Nani aliyetulaani wana wa mkoa wa Mara?

Nani aliyetulaani wana wa mkoa wa Mara?

Mkoa wote wa Mara, Wachagga, Wamaasai
Sio mkoa wote wa Mara, Singida na Manyara mbona hujataja. Kuna memba mmoja humu ametoa hoja ya msingi sana. Karne ya 21 vijana wa Tanzania wanajadili mikoa na ukabila!!!? Kweli tunajadili mambo madogo kama haya wenzetu wako kwenye nanotechnology, wanajadili masuala ya kitaifa sio ukabila, sio vyama, sio ushabiki kwa waliotufikisha hapa. Wanajadili mustakabali wa Taifa, wengi wetu humu ni waliopata bahati ya kusoma na kuwa na exposure japo kidogo. Wengi wenzetu hawakupata bahati hiyo ingawa walikuwa akili nzuri tu darasani. Sisi tunajadili fulani hazai, fulani katelekeza mtoto n.k. Ikifika masuala ya Kitaifa tunaingiza uvyama, ukabila na ukanda. Mwelekeo hakuna
 
Kuna wadada wawili humu bila shaka wana maumivu ya kuachwa na wanaume wa kikurya....kitu nachojua wakurya hatujawahi kupungukiwa na wanawake wazuri...sijazaliwa huko lakini kwa wakurya nao wajua hapa dar,wote wana wanawake wazuri halafu we don't care..kuvunja mahusiano kwetu simple tu..tuna sura ngumu &viburiiiii tunawaendesha wanawake wazuri tutakavyo halafu tunavunja mahusiano sasa Hilo beef lake sasa.Mapenzi yenyewe wanasema hatujui lakini wanawake wazuri tuna Nyota nao hatari.Sisi ukiachana na sisi lazima utuchukie sababu piga ua lazima tukuendeshe tutakavyo na uzuri wako mixer makofi wakati sijakuoa halafu mwisho wa siku nakuacha kwenye mataa...
Hahahahahaa yaani huo ndio ukweli mtupu mura sisi wasaghane hawatuendeshi hata kidogo akizingua anakula kibuti mwenzake anachukua siti...

Anabaki analialia tu
 
Sasa 'mura' kwa nini usiitaje tu moja kwa moja hiyo serikali kwa kuua viwanda ila comment yangu ndiyo umeiona kubebea bango la wananchi kuacha kulima kahawa..?
Kwani mnatumia vigezo gani kusema mkoa wa Mara uko nyuma kimaendeleo? mbona ndio hali halisi ya nchi hii?kuna mkoa usiokuwa na imani za kishirikina nchi hii? Hizo rasilimali kama madini zingewanufaishaje wana Mara kama zilikuwa mikononi mwa wageni? Wakati biashara ya sangara ikiwa kwenye peak wavuvi walikuwa wakiuza kilo moja kwa Sh 600 hadi 1000. Wenye viwanda wakichakata na kupeleka ulaya wanauza USD 20 kwa 1kg. Tarime tulikuwa tunalima kahawa sana, lakini chama kikuu cha ushirika (Mara cooperative union- MCU 1984) kwa kushilikiana na serikali wakakiua kwa kuwakopa wakulima kahawa bila kulipa, wakaacha kulima kwani huwa hatupendi upumbavu. Wilaya ya Rorya na Musoma vijijini ni wilaya zenye ardhi duni sana na walitegemea ziwa victoria (samaki hakuna) wamefaidi wahindi na wabongo wachache (Mawakala).
 
Mumuogope Mungu, mbona mnayoyaongea mimi mkurya (Mwireghi) wa kijiji cha Itiryo wilaya ya Tarime siyaoni? Unajua asili ya koo katika makabila mengi ya Tanzania? Unajua kwa nini tulikuwa na mapigano ya koo? unadhani ni chuki miongoni mwetu? wakulima na wafugaji wanvyopigana ni kwa sababu ni koo tofauti ndani ya kabila moja? Mbona wanaJF wanaparurana kila siku humu kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa tena kwa matusi mazito sana, wangekuwa wanaonana uso kwa uso si ingekuwa balaa. mbona waireghi, watimbaru, wanyabhasi na koo zingine tunaishi vizuri sana, tunaoana, tunafanya biashara pamoja tena kipindi hiki ambako wizi wa mifugo haupo kwani imeisha. Wakati mwingine ni vizuri kuchangia kitu ulicho na hakika nacho, si tu umezaliwa unasikia wakurya wakorofi na wewe unaamini hivyo hivyo, mambo yanabadilika sana. Tatizo la wakurya hawapendi longolongo akipewa ofisi walozoea misheni town wanakiona cha moto, na sisi wabongo wengi tulishazoea dili. Mwisho Wakurya ni miongoni mwa makabila mazuri na rahisi sana kuishi nao ukiacha matatizo machache kama ya domestic violence na haya yanaendela kupungua
Tena nyie Wairege ndio kumbavu kabisa, wabaguzi sana, ukienda pale Nyamwaga hakuna mnyabasi wala koo nyingine anafanyia biashara, ukifungua biashara hupati wateja, ukitembea vijijini vyenu huko ajenda sasa mnataka mbunge mwirege, hamjali hata uwakilishi wa Heche, nyie ndio mnaishi karne ya 20.
 
Sasa 'mura' kwa nini usiitaje tu moja kwa moja hiyo serikali kwa kuua viwanda ila comment yangu ndiyo umeiona kubebea bango la wananchi kuacha kulima kahawa..?
Sorry mkuu, kuna watu kwenye comments za mwanzoni walinitoa kwenye reli. Kahawa tuliacha watu wakaanza kulima bangi kupeleka kenya ukivuna mara moja unapaua nyumba ya bati mgongo wa tembo. Ingawa sijawahi jaribu hiyo biashara ila nilisomeshwa kwa kahawa shule za private miaka hiyo. ila kwa mkoa wa Mara watu wa Tarime ni wapambanaji sana kimaisha. Karibuni Tarime kwa Mh (Esther na Heche)
 
Tena nyie Wairege ndio kumbavu kabisa, wabaguzi sana, ukienda pale Nyamwaga hakuna mnyabasi wala koo nyingine anafanyia biashara, ukifungua biashara hupati wateja, ukitembea vijijini vyenu huko ajenda sasa mnataka mbunge mwirege, hamjali hata uwakilishi wa Heche, nyie ndio mnaishi karne ya 20.
Wasiojali ni wananchi au wanaCCM. Lengo la CCM kugawa jimbo la uchaguzi kuwa mawili halikutimia, ilikuwa hesabu ya kipumbavu kwelikweli. Sasa utalawalazimisha wanyabhasi wakakae Nyamwaga au Itiryo? mbona Nyamongo kuna mchanganyiko wote na hawapigani? Mbona sisi wengine tumeoa kwa watimbaru bila shida yoyote? kujadili ukanda, ukabila na koo ni utoto, mwisho tutaanza kujadili familia huku wanasiasa wakiendelea kututumia. Tujadili mambo ya msingi ya kitaifa bila kuingiza utoto na uvyama vinginevyo tutabaki kushabikia tu.
 
Usidanganye watu wakurya hawapo hivyo. Wakurya hawana tabia ya kuongelea kwapani. Lao ni ndio au hapana na hawabebi umbea Wala majungu. Hao unao wasema wametoka Tarime au? Think again!
Ni kweli unajua kwa sababu ya umaarufu wa wakurya, kuna watu wanafikiri kuwa kila anayetoka Mara ni mkurya. Hata mtu akisema anatokea Musoma wao wanajua ni mkurya.
 
Tena nyie Wairege ndio kumbavu kabisa, wabaguzi sana, ukienda pale Nyamwaga hakuna mnyabasi wala koo nyingine anafanyia biashara, ukifungua biashara hupati wateja, ukitembea vijijini vyenu huko ajenda sasa mnataka mbunge mwirege, hamjali hata uwakilishi wa Heche, nyie ndio mnaishi karne ya 20.
Wairege wana tabia ya ubaguzi sana nimekaa nyamwaga mriba kemendi ni shida tupu
 
Jamaa huwa hawana ubinafsi na choyo.ndio maana hawakuipendelea mikoa yao.lkn la pili hawana maarifa ya kimaendeleo hataka wanakuwa na pesa huishia kujenga nyumba basi.utakuta mkurya nyumba nzuri lkn mpangilio ndani ya nyumba unakuwa mbaya au sebule haina muonekano mzuri.ila ni watu poa sana
 
Back
Top Bottom