Namtumbo: Wazazi waacha kupeleka Watoto Shuleni wakiaminishwa Yesu Kristo anakaribia kurudi

Namtumbo: Wazazi waacha kupeleka Watoto Shuleni wakiaminishwa Yesu Kristo anakaribia kurudi

Kweli huwa mnaeenda kusomea ujinga, mnatutia aibu Tanzania hii
Bora nimtoe mtoto shule nimpeleke msumbiji akajishughulishe, kuliko kumtoa amsubiri tapeli mmoja alipaa na ungo
 
Labda akikuta watoto wako shule atakasirika sana manake walipenda awakute nyumbani wanamsubiri hata km ni miaka 800.
Atakua yesu wa mchongo mwanza toka apewe dozi hajaridi kila akisoma mchezo naaona ntakufa tena
 
Mtu kama huyu hastahili kuachwa hivihivi. Sijui aelimishwe kwa namna gani.

View attachment 2875334
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Malenya amefanya msako wa Wanafunzi ambao hawajaripoti Shule za Msingi na Sekondari Vijijini ambapo katika hali isiyo ya kawaida alipofika Kijiji cha Chengena kwenye msako wa nyumba kwa nyumba amebaini uwepo wa Mtumishi wa Mungu Erick Manyanya ( 33) Mwinjilisti wa Kanisa la Country Living ambaye amefungua Kanisa Kijijini hapo akiwahubira Wazazi wasiwapeleke Watoto Shule kwakuwa Yesu Kristo atarudi muda sio mrefu kuchukua kondoo wake hivyo badala ya kwenda Shule wajiandae kumpokea Yesu.

Erick ni Kijana ambaye alikuwa anasoma Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambaye anadai baada ya kusoma vitabu na kuijua imani yake vizuri akaacha Chuo na kwenda kuanzisha Kanisa hilo Namtumbo “Nimesoma UDOM sikuhitimu elimu yangu sababu ni baada ya kuijua imani yangu vizuri katika vitabu, maana tumeambiwa Mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu, mpaka nafika Chuo Kikuu nipo katika mikono ya Wazazi baada ya kujitambua Mimi nachagua njia yangu inayonipa furaha, nyakati zinazokuja chap- ya mnyama itasurutishwa, kitabu cha ufunuo wa Yohana kuna namba 666 sasa huo wakati upo karibu yetu”

DC Ngollo amesema Erick amefanikiwa kuwarubuni Wazazi mbalimbali ambao ni wa dhehebu la Wasabato Kijijini hapo na wameachisha Watoto wao Shule ili wajiandae kumpokea Yesu ambapo hadi sasa Watoto 13 tayari wameacha kwenda Shule na wameaminishwa kuwa elimu ya Mungu haipaswi kuchangamana na Elimu Dunia inayotolewa na Shule za Serikali na binafsi.

DC Ngollo akiwa na Kamati ya Usalama wa Wilaya ameagiza kukamatwa kwa Mwinjilisiti Erick na Mwinjilisti mwenzake anayemsaidia kazi za Kanisa Anthony Mkomela kwa mahojiano zaidi
Imani ni shambulio la akili
 
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Malenya amefanya msako wa Wanafunzi ambao hawajaripoti Shule za Msingi na Sekondari Vijijini ambapo katika hali isiyo ya kawaida alipofika Kijiji cha Chengena kwenye msako wa nyumba kwa nyumba amebaini uwepo wa Mtumishi wa Mungu Erick Manyanya ( 33) Mwinjilisti wa Kanisa la Country Living ambaye amefungua Kanisa Kijijini hapo akiwahubira Wazazi wasiwapeleke Watoto Shule kwakuwa Yesu Kristo atarudi muda sio mrefu kuchukua kondoo wake hivyo badala ya kwenda Shule wajiandae kumpokea Yesu.

