Nani aliwadanganya CHADEMA wamponde Hayati Magufuli majukwaani!!? Hili jambo litawanyima kura miaka elfu

Nani aliwadanganya CHADEMA wamponde Hayati Magufuli majukwaani!!? Hili jambo litawanyima kura miaka elfu

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Inawezekana kabisa kwamba magufuli alikuwa na madhaifu yake, na inaweza isiwe dhambi kumsema vibaya. Ila kwa watu wenye malengo ya kutafuta kura Kwa wananchi wa kawaida walipaswa kupotezea kabisa habari za magufuli.

Kuna baadhi ya mambo ambayo hata Magufuli angekuwepo naamini asingebadili chochote lakini alishawaaminisha watu Imani ambayo ni ngumu kufutika katika kizazi kilichowahi kuyaona na kuyasikia maamuzi yake.

Ukweli ni kwamba kumsema vibaya Magufuli ukiondoa kujipoza machungu na kuwapoza machungu wahanga wachache wa utawala wake hakuna tija yoyote linapohusika suala la kuongeza kura.

Magufuli mwenyewe alizoea kuwasema vibaya watangulizi wake lakini alitenda jambo lililowaaminisha watu kuwa inawezekana ni kweli watangulizi wake walikuwa na shida.

Unapomponda Magufuli huku vitu vinapanda bei, umeme unakatika hovyo rushwa na urasimu na mauzauza mengi serikalini unakua hujui unalotenda.

Licha ya matatizo ya Magufuli lakini sio uongo kwamba bado ana waumini wake wengi pengine kuliko kiongozi mwingine yeyote wa hivi karibuni hapa nchini. Hivyo hata kama unamchukia kwa kiwango gani Kwa ajili ya kulinda kura ni bora ukapitezea kabisa mada zinazomhusu.
 
Licha ya matatizo ya magufuli lakini sio uongo kwamba bado ana waumini wake wengi pengine kuliko kiongozi mwingine yeyote wa hivi karibuni hapa nchini. Hivyo hata kama unamchukia Kwa kiwango gani Kwa ajili ya kulinda kura ni bora ukapitezea kabisa mada zinazomhusu
Mie sijawahi kuwaelewa hao watu wa JPM wasimpompa kura Chadema ndio watampa Samia ambaye ndio anamng'onga JPM Kila kukicha!!?

Tatizo sukuma gang hawana option wakimpigia Samia Yale Yale wakimpigia Chadema Yale Yale wote hawaivi na JPM. So hoja Yako ingekua mashiko kama kungekua na chama Cha tatu ambacho ni loyalists wa JPM but since hakipo then hakuna kura ya Chadema itapotea labda tu watu wa JPM hawatopiga kura ndio madhara pekee nayoona.
 
Tangu 2015 mpaka 2020, CHADEMA walikuwa wakimponda Magufuli na bado kura wakapewa nyingi (japokuwa ziliibiwa), sembuse sasa ambapo hata maCCM (yaliyokuwa yakimuona Magufuli kama mungu wao fulani kwa kumsifia) yamegeuka na kumtukana vibaya Magufuli.
 
Tangu 2015 mpaka 2020, CHADEMA walikuwa wakimponda Magufuli na bado kura wakapewa nyingi (japokuwa ziliibiwa), sembuse sasa ambapo hata maCCM (yaliyokuwa yakimuona Magufuli kama mungu wao fulani kwa kumsifia) yamegeuka na kumtukana vibaya Magufuli.
We jamaa una umri gani hata hujui kama magufuli ndie waziri pekee wa ccm kuwahi kusifiwa na wabunge wa upinzani
 
Mie sijawahi kuwaelewa hao watu wa JPM wasimpompa kura Chadema ndio watampa Samia ambaye ndio anamng'onga JPM Kila kukicha!!?

Tatizo sukuma gang hawana option wakimpigia Samia Yale Yale wakimpigia Chadema Yale Yale wote hawaivi na JPM. So hoja Yako ingekua mashiko kama kungekua na chama Cha tatu ambacho ni loyalists wa JPM but since hakipo then hakuna kura ya Chadema itapotea labda tu watu wa JPM hawatopiga kura ndio madhara pekee nayoona.
Wewe una hoja ila hata kama wafuasi wa magufuli wasingekuwa na chaguo chadema wangekuwa kwenye position nzuri sana kujaza hilo gap walipaswa kuja na majibu yanayopwaya sasa na si kumsengenya magufuli. Kwa akili yangu ya kawaida tu naamini Kwamba kwenye kampeni za 2025 ingawa amekufa bado atakuwa kiini kikuu cha mijadala mingi miongoni mwa wagombea
 
Kama Magufuli alikuwa na wafuasi wengi wa hivyo ni kwanini alinajisi uchaguzi? Ni hivi, uhayawani wa Magufuli utawekwa wazi bila kujali habari za kura wala nini. Isitoshe Tanzania hakuna uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Hivyo usijifiche kwenye box la kura wakati hakuna uchaguzi bali uhuni.
 
Mimi ni CHADEMA lakini kwa suala hili chama kinazingua sana, kuna haja gani ya kuhangaika na mtu aliyetangulia kwa Mungu?
 
Wewe una hoja ila hata kama wafuasi wa magufuli wasingekuwa na chaguo chadema wangekuwa kwenye position nzuri sana kujaza hilo gap walipaswa kuja na majibu yanayopwaya sasa na si kumsengenya magufuli. Kwa akili yangu ya kawaida tu naamini Kwamba kwenye kampeni za 2025 ingawa amekufa bado atakuwa kiini kikuu cha mijadala mingi miongoni mwa wagombea

Labda wagombea wa sukuma gang ndio mtamtumia kuombea kura. CDM hawahitaji kuungwa mkono na sukuma gang yoyote. Kama angekuwa na ushawishi wa hivyo angechezea chaguzi kipindi chake akiwa rais?
 
Back
Top Bottom