Tuwekane sawa kwanza.
Maziwa yanasaidia kwenye sumu ingawa sio moja kwa moja.
Maziwa yana protini na ndani ya protini kuna amino acid.
Baadhi ya kazi za protini ni ukuaji, kurekebisha seli za mwili.
Pia protini inahusika katika chembe seli nyekundu za damu ambazo zinaunda haemoglobin yenye kazi kubwa ya kusafirisha oksijeni.
Kuna aina mbalimbali za sumu na hutegemea kiwango au dozi pamoja na mahali inapoweza kudhuru au kuleta madhara katika mwili.
Sumu huweza kuleta madhara katika seli, tishu, ogani, mfumo au kudhuru kiumbe moja kwa moja.
Kwa sababu sumu ina athari inapoingia katika mwili hivyo basi njia moja wapo ya kusaidia mwili au seli ni matumizi ya protini kama virutubisho ambavyo vinapatikana katika maziwa pia.
Kwa hiyo inatarajiwa mtu anapotumia sumu ni muhimu pia kupata virutubisho vya protini.
Ingawa nakubaliana na wewe kuwa dhana ya maziwa kutumika kama antidote/kigeuza - sumu au kikata - sumu imekuwepo muda mrefu sana.
Mwisho tunaishi katika dunia iliyozungukwa na sumu sumu sumu kuanzia tunavyotumia, kunywa na kula hata hewa tunayovuta.
Pia ikumbukwe kuwa maziwa yana placebo effect ambayo ni chanya na inasaidia kuleta utulivu wa akili na mwili kwa muhanga aliyekunywa sumu kwa kuondoa hofu hasa katika huduma ya kwanza.