Erick ni Kijana ambaye alikuwa anasoma Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambaye anadai baada ya kusoma vitabu na kuijua imani yake vizuri akaacha Chuo na kwenda kuanzisha Kanisa hilo Namtumbo “Nimesoma UDOM sikuhitimu elimu yangu sababu ni baada ya kuijua imani yangu vizuri katika vitabu, maana tumeambiwa Mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu, mpaka nafika Chuo Kikuu nipo katika mikono ya Wazazi baada ya kujitambua Mimi nachagua njia yangu inayonipa furaha, nyakati zinazokuja chap- ya mnyama itasurutishwa, kitabu cha ufunuo wa Yohana kuna namba 666 sasa huo wakati upo karibu yetu”

DC Ngollo amesema Erick amefanikiwa kuwarubuni Wazazi mbalimbali ambao ni wa dhehebu la Wasabato Kijijini hapo na wameachisha Watoto wao Shule ili wajiandae kumpokea Yesu ambapo hadi sasa Watoto 13 tayari wameacha kwenda Shule na wameaminishwa kuwa elimu ya Mungu haipaswi kuchangamana na Elimu Dunia inayotolewa na Shule za Serikali na binafsi.

DC Ngollo akiwa na Kamati ya Usalama wa Wilaya ameagiza kukamatwa kwa Mwinjilisiti Erick na Mwinjilisti mwenzake anayemsaidia kazi za Kanisa Anthony Mkomela kwa mahojiano zaidi
"....DC Ngollo akiwa na Kamati ya Usalama wa Wilaya ameagiza kukamatwa kwa Mwinjilisiti Erick na Mwinjilisti mwenzake anayemsaidia kazi za Kanisa Anthony Mkomela kwa mahojiano zaidi"
Nashauri: Hao wakapumzishwe pale Kingolwira miezi 6 wakati msako una endelea, halafu ndo baadaye hayo mahojiano yaendelee.
 
Mfuasi wa Kibwetele huyo.

DINI ZINA WAPUMBAZA WATU WENGI SANA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
...Wale waliohamia pale Uwanja wa Ndege Dar wakiaminidhwa na Kiongozi Wao kwamba Watakwenda sijui Jerusalem bila kuhitaji Pasipoti Miaka ya Tisini na wakaanza kuchafua Uwanja Wetu wa Ndege Kwa Vinyesi Hadi wakatimuliwa na Polisi, kumbe nao walikuwa Dini Gani ??? [emoji848][emoji848][emoji848]

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
 
Ila Wasabato bhana [emoji23][emoji23][emoji23]
Huyu jamaa alikua Msabato alikua anasali Nyegezi akahasi akafukuzwa kwa taratibu za Kanisa..Hivyo sio Mwadventista tena. ieleweke hivo kuwa sio Msabato na Wasabato wanahimiza watoto kwenda shule tena kwa mtaala wa sasa somo la dini ni la lazima kwa wanafunzi wote.
Somo linaitwa Sport Culture and Religion.
Huyo n muuni TU aliyechanganyikiwa
 
Huyu msabato wa wapi? Maana kanisa lineandikwa Country living hii itakuwa ni tafsiri yake katika maandiko sababu kanisa la Waadventista wasabato huwa linaongozwa na mchungaji katika mtaa husika, wainjilisti huwa wanapelekwa kusambaza injili lakini sio kuanzisha kanisa ili kanisa lianzishwe lazima liwe na baraka ya uongozi wa juu wa kanisa, na lazima lipewe mchungaji

Pichani ni mfumo wa kanisa kuanzia juu mpaka chini
Huyo jamaa alishahasi Kanisa akafukuzwa alikua Msabato kwa Sasa sio Msabato tena
 
Biblia yenyewe inasisitiza watoto wapewe elimu yeye hayo ya Yesu kurudi na watoto kutokwenda shule kayatoa wapi?

Akamatwe akanyee ndoo huko jela kwa kosa la kupotosha raia
 
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Malenya amefanya msako wa Wanafunzi ambao hawajaripoti Shule za Msingi na Sekondari Vijijini ambapo katika hali isiyo ya kawaida alipofika Kijiji cha Chengena kwenye msako wa nyumba kwa nyumba amebaini uwepo wa Mtumishi wa Mungu Erick Manyanya ( 33) Mwinjilisti wa Kanisa la Country Living ambaye amefungua Kanisa Kijijini hapo akiwahubira Wazazi wasiwapeleke Watoto Shule kwakuwa Yesu Kristo atarudi muda sio mrefu kuchukua kondoo wake hivyo badala ya kwenda Shule wajiandae kumpokea Yesu.

