea zawadi ananiambia fumba macho ili anipe, nafumba ghafla naanza kupiga kelele nafumbua macho!

Dah of course inamuuma sana akiniona na hali hiyo lkn akili yangu najaribu kuirudisha upya imegoma kabisa, nawaza kutoroka tuu muda wowote na inaniuma kuondoka bila kumuaga nifanye je?nisaidiwe nn cha kufanya? Halafu amenihofia je nikitoroka akaninasa njian? Maana ananiwinda sana. Nampenda lakini nipo tayr kujisacrify kumuacha, nitumie njia ipi?
You are living with a psychopathy.
Run for your life
 
Back
Top Bottom