Nani aliyetulaani wana wa mkoa wa Mara?

Nani aliyetulaani wana wa mkoa wa Mara?

Daaa!! weee! jamaaa!! midevu yooote hiyo kuumbe weye ni ''Yego Mwamba?'' Huwezi kudadavua hivi bana weee!! sasa fanyeni hivi nawapa dawa changanyeni DAMU nzuri za , kutoka, moshi, arusha! kenya si karibu tu hapo? sukuma land, uone!!
Aseee man hebu jifunze kwa kuishi maeneo tofauti tofauti nchini.

Arusha kuna wajita wengi tu walioOA wachaga, wajaluo, wapale na hata lile kabila pendwa kutoka hapa karatu ila sasa, hamna kitu aseee, ni bora aliyeoa mchina.

Tatizo siyo kuOA kabila flani, mwana hata wachaga wanaoana wao kwa wao but hakuna ubinafsi, ila hii ni roho mbaya kama waliyo nayo ndg zangu wa hapa pemba kwa wageni mnaokuja.
 
Mkoa wa Mara ni miongoni mwa mikoa ambayo imebahatika kutoa viongozi wengi katika Serikali zote za kuanzia muasisi wa taifa hili.Lakini ni kati ya mikoa ambayo maendeleo yake yako nyuma sana, ukifatilia kiundani ni kuwa hata viongozi ambao walipewa nyadhifa mbalimbali wao kwa wao hawaelewani bila kujali itikadi zao za vyama.

Kwa mfano Wasira na Jaji Warioba ni watu wasiopikika chungu kimoja japo wote wako ccm. Mwanasheria mkuu aliyestafu Jaji Welema na Mbunge Nimrod Mkono na Pro ,Mhongo ni maadui na uhasama huu unatokana na masilahi,baada ya kuchaguliwa Mhongo kuwa waziri wa nishati kwa kushirikiana na Mwanasheria mkuu Jaji Welema walikata mirija ya ulaji ambayo Nimrod mkono alikuwa analipwa kwenye kampuni yake ya uwanasheria kutokana na lile sakata la Dowas.

Mkono nae nae akaamua kuwalipua kwa kumpa documents Kafulila na kuwakomalia mbugeni na kusababisha Mhongo,Eriakim Maswe na Welema kupoteza nafasi.

Ninachomaanisha hapa ni kuwa viongozi kutoka mkoa wa Mara bila kujali itikadi zao ni watu ambao hawawezi kukakaa meza moja na kuzungumzia matatizo ya Mara kwa sababu wao kwa wao hawapendani.

Ni mji ambao hata miundombinu yake ni shida pamoja na kuwa na ziwa victoria lkn maji bado ni shida hasa kwa wakazi wa nje kidogo ya mji, Ukienda makao mkuu ya wilaya ya Serengeti mji wa Mugumu huwezi amini palivyo choka na wakati wako karibu na hifadhi.

Wakuu wa kaya nao wameususa kuanzia awamu ya Jk na sasa JPM ndio hana hbr kabisa na mkoa wa Mara.

Tupatiwe fursa hata viwanda vilivyokuwepo vifanye kazi pamoja na kuwa na chuo kikuu ,kwani chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere ni jina tu hakuna kinachoendelea.
@Gentamycin
 
Binafsi nipo musoma kikazi huu mwez wa 2 sasa lakini mazingira ya musoma mjini naona walau yana unafuu sio kama manispaa nyingine
Kama tabora songea sumbawanga lindi mtwara babati

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom