mushairizi
JF-Expert Member
- Nov 27, 2011
- 290
- 249
Mimi nadhani sio suala la kuona maana kuona hakuna maana kama hukushirikishwa katika kufikia uamuzi. Tunaona mambo mabovu yaliyoingiwa kwa vizazi vijavyo ambao watataabika na ulipaji wa mikopo hiyo. Kwa maoni yangu kabla ya jambo kuamuliwa na kuanza utejekezaji ushirikishwaji uwekwe wazi wananchi wajiamulie wenyewe kuliko kuletewa yaliyokwisha amuliwa na ambayo hata ukiona hakuna faida yoyoteNdugu zangu watanzania, wakati tunaendelea kujadili siasa za nchi yetu ni vema tuangalie serikali zilizopita na ya sasa kwa kuangalia namna ambavyo kumekuwa na tofauti katika utendaji wake wa mambo mbalimbali.
Leo hii napenda kuwauliza wenzetu wanaopenda kuweka ulimganyo wa utendaji wa serikali ya Magufuli n Samia. Labda tujiulize yafuatayo kuhusu serikali ya Magufuli ili tuilinganishe na hii iliyopo especially kwenye masuala ya mikopo inayolalamikiwa na mikataba;
Nani amewahi kuona mkataba wowote unajadiliwa Bungeni?
[emoji407]Nani amewahi kuona mkataba wa mkopo?
[emoji407]Nani amewahi kuona mkataba wa Stiegler’s Gorge, SGR, Bandari ya Bagamoyo?
[emoji407]Nani ameuona mkataba wa manunuzi ya Ndege?
[emoji406]Lini ripoti ya CAG imeongelea mikopo?
Tujihoji huku tukiangalia uwazi ambao umekuwepo sasa wakati wa kusainiwa hii mikataba.
I submit.
Sent from my TECNO LA7 using JamiiForums mobile app