Erick ni Kijana ambaye alikuwa anasoma Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambaye anadai baada ya kusoma vitabu na kuijua imani yake vizuri akaacha Chuo na kwenda kuanzisha Kanisa hilo Namtumbo “Nimesoma UDOM sikuhitimu elimu yangu sababu ni baada ya kuijua imani yangu vizuri katika vitabu, maana tumeambiwa Mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu, mpaka nafika Chuo Kikuu nipo katika mikono ya Wazazi baada ya kujitambua Mimi nachagua njia yangu inayonipa furaha, nyakati zinazokuja chap- ya mnyama itasurutishwa, kitabu cha ufunuo wa Yohana kuna namba 666 sasa huo wakati upo karibu yetu”

DC Ngollo amesema Erick amefanikiwa kuwarubuni Wazazi mbalimbali ambao ni wa dhehebu la Wasabato Kijijini hapo na wameachisha Watoto wao Shule ili wajiandae kumpokea Yesu ambapo hadi sasa Watoto 13 tayari wameacha kwenda Shule na wameaminishwa kuwa elimu ya Mungu haipaswi kuchangamana na Elimu Dunia inayotolewa na Shule za Serikali na binafsi.

DC Ngollo akiwa na Kamati ya Usalama wa Wilaya ameagiza kukamatwa kwa Mwinjilisiti Erick na Mwinjilisti mwenzake anayemsaidia kazi za Kanisa Anthony Mkomela kwa mahojiano zaidi.

Pia soma - Ndugu yetu aliyekamatwa kwa kuzuia Watoto kwenda shule mbona hapewi dhamana na Polisi?
Another Mackenzie in town. Na bado kuna wajinga wamemwamini.
 
Wanafunzi kadhaa wa secondary na msingi, wametolewa shule na Mchungaji na Muinjilisti Erick Manyanya, pamoja na wazazi wao, wakiwa kanisani, wakimsubiri Yesu arudi, huko Namtumbo.
 
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Malenya amefanya msako wa Wanafunzi ambao hawajaripoti Shule za Msingi na Sekondari Vijijini ambapo katika hali isiyo ya kawaida alipofika Kijiji cha Chengena kwenye msako wa nyumba kwa nyumba amebaini uwepo wa Mtumishi wa Mungu Erick Manyanya (33) Mwinjilisti wa Kanisa la Country Living ambaye amefungua Kanisa Kijijini hapo akiwahubira Wazazi wasiwapeleke Watoto Shule kwakuwa Yesu Kristo atarudi muda sio mrefu kuchukua kondoo wake hivyo badala ya kwenda Shule wajiandae kumpokea Yesu.

Erick ni Kijana ambaye alikuwa anasoma Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambaye anadai baada ya kusoma vitabu na kuijua imani yake vizuri akaacha Chuo na kwenda kuanzisha Kanisa hilo Namtumbo “Nimesoma UDOM sikuhitimu elimu yangu sababu ni baada ya kuijua imani yangu vizuri katika vitabu, maana tumeambiwa Mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu, mpaka nafika Chuo Kikuu nipo katika mikono ya Wazazi baada ya kujitambua Mimi nachagua njia yangu inayonipa furaha, nyakati zinazokuja chap- ya mnyama itasurutishwa, kitabu cha ufunuo wa Yohana kuna namba 666 sasa huo wakati upo karibu yetu”

DC Ngollo amesema Erick amefanikiwa kuwarubuni Wazazi mbalimbali ambao ni wa dhehebu la Wasabato Kijijini hapo na wameachisha Watoto wao Shule ili wajiandae kumpokea Yesu ambapo hadi sasa Watoto 13 tayari wameacha kwenda Shule na wameaminishwa kuwa elimu ya Mungu haipaswi kuchangamana na Elimu Dunia inayotolewa na Shule za Serikali na binafsi.

DC Ngollo akiwa na Kamati ya Usalama wa Wilaya ameagiza kukamatwa kwa Mwinjilisiti Erick na Mwinjilisti mwenzake anayemsaidia kazi za Kanisa Anthony Mkomela kwa mahojiano zaidi.

Pia soma

Dini zingine ni majanga kwa jamii na taifa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom